Makamanda nguvu zimewaishia kabisa

Makamanda nguvu zimewaishia kabisa

Kwani ccm ina kundi la wahuni kama chadema!

Wahuni wa CCM huwajui? Kwa uchache tu:
  1. Mwenyekiti wenu wa CCM(T).
  2. Polepole-Uenezi na Uongo(CCM).
  3. Kinena-KM-CCM
  4. Job Ndugai-Spika.
  5. Makund*- RC Dar
  6. Lusind*-Kibajaj(MB-Mtera)
  7. Wewe mwenyewe.
  8. Lumuba +++++!!
screenshot_2017-11-29-22-34-28-1-png.641635

Iwapo CCM mnakubalika kama mnavodai ruhusuni basi KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI turudi kwenye Ballot Box then tutajua nani anakubalika kati ya CHADEMA na CCM....!
Napenda kukuhakikishia kwamba kama uwanja utakuwa sawa kwa kuleta Katiba mpya na Tume Huru CCM mtaondoka asubuhi na mapema!!!!!!
 
HA HA HA HA CHADEMA WAMEZIDIA UTAWALA HUU HALAFU WANAJIITA MAKAMANDA HUKU MWINGINE KAKIMBIA NA MKEWE USIKU WA KUAMKIA LEO ETI ANASINGIZIA KAVAMIWA
 
HA HA HA HA CHADEMA WAMEZIDIA UTAWALA HUU HALAFU WANAJIITA MAKAMANDA HUKU MWINGINE KAKIMBIA NA MKEWE USIKU WA KUAMKIA LEO ETI ANASINGIZIA KAVAMIWA
Yaani wanataka kutufanya wote akili zetu kama vijana wa ufipa!
 
Mengi yaliyoripotiwa na kutiwa chumvi ni uoga wa mbowe kutaka kuficha udhaifu wa chama kuangukia pua!

Sio suala la kuripotiwa, tumeona kwa macho yetu. Ule ulikuwa ni upuuzi wa hali ya juu. Hata Mbowe akisema atashiriki sisi wengine tutaendelea kuwataka wapinzani na wengine wanaomini faida za vyama vya upinzani wasiende kupiga kura. Bakini wanaccm mshinde kwa kishindo na upuuzi wenu uwe wazi peupe. Hatuwezi kama nchi mtu mmoja asiyeweza siasa akaamua kuua upinzani sisi tukaendelea kushiriki uchaguzi ili kudanganya dunia kuna vyama vingi.
 
Sio suala la kuripotiwa, tumeona kwa macho yetu. Ule ulikuwa ni upuuzi wa hali ya juu. Hata Mbowe akisema atashiriki sisi wengine tutaendelea kuwataka wapinzani na wengine wanaomini faida za vyama vya upinzani wasiende kupiga kura. Bakini wanaccm mshinde kwa kishindo na upuuzi wenu uwe wazi peupe. Hatuwezi kama nchi mtu mmoja asiyeweza siasa akaamua kuua upinzani sisi tukaendelea kushiriki uchaguzi ili kudanganya dunia kuna vyama vingi.
Naamini kama upinzani umejengwa katika misingi ya upinzani upinzani hufa kama tu umejengwa na misingi ya chama tawala kama ilivyo nccr,cuf,tlp na chadema!
 
Wahuni wa CCM huwajui? Kwa uchache tu:
  1. Mwenyekiti wenu wa CCM(T).
  2. Polepole-Uenezi na Uongo(CCM).
  3. Kinena-KM-CCM
  4. Job Ndugai-Spika.
  5. Makund*- RC Dar
  6. Lusind*-Kibajaj(MB-Mtera)
  7. Wewe mwenyewe.
  8. Lumuba +++++!!
screenshot_2017-11-29-22-34-28-1-png.641635

Iwapo CCM mnakubalika kama mnavodai ruhusuni basi KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI turudi kwenye Ballot Box then tutajua nani anakubalika kati ya CHADEMA na CCM....!
Napenda kukuhakikishia kwamba kama uwanja utakuwa sawa kwa kuleta Katiba mpya na Tume Huru CCM mtaondoka asubuhi na mapema!!!!!!
Hata waletwe waangalizi kutoka marekani bado hamna uwezo wacha hiyo tume huru!
 
Naamini kama upinzani umejengwa katika misingi ya upinzani upinzani hufa kama tu umejengwa na misingi ya chama tawala kama ilivyo nccr,cuf,tlp na chadema!

Tutaendelea kuwa wapinzani humuhumu jukwaani lakini huko mnakopiga risasi wapinzani wenu hapana. Nashukuru kila mmoja sasa ameijua ccm sio chama cha siasa bali ni kikundi cha kijasusi kilichojificha kwenye siasa. Ujumbe ulikuwa wazi siku madiwani walipopokekewa kwenye hafla ya kijeshi.

Endeleeni kuongoza nchi mpendavyo na kwakuwa mmejua hamna majibu ya maisha ya wananchi njia pekee ni kuua upinzani unaoanika mapungufu yenu.
 
Tutaendelea kuwa wapinzani humuhumu jukwaani lakini huko mnakopiga risasi wapinzani wenu hapana. Nashukuru kila mmoja sasa ameijua ccm sio chama cha siasa bali ni kikundi cha kijasusi kilichojificha kwenye siasa. Ujumbe ulikuwa wazi siku madiwani walipopokekewa kwenye hafla ya kijeshi.

Endeleeni kuongoza nchi mpendavyo na kwakuwa mmejua hamna majibu ya maisha ya wananchi njia pekee ni kuua upinzani unaoanika mapungufu yenu.
Mnajaribu kutafuta huruma jumuiya za kimataifa jengeni chama kaeni mjitafakari mnakosea wapi tatizo ni hayo majangili na wafua umeme au wananchi wamechoka usanii wenu!
 
Mnajaribu kutafuta huruma jumuiya za kimataifa jengeni chama kaeni mjitafakari mnakosea wapi tatizo ni hayo majangili na wafua umeme au wananchi wamechoka usanii wenu!

Jumuiya za kimataifa zitasaidia nini? Kama chama kingekuwa kimepotea tusingeona ccm ikitumia nguvu kubwa vile isiyo ya kisiasa kushinda. Naona unajaribu kuchomekea ili uzi wake uende page nyingi kwa michango yetu. Hamuwezi siasa kwa kuiga tabia ya mwenyekiti wenu. Ngoja tuwapotezee tu.
 
Na kila tukiwashauri wanapotezwa na uongozi hawataki sikia, ila tuwaache waugulie, si mchezo, ni kipigo kitakatifu, wasiwasi ni baada ya miaka 3, maana kwa kasi hii hata Ubunge watapoteza wengi, kuanzia Kawe..
 
Amani iwe nayi wakuu,

Kweli mfa maji haachi kutapatapa.Tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani chini ya uongozi mahiri wa Dkt. John Pombe Magufuli, CHADEMA wamekuwa wa kutapatapa tu. Wamekuwa wafa maji, hawana tofauti na Kuku aliyekatwa shingo.

Jambo moja lililowapumaza ni imani kwamba kasi aliyoingia nayo Rais John Pombe Magufuli ilikuwa nguvu za soda. Baada ya kudhihirika pasipo na shaka kwamba dhamira ya Rais ni ya kweli wamebaki kudonoa donoa vijimambo, vimatukio, kutumia wahuni wahuni tu kuwasemea ilimradi tu waonekane wanapambana na Rais John Pombe Magufuli.

Hili ni jambo baya sana kwa mustakabali wa chama. Ni jambo baya kwa sababu chama hakipo kupambana na Rais bali kupamabana na matatizo ya wananachi. CHADEMA hilo wameliweka pembeni. Wananchi hawatasita kuwaadhibu.

Serikali ya awamu ya tano na Chama tawala CCM wamekwepa mishale yote hii ya CHADEMA na wananchi wamewaelewa.

1: Rais John Pombe Magufuli ameingia kwa nguvu za soda
2. Hujuma za kupandisha bei ya bidhaa kama unga, Sukari n.k
3. Kauli za CHADEMA kuwa Rais Magufuli anatekeleza sera za chama chao
4. Kauli ya Lowassa kuwa Wafanyabiashara wa Kariakoo waliokiunga mkono CHADEMA uchaguzi wa 2015 wanaonewa na Rais John Pombe Magufuli. (maana yake Lowassa angeingia madarakani asingehangaika na ukusanyaji kodi)
5. Kauli za CHADEMA kuwa Rais John Pombe Magufuli ni dikteta
6. Porojo kwamba mahusiano ya Tanzania na nchi za nje yatadorora kwa sababu Rais John Pombe Magufuli hasafiri nje ya nchi. Hakuna kipindi Tanzania inazungumzwa kwa mazuri nchi za nje kama awamu hii ya tano. Wameumbuka
7. Kauli kwamba Rais Magufuli ni rafiki wa Rais Kagame wa Uganda na Yoweri Mseveni wa Uganda kwa porojo kwamba ni madikteta. Wamesahau kwamba enzi la Jakaya Kikwete walipiga porojo hizo hizo kwamba Jakaya Kikwete na Kagame hawaelewani na kwamba uchumi wa Rwanda uko juu.
8. Jitihada zao za hivi karibuni za kutaka kuichonganisha Serikali ya Tanzania na ya Kenya, kuwachonganisha Rais John Pombe Magufuli na Uhuru Kenyatta.

Uchaguzi wabaya hawa wa Taifa letu pendwa wametumia nguvu nyingi sana kwenye matukio ya Uchaguzi wa Kenya, matukio ya kupigwa mnada Ngo'mbe na kuteketezwa kwa vifarangkwa mujibu wa sheria zetu baada ya kuingizwa kinyume cha sheria nchini mwetu kutaka kutuchonganisha majirani zetu.

Swali la kujiuliza ni je, mahusiano yetu kuwa.mabaya baina yetu na majirani zetu kunawasaidiaje CHADEMA kushika dola? Kunasaidiaje upatikanaji wa maji, madawa, umeme na huduma.zingine jamii? Au CHADEMA
wanadhani wakenya watawapigia kura?

Matuko ya Mbunge wa Iringa mjini, Peter Msigwa na Mbunge wa Arusha mjini kwenda Studio za KTN TV ya kenya kuanza kumshambulia Rais Magufuli na Serikali yao. Hili sijui tunaliitaje, ni kukosa uzalendo? Ni uasi? Ni ushamba?
9. Porojo za kwamba Serikali inanunua Ndege, inajenga reli badala ya kuwanunulia wananchi unga, sukari n.k

CHADEMA acheni kutapata, Serikali hii imeamua kuijenga Tanzania mpya, hamtaweza kuidhoofisha kamwe. Rais Uhuru Kenyatta ametoa ruhusa ya kufanyakazi na kuishi huko. Nendeni.
 
Nasoma kwa masikitiko sipendi na sitaki kuona maiti haijalishi ni chadema ,ccm, cuf au yeyote, sipendi wala sitaki kuona uonevu haijalishi anafanyiwa nani ,naogopa na kuchukia mateso wanayopewa watu haijalishi anafanyiwa mtu wa chama gani. Ushabiki wetu kwa mambo ya ajabu haya utatupeleka kubaya, baada ya walengwa kuisha nani anajua ni zamu ya nani? Watawala wetu inawezekana ni wazuri ila wafuasi wao wanapowashangilia kwa kufanya mabaya dhidi ya watanzania wenzetu wanahisi wanafurahisha wafuasi wao na hivyo kuongeza kasi ya utesi, uonevu nk ila kuna msemo usemao mwenzio akinyolewa nywele tia maji zako.
Nadhani kama wana wa Tanzanian tunayo ya kupongezana, kushauriana, kuonyana ili hatimae tuwe taifa Kubwa lenye uchumi mzuri na ustawi wa jamii usiotiliwa Shaka.
 
SASA MBONA MNATUMIA BUNDUKI NA MAPANGA TENA KAMA WANANCHI WAMEWAELEWA?
 
Chadema wamepata pigo la kufungia Mwaka, Da Mange nae anajitafakari kurudi CCM
 
Fanyeni kila kitu kwa haki na uwazi bila kutumia mabavu muone wananchi akili zimelala wapi kwa sasa
 
Back
Top Bottom