MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Kada Makamba alinukuliwa na gazeti la Msema Kweli Toleo Na. 040, hivi: "Makamba atoa zawadi ya nguruwe kwa shule".
Licha ya Mwandishi wa gazeti hilo kushangaa kwa kitendo hicho cha kada huyu kutoa nguruwe ambayo imeharamishwa na Mungu ni kudhihirisha yale Waislamu waliyokuwa na shaka nayo kuhusu Uislamu wake wakati anafanya mambo kinyume, sio kwa bahati mbaya, ila ni kwa jeuri na kibri ya utawala wa dunia.
Waislamu siku zote tumelalamika kuhusu kuzagaa kwa nguruwe na mabucha ya nyama ya nguruwe bila mafanikio, leo katudhihirishia kwamba kufuga nguruwe ni sera maalum. Vipi shule ambayo haifugi wewe uamue kutoa nguruwe halafu uhimize Waislamu kupeleka watoto wao waje. Siku wakipangiwa kusafisha zizi nani alaumiwe?
Waislamu tumepata madhila mengi juu ya huyu Bwana tangu awe mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Mtume (s.a.w.) anasema Muislamu wa kweli ni yule ambaye Waislamu wenzake wanasalimika na ulimi wake na vitendo vyake.
Yeye alikuwa mtu wa kwanza kuwatuhumu Waislamu kuiba bia wakati wa vurugu za Mwembechai, kasema tumekamata silaha Msikitini, kumbe ni vigingi vya jukwaa si hilo tu wakati anafungua Bia mpya aliwahi kusema kuwa Watanzania kunyweni Bia hii kwa wingi ili serikali ipate kodi kwa wingi.
NASAHA: Ndugu Luteni amedai mtu asitawaliwe na dini bali yeye aitawale dini; watu wanasema ukistajaabu ya Musa utaona ya Firauni, lakini mimi nasema "ukistaajabu ya Firauni utaona ya Musa, kwanza yeye sio kiongozi wa dini yoyote wala si kiongozi wa taasisi ya dini kwa hiyo fatwa yake inamrejea yeye mwenyewe.
Kama ni umaarufu wengi wameutafuta, lakini dunia wameiacha, uhai ni kama mvua, leo mafuriko kesho ukame, yeye adai tusitumie kigezo cha dini kujenga tofauti zetu.
Je, mbona hawaambii chama tawala wasitumie chama kujenga tofauti na vyama vingine mbona amekuwa mstari wa mbele kuviponda vyama vya upinzani. Je, yeye haoni anazidisha tofauti? Je, mbona kama ni msuluhishi mzuri mbona haendi kuchangia vyama upinzani.
Je, umoja unaletwa kwa kulazimishwa matakwa yako katika dini. Mungu anasema: "Na wanapokuwa na walioamini husema tumeamini na wanapokuwa peke yao kwa mashetani wao husema "Hakika sisi tu pamoja nanyi tunawacheza shere tu" (2:14)
Usifikiri Mungu ameghafirika na yale wanayoyafanya watu madhalimu Hakika Yeye anawangojea siku yatakapotoka macho.
Haki iko juu wala haikaliwi Mungu ndiye Mjuzi, mtambuzi, mwenye nguvu, mshindi, mfalme wa wafalme. Kwake hakuna kugeuka geuka haramu ni haramu na halali ni halali.
Licha ya Mwandishi wa gazeti hilo kushangaa kwa kitendo hicho cha kada huyu kutoa nguruwe ambayo imeharamishwa na Mungu ni kudhihirisha yale Waislamu waliyokuwa na shaka nayo kuhusu Uislamu wake wakati anafanya mambo kinyume, sio kwa bahati mbaya, ila ni kwa jeuri na kibri ya utawala wa dunia.
Waislamu siku zote tumelalamika kuhusu kuzagaa kwa nguruwe na mabucha ya nyama ya nguruwe bila mafanikio, leo katudhihirishia kwamba kufuga nguruwe ni sera maalum. Vipi shule ambayo haifugi wewe uamue kutoa nguruwe halafu uhimize Waislamu kupeleka watoto wao waje. Siku wakipangiwa kusafisha zizi nani alaumiwe?
Waislamu tumepata madhila mengi juu ya huyu Bwana tangu awe mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Mtume (s.a.w.) anasema Muislamu wa kweli ni yule ambaye Waislamu wenzake wanasalimika na ulimi wake na vitendo vyake.
Yeye alikuwa mtu wa kwanza kuwatuhumu Waislamu kuiba bia wakati wa vurugu za Mwembechai, kasema tumekamata silaha Msikitini, kumbe ni vigingi vya jukwaa si hilo tu wakati anafungua Bia mpya aliwahi kusema kuwa Watanzania kunyweni Bia hii kwa wingi ili serikali ipate kodi kwa wingi.
NASAHA: Ndugu Luteni amedai mtu asitawaliwe na dini bali yeye aitawale dini; watu wanasema ukistajaabu ya Musa utaona ya Firauni, lakini mimi nasema "ukistaajabu ya Firauni utaona ya Musa, kwanza yeye sio kiongozi wa dini yoyote wala si kiongozi wa taasisi ya dini kwa hiyo fatwa yake inamrejea yeye mwenyewe.
Kama ni umaarufu wengi wameutafuta, lakini dunia wameiacha, uhai ni kama mvua, leo mafuriko kesho ukame, yeye adai tusitumie kigezo cha dini kujenga tofauti zetu.
Je, mbona hawaambii chama tawala wasitumie chama kujenga tofauti na vyama vingine mbona amekuwa mstari wa mbele kuviponda vyama vya upinzani. Je, yeye haoni anazidisha tofauti? Je, mbona kama ni msuluhishi mzuri mbona haendi kuchangia vyama upinzani.
Je, umoja unaletwa kwa kulazimishwa matakwa yako katika dini. Mungu anasema: "Na wanapokuwa na walioamini husema tumeamini na wanapokuwa peke yao kwa mashetani wao husema "Hakika sisi tu pamoja nanyi tunawacheza shere tu" (2:14)
Usifikiri Mungu ameghafirika na yale wanayoyafanya watu madhalimu Hakika Yeye anawangojea siku yatakapotoka macho.
Haki iko juu wala haikaliwi Mungu ndiye Mjuzi, mtambuzi, mwenye nguvu, mshindi, mfalme wa wafalme. Kwake hakuna kugeuka geuka haramu ni haramu na halali ni halali.