Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Swali: Baada ya kongamano la kumbukumbu ya miaka 10 ya Mwalimu Nyerere, baadhi ya viongozi wamelaani majadiliano, na hata kuwaita majina mabaya baadhi ya washiriki. Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba alikwenda mbali zaidi kwa kuwaita wehu. Uliyapokeaje maoni hayo?
Jibu: Sisi tumesikia matusi aliyotoa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, lakini hayatunyimi usingizi. Makamba si Waziri Mkuu wa Rais (Jakaya) Kikwete, lakini inaonekana anatumia muda mrefu sana kuzungumzia mambo ya Serikali badala ya kujishughulisha na mambo ya chama.
Kwa muda sasa, kumetokea maneno ya kubeza, kukejeli, matusi kila baadhi yetu tunapozungumzia mambo ya msingi ya kitaifa na hayo yametokea, yamesemwa kutoka Makao Makuu ya Chama, si kutoka serikalini.
Oktoba, ninyi waandishi wa habari mlituhoji mimi na Salim (DK. Salim Ahmed Salim) ili tutoe maoni yetu kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 10 tangu Mwalimu alipotutoka.
Baada ya kusema tuliyosema alitokea mtu makao makuu ya chama akatutukana. Hakushughulika na hoja tulizotoa, sisi tulizungumzia mambo mawili makubwa.
Moja, ni kuporomoka kwa maadili katika Taifa letu, la pili mmomonyoko kwenye umoja wa Taifa, lakini tulitukanwa kwamba sisi ni watu tunaomwandama Rais Kikwete.
Lakini mwezi huo huo, Rais Kikwete akahutubia Taifa kutokea Butiama akazungumzia mambo yale tuliyozungumza tena kwa ufasaha zaidi kuonyesha kwamba ni matatizo kwenye nchi.
Alizungumzia kuporomoka kwa maadili, hatari inayoonekana kwenye kusambaratika kwa umoja wetu. Alizungumzia rushwa, akazungumzia ufisadi. Ni yale yale tuliyokuwa tumeyasema. Tulifarijika, tukapumua tukaona kumbe Rais wetu anaelewa haya matatizo.
Sasa wakati ule tumetukanwa kulikuwa na reaction ya watu mbalimbali baadhi walituambia kwamba yule kijana aliyesema alikuwa ametumwa na Makamba ili atutukane, sisi hatukuamini.
Kwa sababu ni huyo huyo alikuwa amesema maneno kama hayo huko nyuma sasa tukaambiwa amekuwa anatumwa, hatukuamini.
Sasa imekuja hii. Wote waliokuwa kwenye kongamano wanajua yaliyozungumzwa na katika majumuisho hayo inaonyesha yaliyozungumzwa ni mambo ya msingi na yamezungumzwa na watu wengi pale, tena kwa makini kabisa, na utaona katika majumuisho kuna sehemu nyingi wanatambua juhudi za Serikali.
Kongamano limetambua juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya madini, lakini wametoa ushauri namna ya kuboresha zaidi. Wametambua juhudi za Serikali kuhusu umiliki wa ardhi, lakini wamesema juhudi zaidi zinahitajika. Wametambua juhudi za Serikali katika kuboresha elimu, lakini wanasema juhudi zaidi zinahitajika.
Lakini kubwa zaidi walizungumza sana kuhusu kuporomoka kwa maadili na dalili za kusambaratisha umoja wetu. Sasa haya ni mambo ya msingi na kama nilivyosema Rais mwenyewe alikwishayatambua.
Hatuoni ni kosa gani ambalo tumefanya kwa kuzungumza haya mambo. Jana (Desemba 6, 2009), nilikuwa kanisani kwetu (St. Alban, Anglikana - Dar es Salaam) kulikuwa na kumbukumbu ya miaka 75, mgeni rasmi ilikuwa awe Waziri Mkuu lakini kwa bahati mbaya akawa amesafiri kwenda Vienna kwa hiyo akamtuma Waziri Marmo (Philip Marmo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Bunge) kusoma hotuba yake, ilikuwa ni hotuba ya Waziri Mkuu iliyosomwa na Waziri Marmo.
Na sehemu ya hotuba hiyo inasema ifuatavyo; Kama nilivyoeleza Tanzania ina watu wapatao milioni 40. Watu hawa wana viwango tofauti vya mapato na hili linaeleweka. Hatuwezi kuwa na mapato sawa.
Tatizo linakuja pale ambapo tofauti ya kipato inapokuwa kubwa miongoni mwa makundi katika jamii. Lakini tatizo hili linazidi kuwa kubwa pale ambapo tofauti ya kipato inapokuwa kubwa miongoni mwa makundi katika jamii.
Lakini tatizo hili linazidi kuwa kubwa pale ambapo ukubwa wa tofauti hiyo unapoongezeka. Madhara ya ongezeko hilo mnayafahamu kwani kuna hatari ya matajiri wachache kuendesha maisha ya masikini walio wengi kwa njia ambayo itazidi kuwaongezea utajiri huku ikiwadidimiza zaidi masikini.
Si ajabu matajiri hao wachache wakawa ndio wanaoendesha vyama vya siasa, Serikali, Mahakama, Bunge, Makanisa, Misikiti n.k. Katika hali hiyo Taifa halina usalama.
Hivyo hatuna budi kuwa na misingi inayopunguza tofauti kati ya masikini na tajiri. Kama serikali tunazo njia mbalimbali tunazotumia kupunguza tofauti hiyo. Lakini ninaamini madhehebu ya dini nayo yana jukumu la kufanya.
Licha ya kuchukua tahadhari yasiendeshwe kwa matakwa ya matajiri hao, yana jukumu la kuona na kuhakikisha kuwa vyanzo vyanzo vya utajiri wa waumini wao ni vya haki na havitokani na mapato haramu au kuvunja amri za Mungu.
Hivyo, ningependa kuwaomba viongozi wa dini kushirikiana na mihimili yote ya dola ili kupunguza kuongezeka kwa tofauti ya kipato kati ya matajiri na masikini kwa kuwa mwisho wake si mwema, anahitimisha kunukuu hotuba ya Waziri Mkuu na kuendelea kusema;
Sasa haya maneno sasa haya maneno ya Waziri Mkuu hayana tofauti kabisa na yale yaliyozungumzwa katika kongamano. Tulichoona hapa ni kwamba Serikali kama Serikali inasikiliza ushauri. Rais amewahi kuyasema na Waziri Mkuu anayasema.
Na kongamano lilikuwa linaishauri Serikali, kama Serikali haina tatizo na hayo yaliyosema huko mheshimiwa Makamba ana matatizo gani mpaka atutukane kwamba sisi ni wehu na wahuni.
Uongozi ni kuonyesha njia, mheshimiwa Makamba ni kiongozi wa ngazi ya juu katika chama, ndiye mtendaji mkuu na ukiwa kiongozi mwenye madaraka lazima uchunge lugha yako.
Lakini tumeona kwa muda mrefu mheshimiwa Makamba lugha yake ya kawaida ni kukebehi, kubeza na kutukana. Sasa anatoa dira gani kwa viongozi wengine na wananchi kwa ujumla.
Kwa sababu wananchi na viongozi wengine watafuata mwelekeo wa viongozi wakubwa sasa kama kiongozi wetu wa chama lugha yake ni hiyo, wengine watafuata.
Na ndiyo sababu unaona siku hizi kebehi, kubeza, matusi kati ya viongozi imekuwa ni jambo la kawaida, viongozi wanatukanana. Katika maneno yake aliyosema hakugusia hoja za msingi na ndiyo inavyokuwa wakati wote tukisema, hawagusi hoja.
Kongamano limesema; maadili yameporomoka, Makamba anatukana bila kusema kama maadili yameporomoka au hayakuporomoka vivyo hivyo kuhusu hatari tunaziona zinazohatarisha umoja wetu kama ubaguzi huu wa kimatabaka, ubaguzi wa kikabila, ubaguzi wa kidini, ubaguzi wa kimtandao.
Haya ndiyo tunayosema, atuambie je, ni nini ambacho tunasema hapa ni kibaya kwa Serikali yetu. Sisi haya mawazo ama ushauri tunautoa mara nyingi tu kwa wanaohusika, tunazungumza kwa mawaziri mara nyingi tu, tunatoa hoja nao wanatoa hoja.
Baadhi ya nyakati wanaona hoja zetu na baadhi ya wakati tunaona hoja zao, ndiyo njia ya kushauriana katika uongozi, lakini wakati wote tunaheshimiana.
Mawaziri wengi wanatuheshimu sana, tena sana, hata pale ambapo tunatofautiana mawazo heshima ipo. Hawatutukani, hawatukeji, hawatubezi. Na hiyo ni pamoja na Rais.
Rais pamoja na cheo chake anaheshimu sana watu. Anatuheshimu sana sisi wazee. Hatutukani. Hatubezi, hata pale ambapo tunatofautiana mawazo, Rais anatuheshimu sana, nasi tunamheshimu.
Na viongozi wengi wa chama ni vivyo hivyo. Katika kongamano lile kulikuwa na viongozi wengi wa ngazi za juu katika CCM. Walikuwapo wajumbe wa Halmashauri Kuu.
Ukiwachukua Dk. Salim mjumbe wa NEC, Frederick Sumaye, Abdulrahman Kinana, George Mkuchika wote ni wajumbe. Mkuchika amekaa siku ya mwisho tangu asubuhi hadi jioni amesikia na kuzungumza na wanakongamano kwa heshima kabisa.
Hawa hawana matatizo na walikuwapo pale, hujawasikia wametoka wakatoa matamko. Anakuja mheshimiwa Makamba anaita waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wake mwenyewe alikuwapo kwenye kongamano lakini kwenye mazungumzo na waandishi wa habari hakuwapo. Huyu (Mkuchika) ndiye aliyekuwa anajua nini kimetokea kule.
Angeshauriana naye angejua nini kimetokea kule, lakini inaonekana mheshimiwa Makamba yeye ana kundi lake ambalo lina lenga watu fulani fulani, wakisema chochote basi lile kundi linakuja kuwatukana.
Ana vijana wake pale makao makuu na ana mmoja mikoani anaitwa Mgeja, Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga. Tumeona aliyosema na hata wakati ule ambapo nilisema nikashambuliwa na yeye alijiunga humo na safari hii naye ameingia tena humo.
Safari hii anasema kama yale aliyosema mwanzo anasema hivi (anasoma gazeti lililomnukuu Mgeja); kauli ya Makamba inaungwa mkono na Mwenyekiti wa CCM, Hamis Mgeja ambaye ameiambia Mwananchi Jumapili kwamba wanaopiga kelele wanasukumwa na chuki binafsi tangu makundi yao yaliposhindwa kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.
Alieleza kuwa Dk. Harrison Mwakyembe alikuwa kundi la Mark Mwandosya, Anna Kilango alikuwa kundi la John Malecela, Christopher ole Sendeka alikuwa kundi la Sumaye na wamekuwa wakiendelea kuwapotosha Watanzania kwa makusudi.
Alisema kuwa ni wazi kwamba Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku na Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, ambao hata sasa wakati Rais anaelekea kumaliza kipindi cha miaka mitano hawajawahi kuona wala kuzungumzia zuri hata moja la awamu ya nne, walikuwa upande wa Salim hivyo chuki yao inazidi kuwatafuna.
Huyo ni Mgeja anasema anatufahamu mimi simfahamu. Sikuwahi kufanya naye kazi, sijui anatufahamu vipi.
Watu waliogombea mwaka 2005, Malecela, Sumaye, Mwandosya, Salim. Kwa hiyo wale wote anaofikiria kwamba waliwaunga mkono wagombea hao wakisema chochote ni ovyo kwake, wanasema tuna chuki na wivu.
Hawa wakiongozwa na Mh. Makamba ndio wanaoleta mgawanyiko katika chama, wao ndio wanakundi. Akisema mtu ambaye hayuko kwenye kundi lao wala hawachunguzi waone kilichosemwa hoja iliyotolewa hapana, ni kutukana.
Rais Kikwete akisema nchi inakabiliwa na matatizo ya kuporomoka kwa maadili, ubaguzi, rushwa na ufisadi ni sawa. Salim na Warioba wakisema hayo hayo wanaitwa watu wenye chuki na wivu.
Waziri Mkuu Pinda akisema kwamba tofauti ya kipato kati ya matabaka ni hatari kwa usalama wa taifa Makamba anaona ni sawa. Lakini maneno hayo hayo yakisemwa na Salim na Warioba wanaonekana ni wehu na wahuni.
Maneno hayo hayo yamesemwa kwenye makongamano na semina nyingi, Bungeni na mahali pengine lakini Mh. Makamba hakuita waandishi wa habari. Lakini yaliposemwa kwenye kongamano la Taasisiya Mwalimu Nyerere ameita waandishi wa habari na kutukana.
Mheshimiwa Makamba anasema Rais Kikwete ni zaidi ya CCM, Rais ni popular kwa wananchi sawa lakini ukifika mahali Katibu Mkuu wa chama anasema mtu mmoja ni zaidi ya chama ujue ameshindwa kufanya kazi, kwa hiyo hadhi ya chama imeporomoka.
Makamba sasa ndiye analeta mgawanyiko ndani ya chama, hawa wote anaowasema Rais hana matatizo nao, Rais alikwisha kuondokana na hili, anafanya kazi nao vizuri tu.
Kwa sababu kama unasema wale waliowaunga mkono wagombea (2005) wana chuki maana yake unasema hawa waliogombea ndiyo wana chuki.
Ukisema mimi nina chuki kwa sababu nilimuunga mkono Salim, maana yake Salim ana chuki. Rais hana chuki na watu hawa. Kuna watu ambao hawakumuunga mkono kwenye uchaguzi na anafanya nao kazi serikalini hata Mwandosya yuko serikalini.
Rais ana wasaidizi wanaojitahidi, ukimwoma Makamu wake (Dk. Ali Mohamed Shein) anafanya kazi. Anazunguka nchi hii kujaribu kusaidia utekelezaji wa sera na anatoa maonyo mengi tu kwa mambo ambayo anaona hayako sawa.
Ukimwona Waziri Mkuu (Pinda) anafanya kazi kwa uwezo wake kwa commitment kubwa kabisa, na hawa wanasikiliza ushauri wanaopewa. Hawagombani na mtu, wanaheshimu watu, hawatukani watu.
Makamba ameacha kufanya kazi ya chama ya kuimarisha chama, ya kuunganisha chama anajifanya yeye ndiye Waziri Mkuu wa nchi hii wa kumtetea Rais na kumtetea Rais ni kuwatukana watu, kuwabeza watu na kuwakejeli watu.
Uongozi wa chama umevurugika, viongozi wanalaumiana, wanatukanana na huyu ndiye mtendaji mkuu wa chama badala ya kufanya jitihada za kuunganisha chama anaendelea na jitihada za kugawanya chama. Hafanyi kazi ya chama, anafanya kazi ya kundi, anaeneza chuki. Yeye na wenzake ndio wanaajenda ya chuki ambayo ni hatari sana kwa usalama wa CCM na nchi.
Kwa hiyo, kama nilivyosema, tumesikia matusi yake akae huko akifikiri sisi ni wehu na wahuni. Haitunyimi usingizi. Nchi hii ni yetu sote, tuna wajibu wa kutoa maoni yetu, kutoa ushauri wetu bila woga wowote na hayo matusi yake hayatatuzuia kuendelea kutoa ushauri wa ndani au wa hadharani. Tutaendelea kwa sababu tunaitakia nchi hii mema.
Yakitokea madhara tutahusika, sisi, watoto wetu na wajukuu zetu. Tunakata Tanzania ibaki nchi ya umoja, amani, utulivu na mshikamano. Tukiona kitu chochote kinahatarisha hayo, tutasema.
Swali: Kuhusu suala la kundi. Rais alikuwa na kundi lake aliposhinda akalivunja na makundi mengine yametangazwa kuvunjwa, unazungumzia kundi gani?
Jibu: Mimi sijui, ninachosema Rais hana kundi sasa kwa jinsi tunavyomuona. Hana kundi. Kuna mmoja aliniletea ujumbe hapa na kuna wenzangu wamepata ujumbe wa aina hiyo.
Wanasema hivi mnafikiri Makamba anasema hivi bila baraka (za Rais) za viongozi wake? Kumbe Mimi nasema viongozi wake hawahusiki na haya anayosema (matusi) ni yake kwa sababu Rais tunamwelewa.
Tunamjua, tumekuwa naye pamoja. Tunajua heshima anayotupa, hatukani, tunamwelewa Rais aliacha yale makundi, kundi lake. Ukiona katika chama na Serikali amewachukua watu ambao hawakuwa katika kundi lake, anao anafanya kazi nao vizuri.
Ukianza na makao makuu ya chama pale, viongozi wa ngazi za juu si wote waliomuunga mkono wakati wa uchaguzi. Ukiingia serikalini ni hivyo hivyo, kwa hiyo sisi tunaamini hii Makamba anatumia jina la Rais kwa madhumuni yake mwenyewe, sasa hatujui anayemtumikia ni nani.
Unaona anakumbatia na kutetea sana matajiri, lakini umeona Waziri Mkuu alivyosema ni tofauti kabisa.
Swali: Ni ushauri wake kuhusu uongozi wa chama chenu?
Jibu: Kama ninavyosema na kama ilivyokuwa kwenye kongamano, hatutaki kuzungumzia watu, tunazungumzia hoja. Kwenye kongamano tumesema maadili yameporomoka, umoja wetu unahatarishwa na ubaguzi. Haya tumeyasema na tumemwambia Rais aelewe hali hii achukue maamuzi magumu, au serikali kwa ujumla ichukue maamuzi magumu tusiingie hatarini.
Maana yake nini? Maana yake tunamwambia Rais hali iko hivi inahitajika maamuzi magumu, lakini kwa kusema hivyo tunamwambia ukifanya uamuzi unaungwa mkono, sisi tunamuunga mkono ajue wananchi wanamuunga mkono.
Kwa hiyo aone hatua zozote anazoweza kuchukua ili turekebishe hali hiyo. Ni kweli tunataka kumsaidia Rais na moja ya namna ya kumsaidia ni kumuonyesha concern kwamba kuna mambo haya yanahitaji uamuzi, sasa ukiyafanya tunakuunga mkono.
Swali:Kuna hoja kwamba, wakati wenu mkiwa uongozini mlifanya nini?
Jibu: Wakati wowote ule katika nchi yoyote ile, katika jitihada za kuleta maendeleo kutakuwa na mafanikio na matatizo. Nilimsikia mheshimiwa Makamba akisema kwamba matatizo ya sasa yanayoikabili awamu ya nne chanzo chake ni awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu.
Maana yake anasema zile awamu hazikufanya vizuri, ni mawazo yake sigombani kama ana mawazo yake. Lakini mafanikio tunayojivunia yameletwa na nani?
Tunaposema nchi hii ni ya umoja wa kitaifa yenye amani, utulivu mshikamano nani alileta hayo? Tunaposema maadili yameporomoka maana yake tulikuwa na maadili mazuri, nani aliyaleta hayo?
Hakuna anayebisha kwamba kwenye hizo awamu za kwanza mwanzo kuna makosa yalifanywa lakini pia kuna mafanikio makubwa yaliyoletwa hiyo ni kawaida katika maendeleo ya nchi.
Kama mheshimiwa Makamba anataka kutuambia kwamba awamu ya sasa ni mazuri tu hakuna makosa yanayotokea na kama yapo yametokana na hao walioongoza mwanzoni, basi.
Maana hawa wa mwanzoni kwa kuwa wametoka lakini naye alikuwapo kuanzia awamu ya kwanza mpaka sasa. Yeye anaweza kusema kila alipokaa hakukutokea matatizo na kama yalitokea ilikuwa mwiko kuyazungumzia? Anapenda sana sifa. Makamba alikuwa anawasifu sana viongozi waliopita. Sasa anawalaumu. Hivi Makamba anamsifu kiongozi toka moyoni kwake au ni kutekeleza agenda binafsi. Kumsaidia kiongozi wako siyo lazima kumsifu wakati wote bali pia kutoa ushauri mgumu.
Chanzo: Raia Mwema
Jibu: Sisi tumesikia matusi aliyotoa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, lakini hayatunyimi usingizi. Makamba si Waziri Mkuu wa Rais (Jakaya) Kikwete, lakini inaonekana anatumia muda mrefu sana kuzungumzia mambo ya Serikali badala ya kujishughulisha na mambo ya chama.
Kwa muda sasa, kumetokea maneno ya kubeza, kukejeli, matusi kila baadhi yetu tunapozungumzia mambo ya msingi ya kitaifa na hayo yametokea, yamesemwa kutoka Makao Makuu ya Chama, si kutoka serikalini.
Oktoba, ninyi waandishi wa habari mlituhoji mimi na Salim (DK. Salim Ahmed Salim) ili tutoe maoni yetu kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 10 tangu Mwalimu alipotutoka.
Baada ya kusema tuliyosema alitokea mtu makao makuu ya chama akatutukana. Hakushughulika na hoja tulizotoa, sisi tulizungumzia mambo mawili makubwa.
Moja, ni kuporomoka kwa maadili katika Taifa letu, la pili mmomonyoko kwenye umoja wa Taifa, lakini tulitukanwa kwamba sisi ni watu tunaomwandama Rais Kikwete.
Lakini mwezi huo huo, Rais Kikwete akahutubia Taifa kutokea Butiama akazungumzia mambo yale tuliyozungumza tena kwa ufasaha zaidi kuonyesha kwamba ni matatizo kwenye nchi.
Alizungumzia kuporomoka kwa maadili, hatari inayoonekana kwenye kusambaratika kwa umoja wetu. Alizungumzia rushwa, akazungumzia ufisadi. Ni yale yale tuliyokuwa tumeyasema. Tulifarijika, tukapumua tukaona kumbe Rais wetu anaelewa haya matatizo.
Sasa wakati ule tumetukanwa kulikuwa na reaction ya watu mbalimbali baadhi walituambia kwamba yule kijana aliyesema alikuwa ametumwa na Makamba ili atutukane, sisi hatukuamini.
Kwa sababu ni huyo huyo alikuwa amesema maneno kama hayo huko nyuma sasa tukaambiwa amekuwa anatumwa, hatukuamini.
Sasa imekuja hii. Wote waliokuwa kwenye kongamano wanajua yaliyozungumzwa na katika majumuisho hayo inaonyesha yaliyozungumzwa ni mambo ya msingi na yamezungumzwa na watu wengi pale, tena kwa makini kabisa, na utaona katika majumuisho kuna sehemu nyingi wanatambua juhudi za Serikali.
Kongamano limetambua juhudi za Serikali katika kuboresha sekta ya madini, lakini wametoa ushauri namna ya kuboresha zaidi. Wametambua juhudi za Serikali kuhusu umiliki wa ardhi, lakini wamesema juhudi zaidi zinahitajika. Wametambua juhudi za Serikali katika kuboresha elimu, lakini wanasema juhudi zaidi zinahitajika.
Lakini kubwa zaidi walizungumza sana kuhusu kuporomoka kwa maadili na dalili za kusambaratisha umoja wetu. Sasa haya ni mambo ya msingi na kama nilivyosema Rais mwenyewe alikwishayatambua.
Hatuoni ni kosa gani ambalo tumefanya kwa kuzungumza haya mambo. Jana (Desemba 6, 2009), nilikuwa kanisani kwetu (St. Alban, Anglikana - Dar es Salaam) kulikuwa na kumbukumbu ya miaka 75, mgeni rasmi ilikuwa awe Waziri Mkuu lakini kwa bahati mbaya akawa amesafiri kwenda Vienna kwa hiyo akamtuma Waziri Marmo (Philip Marmo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Bunge) kusoma hotuba yake, ilikuwa ni hotuba ya Waziri Mkuu iliyosomwa na Waziri Marmo.
Na sehemu ya hotuba hiyo inasema ifuatavyo; Kama nilivyoeleza Tanzania ina watu wapatao milioni 40. Watu hawa wana viwango tofauti vya mapato na hili linaeleweka. Hatuwezi kuwa na mapato sawa.
Tatizo linakuja pale ambapo tofauti ya kipato inapokuwa kubwa miongoni mwa makundi katika jamii. Lakini tatizo hili linazidi kuwa kubwa pale ambapo tofauti ya kipato inapokuwa kubwa miongoni mwa makundi katika jamii.
Lakini tatizo hili linazidi kuwa kubwa pale ambapo ukubwa wa tofauti hiyo unapoongezeka. Madhara ya ongezeko hilo mnayafahamu kwani kuna hatari ya matajiri wachache kuendesha maisha ya masikini walio wengi kwa njia ambayo itazidi kuwaongezea utajiri huku ikiwadidimiza zaidi masikini.
Si ajabu matajiri hao wachache wakawa ndio wanaoendesha vyama vya siasa, Serikali, Mahakama, Bunge, Makanisa, Misikiti n.k. Katika hali hiyo Taifa halina usalama.
Hivyo hatuna budi kuwa na misingi inayopunguza tofauti kati ya masikini na tajiri. Kama serikali tunazo njia mbalimbali tunazotumia kupunguza tofauti hiyo. Lakini ninaamini madhehebu ya dini nayo yana jukumu la kufanya.
Licha ya kuchukua tahadhari yasiendeshwe kwa matakwa ya matajiri hao, yana jukumu la kuona na kuhakikisha kuwa vyanzo vyanzo vya utajiri wa waumini wao ni vya haki na havitokani na mapato haramu au kuvunja amri za Mungu.
Hivyo, ningependa kuwaomba viongozi wa dini kushirikiana na mihimili yote ya dola ili kupunguza kuongezeka kwa tofauti ya kipato kati ya matajiri na masikini kwa kuwa mwisho wake si mwema, anahitimisha kunukuu hotuba ya Waziri Mkuu na kuendelea kusema;
Sasa haya maneno sasa haya maneno ya Waziri Mkuu hayana tofauti kabisa na yale yaliyozungumzwa katika kongamano. Tulichoona hapa ni kwamba Serikali kama Serikali inasikiliza ushauri. Rais amewahi kuyasema na Waziri Mkuu anayasema.
Na kongamano lilikuwa linaishauri Serikali, kama Serikali haina tatizo na hayo yaliyosema huko mheshimiwa Makamba ana matatizo gani mpaka atutukane kwamba sisi ni wehu na wahuni.
Uongozi ni kuonyesha njia, mheshimiwa Makamba ni kiongozi wa ngazi ya juu katika chama, ndiye mtendaji mkuu na ukiwa kiongozi mwenye madaraka lazima uchunge lugha yako.
Lakini tumeona kwa muda mrefu mheshimiwa Makamba lugha yake ya kawaida ni kukebehi, kubeza na kutukana. Sasa anatoa dira gani kwa viongozi wengine na wananchi kwa ujumla.
Kwa sababu wananchi na viongozi wengine watafuata mwelekeo wa viongozi wakubwa sasa kama kiongozi wetu wa chama lugha yake ni hiyo, wengine watafuata.
Na ndiyo sababu unaona siku hizi kebehi, kubeza, matusi kati ya viongozi imekuwa ni jambo la kawaida, viongozi wanatukanana. Katika maneno yake aliyosema hakugusia hoja za msingi na ndiyo inavyokuwa wakati wote tukisema, hawagusi hoja.
Kongamano limesema; maadili yameporomoka, Makamba anatukana bila kusema kama maadili yameporomoka au hayakuporomoka vivyo hivyo kuhusu hatari tunaziona zinazohatarisha umoja wetu kama ubaguzi huu wa kimatabaka, ubaguzi wa kikabila, ubaguzi wa kidini, ubaguzi wa kimtandao.
Haya ndiyo tunayosema, atuambie je, ni nini ambacho tunasema hapa ni kibaya kwa Serikali yetu. Sisi haya mawazo ama ushauri tunautoa mara nyingi tu kwa wanaohusika, tunazungumza kwa mawaziri mara nyingi tu, tunatoa hoja nao wanatoa hoja.
Baadhi ya nyakati wanaona hoja zetu na baadhi ya wakati tunaona hoja zao, ndiyo njia ya kushauriana katika uongozi, lakini wakati wote tunaheshimiana.
Mawaziri wengi wanatuheshimu sana, tena sana, hata pale ambapo tunatofautiana mawazo heshima ipo. Hawatutukani, hawatukeji, hawatubezi. Na hiyo ni pamoja na Rais.
Rais pamoja na cheo chake anaheshimu sana watu. Anatuheshimu sana sisi wazee. Hatutukani. Hatubezi, hata pale ambapo tunatofautiana mawazo, Rais anatuheshimu sana, nasi tunamheshimu.
Na viongozi wengi wa chama ni vivyo hivyo. Katika kongamano lile kulikuwa na viongozi wengi wa ngazi za juu katika CCM. Walikuwapo wajumbe wa Halmashauri Kuu.
Ukiwachukua Dk. Salim mjumbe wa NEC, Frederick Sumaye, Abdulrahman Kinana, George Mkuchika wote ni wajumbe. Mkuchika amekaa siku ya mwisho tangu asubuhi hadi jioni amesikia na kuzungumza na wanakongamano kwa heshima kabisa.
Hawa hawana matatizo na walikuwapo pale, hujawasikia wametoka wakatoa matamko. Anakuja mheshimiwa Makamba anaita waandishi wa habari, Naibu Katibu Mkuu wake mwenyewe alikuwapo kwenye kongamano lakini kwenye mazungumzo na waandishi wa habari hakuwapo. Huyu (Mkuchika) ndiye aliyekuwa anajua nini kimetokea kule.
Angeshauriana naye angejua nini kimetokea kule, lakini inaonekana mheshimiwa Makamba yeye ana kundi lake ambalo lina lenga watu fulani fulani, wakisema chochote basi lile kundi linakuja kuwatukana.
Ana vijana wake pale makao makuu na ana mmoja mikoani anaitwa Mgeja, Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga. Tumeona aliyosema na hata wakati ule ambapo nilisema nikashambuliwa na yeye alijiunga humo na safari hii naye ameingia tena humo.
Safari hii anasema kama yale aliyosema mwanzo anasema hivi (anasoma gazeti lililomnukuu Mgeja); kauli ya Makamba inaungwa mkono na Mwenyekiti wa CCM, Hamis Mgeja ambaye ameiambia Mwananchi Jumapili kwamba wanaopiga kelele wanasukumwa na chuki binafsi tangu makundi yao yaliposhindwa kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2005.
Alieleza kuwa Dk. Harrison Mwakyembe alikuwa kundi la Mark Mwandosya, Anna Kilango alikuwa kundi la John Malecela, Christopher ole Sendeka alikuwa kundi la Sumaye na wamekuwa wakiendelea kuwapotosha Watanzania kwa makusudi.
Alisema kuwa ni wazi kwamba Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku na Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, ambao hata sasa wakati Rais anaelekea kumaliza kipindi cha miaka mitano hawajawahi kuona wala kuzungumzia zuri hata moja la awamu ya nne, walikuwa upande wa Salim hivyo chuki yao inazidi kuwatafuna.
Huyo ni Mgeja anasema anatufahamu mimi simfahamu. Sikuwahi kufanya naye kazi, sijui anatufahamu vipi.
Watu waliogombea mwaka 2005, Malecela, Sumaye, Mwandosya, Salim. Kwa hiyo wale wote anaofikiria kwamba waliwaunga mkono wagombea hao wakisema chochote ni ovyo kwake, wanasema tuna chuki na wivu.
Hawa wakiongozwa na Mh. Makamba ndio wanaoleta mgawanyiko katika chama, wao ndio wanakundi. Akisema mtu ambaye hayuko kwenye kundi lao wala hawachunguzi waone kilichosemwa hoja iliyotolewa hapana, ni kutukana.
Rais Kikwete akisema nchi inakabiliwa na matatizo ya kuporomoka kwa maadili, ubaguzi, rushwa na ufisadi ni sawa. Salim na Warioba wakisema hayo hayo wanaitwa watu wenye chuki na wivu.
Waziri Mkuu Pinda akisema kwamba tofauti ya kipato kati ya matabaka ni hatari kwa usalama wa taifa Makamba anaona ni sawa. Lakini maneno hayo hayo yakisemwa na Salim na Warioba wanaonekana ni wehu na wahuni.
Maneno hayo hayo yamesemwa kwenye makongamano na semina nyingi, Bungeni na mahali pengine lakini Mh. Makamba hakuita waandishi wa habari. Lakini yaliposemwa kwenye kongamano la Taasisiya Mwalimu Nyerere ameita waandishi wa habari na kutukana.
Mheshimiwa Makamba anasema Rais Kikwete ni zaidi ya CCM, Rais ni popular kwa wananchi sawa lakini ukifika mahali Katibu Mkuu wa chama anasema mtu mmoja ni zaidi ya chama ujue ameshindwa kufanya kazi, kwa hiyo hadhi ya chama imeporomoka.
Makamba sasa ndiye analeta mgawanyiko ndani ya chama, hawa wote anaowasema Rais hana matatizo nao, Rais alikwisha kuondokana na hili, anafanya kazi nao vizuri tu.
Kwa sababu kama unasema wale waliowaunga mkono wagombea (2005) wana chuki maana yake unasema hawa waliogombea ndiyo wana chuki.
Ukisema mimi nina chuki kwa sababu nilimuunga mkono Salim, maana yake Salim ana chuki. Rais hana chuki na watu hawa. Kuna watu ambao hawakumuunga mkono kwenye uchaguzi na anafanya nao kazi serikalini hata Mwandosya yuko serikalini.
Rais ana wasaidizi wanaojitahidi, ukimwoma Makamu wake (Dk. Ali Mohamed Shein) anafanya kazi. Anazunguka nchi hii kujaribu kusaidia utekelezaji wa sera na anatoa maonyo mengi tu kwa mambo ambayo anaona hayako sawa.
Ukimwona Waziri Mkuu (Pinda) anafanya kazi kwa uwezo wake kwa commitment kubwa kabisa, na hawa wanasikiliza ushauri wanaopewa. Hawagombani na mtu, wanaheshimu watu, hawatukani watu.
Makamba ameacha kufanya kazi ya chama ya kuimarisha chama, ya kuunganisha chama anajifanya yeye ndiye Waziri Mkuu wa nchi hii wa kumtetea Rais na kumtetea Rais ni kuwatukana watu, kuwabeza watu na kuwakejeli watu.
Uongozi wa chama umevurugika, viongozi wanalaumiana, wanatukanana na huyu ndiye mtendaji mkuu wa chama badala ya kufanya jitihada za kuunganisha chama anaendelea na jitihada za kugawanya chama. Hafanyi kazi ya chama, anafanya kazi ya kundi, anaeneza chuki. Yeye na wenzake ndio wanaajenda ya chuki ambayo ni hatari sana kwa usalama wa CCM na nchi.
Kwa hiyo, kama nilivyosema, tumesikia matusi yake akae huko akifikiri sisi ni wehu na wahuni. Haitunyimi usingizi. Nchi hii ni yetu sote, tuna wajibu wa kutoa maoni yetu, kutoa ushauri wetu bila woga wowote na hayo matusi yake hayatatuzuia kuendelea kutoa ushauri wa ndani au wa hadharani. Tutaendelea kwa sababu tunaitakia nchi hii mema.
Yakitokea madhara tutahusika, sisi, watoto wetu na wajukuu zetu. Tunakata Tanzania ibaki nchi ya umoja, amani, utulivu na mshikamano. Tukiona kitu chochote kinahatarisha hayo, tutasema.
Swali: Kuhusu suala la kundi. Rais alikuwa na kundi lake aliposhinda akalivunja na makundi mengine yametangazwa kuvunjwa, unazungumzia kundi gani?
Jibu: Mimi sijui, ninachosema Rais hana kundi sasa kwa jinsi tunavyomuona. Hana kundi. Kuna mmoja aliniletea ujumbe hapa na kuna wenzangu wamepata ujumbe wa aina hiyo.
Wanasema hivi mnafikiri Makamba anasema hivi bila baraka (za Rais) za viongozi wake? Kumbe Mimi nasema viongozi wake hawahusiki na haya anayosema (matusi) ni yake kwa sababu Rais tunamwelewa.
Tunamjua, tumekuwa naye pamoja. Tunajua heshima anayotupa, hatukani, tunamwelewa Rais aliacha yale makundi, kundi lake. Ukiona katika chama na Serikali amewachukua watu ambao hawakuwa katika kundi lake, anao anafanya kazi nao vizuri.
Ukianza na makao makuu ya chama pale, viongozi wa ngazi za juu si wote waliomuunga mkono wakati wa uchaguzi. Ukiingia serikalini ni hivyo hivyo, kwa hiyo sisi tunaamini hii Makamba anatumia jina la Rais kwa madhumuni yake mwenyewe, sasa hatujui anayemtumikia ni nani.
Unaona anakumbatia na kutetea sana matajiri, lakini umeona Waziri Mkuu alivyosema ni tofauti kabisa.
Swali: Ni ushauri wake kuhusu uongozi wa chama chenu?
Jibu: Kama ninavyosema na kama ilivyokuwa kwenye kongamano, hatutaki kuzungumzia watu, tunazungumzia hoja. Kwenye kongamano tumesema maadili yameporomoka, umoja wetu unahatarishwa na ubaguzi. Haya tumeyasema na tumemwambia Rais aelewe hali hii achukue maamuzi magumu, au serikali kwa ujumla ichukue maamuzi magumu tusiingie hatarini.
Maana yake nini? Maana yake tunamwambia Rais hali iko hivi inahitajika maamuzi magumu, lakini kwa kusema hivyo tunamwambia ukifanya uamuzi unaungwa mkono, sisi tunamuunga mkono ajue wananchi wanamuunga mkono.
Kwa hiyo aone hatua zozote anazoweza kuchukua ili turekebishe hali hiyo. Ni kweli tunataka kumsaidia Rais na moja ya namna ya kumsaidia ni kumuonyesha concern kwamba kuna mambo haya yanahitaji uamuzi, sasa ukiyafanya tunakuunga mkono.
Swali:Kuna hoja kwamba, wakati wenu mkiwa uongozini mlifanya nini?
Jibu: Wakati wowote ule katika nchi yoyote ile, katika jitihada za kuleta maendeleo kutakuwa na mafanikio na matatizo. Nilimsikia mheshimiwa Makamba akisema kwamba matatizo ya sasa yanayoikabili awamu ya nne chanzo chake ni awamu ya kwanza, ya pili na ya tatu.
Maana yake anasema zile awamu hazikufanya vizuri, ni mawazo yake sigombani kama ana mawazo yake. Lakini mafanikio tunayojivunia yameletwa na nani?
Tunaposema nchi hii ni ya umoja wa kitaifa yenye amani, utulivu mshikamano nani alileta hayo? Tunaposema maadili yameporomoka maana yake tulikuwa na maadili mazuri, nani aliyaleta hayo?
Hakuna anayebisha kwamba kwenye hizo awamu za kwanza mwanzo kuna makosa yalifanywa lakini pia kuna mafanikio makubwa yaliyoletwa hiyo ni kawaida katika maendeleo ya nchi.
Kama mheshimiwa Makamba anataka kutuambia kwamba awamu ya sasa ni mazuri tu hakuna makosa yanayotokea na kama yapo yametokana na hao walioongoza mwanzoni, basi.
Maana hawa wa mwanzoni kwa kuwa wametoka lakini naye alikuwapo kuanzia awamu ya kwanza mpaka sasa. Yeye anaweza kusema kila alipokaa hakukutokea matatizo na kama yalitokea ilikuwa mwiko kuyazungumzia? Anapenda sana sifa. Makamba alikuwa anawasifu sana viongozi waliopita. Sasa anawalaumu. Hivi Makamba anamsifu kiongozi toka moyoni kwake au ni kutekeleza agenda binafsi. Kumsaidia kiongozi wako siyo lazima kumsifu wakati wote bali pia kutoa ushauri mgumu.
Chanzo: Raia Mwema