Nasoma kwa masikitiko sipendi na sitaki kuona maiti haijalishi ni chadema ,ccm, cuf au yeyote, sipendi wala sitaki kuona uonevu haijalishi anafanyiwa nani ,naogopa na kuchukia mateso wanayopewa watu haijalishi anafanyiwa mtu wa chama gani. Ushabiki wetu kwa mambo ya ajabu haya utatupeleka kubaya, baada ya walengwa kuisha nani anajua ni zamu ya nani? Watawala wetu inawezekana ni wazuri ila wafuasi wao wanapowashangilia kwa kufanya mabaya dhidi ya watanzania wenzetu wanahisi wanafurahisha wafuasi wao na hivyo kuongeza kasi ya utesi, uonevu nk ila kuna msemo usemao mwenzio akinyolewa nywele tia maji zako.
Nadhani kama wana wa Tanzanian tunayo ya kupongezana, kushauriana, kuonyana ili hatimae tuwe taifa Kubwa lenye uchumi mzuri na ustawi wa jamii usiotiliwa Shaka.