Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,322
- 33,127
<table border="0" cellpadding="0" cellspacing="0" width="100%"><tbody><tr><td align="left" bgcolor="#cccccc"><table border="0" cellpadding="0" cellspacing="0" width="100%"><tbody><tr><td class="news1">
</td> <td class="news1" align="right" width="150">
</td> </tr> </tbody></table></td> </tr> <tr> <td bgcolor="#999999">
</td> </tr> <tr> <td class="morenews" align="left" bgcolor="#f3f3f3" valign="top"><!--ThumbBegin-->
<!--ThumbEnd-->
Juanita, aliyasema hayo alipokutana na waandishi wetu, Kariakoo, Mchikichini, Dar es Salaam, alipokwenda kufanya shopping ya vitu vyake binafsi.
Alisema, makalio yake yanampa mateso makubwa, kwani mara kwa mara amejitahidi kuyapunguza lakini hakuna mafanikio yoyote ambayo ameyapata mpaka sasa.
Jamani haya si makalio yangu, ni ya kichina, alisema Juanita huku akitoa machozi na kuongeza: Sijui ni lini Mungu atanisaidia kuondokana na mateso haya.
Juanita aliendelea kusema: Wakati mwingine nashindwa kutembea barabarani, kila nikionekana machoni kwa watu naonekana kituko, watu wananishangaa na kunizomea.
Fikirieni wenyewe haya ni mateso kiasi gani, sina raha lakini nimeyataka mwenyewe. Nimejitahidi kutumia dawa kupunguza hayapunguziki.
Akiongea in & out juu ya ishu yake, Juanita alisema, alishawishika kuanza kutumia dawa za Kichina ili kukuza makalio baada ya kuanza kuchekwa na wenzake mtaani kuwa ni kimbaumbau na hana wowowo.
Alisema, kutokana hali ya kuchekwa mara kwa mara, aliona ni vema afanye juu chini ili kuitengeneza heshima yake, ndipo alipoamua kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kuumua makalio ambazo zimemfikisha alipo sasa.
Nilianza kutumia mwaka juzi, mabadiliko yakawa ya ghafla, mtaani watu wakawa wananipongeza kuwa nina shepu nzuri, hipsi safi lakini haikuishia hapo, makalio yangu yaliongezeka kila siku.
Mwaka jana ilikuwa hatari, nikaanza kujiona ni binadamu wa peke yangu, nikawa naona aibu lakini kuna siku mtu aliniletea picha ya yule mshiriki wa Maisha Plus, Efrancya Mangi, nikaambiwa naye anatumia.
Aliyeniletea hiyo picha aliniambia, Juanita usidhani upo peke yako, akaongeza, mbona Efrancya naye anatumia dawa za kichina lakini yupo kawaida na umbo lake ni kubwa kuliko langu? Nilimkubalia na kujiona kumbe mimi si wa ajabu, alisema Juanita.
Aliongeza: Baadaye nikapigwa na butwaa baada ya kusoma habari gazetini kuwa Efrancya yeye makalio yake si ya kichina, bali ni umbo lake halisi, kwa kweli kuanzia hapo niliumia sana na kila siku naona yanakua kiasi ambacho kama mnavyoniona, hata huyo Efrancya ni cha mtoto.
Kuhusu mtindo wake wa maisha kwa sasa, Juanita alisema kuwa analazimika kupunguza pirika za maisha kwa sababu mitaani watu wakimuona wanamzomea hasa akipita Kariakoo.
Alisema, maisha yake ni magumu lakini hulazimika akiwa na safari akodi taksi kwa sababu akipanda daladala watu huacha mazungumzo yanayowahusu na kumjadili yeye waziwazi kitu ambacho alikielezea kwamba huwa kinamuuma.
Hata nyumbani mimi naonekana mtu mzima wakati ni mdogo, wazazi wangu wanajitahidi kunifanya niwe na furaha lakini uwezo wao ni mdogo, ila pamoja na umbo langu lakini ni mwepesi mpaka huwa najishangaa, alisema Juanita.
Alipoulizwa dawa hizo za kichina alinunua hapa Bongo kwa nani, kati ya Maimartha Jesse au Khadija Shaibu Dida ambao wamekuwa wakihusishwa na biashara hiyo, Juanita alijibu kuwa hajanunua kwao, isipokuwa aliletewa na rafiki yake kutoka China.
Huyo rafiki yangu huwa anaziuza Morogoro, sasa alikuwa ananiletea na zilifanya kazi haraka, lakini za kupunguza zimeshindwa, hivi sasa ameniahidi akienda tena anatinunulia, alisema Juanita.
Awali, waandishi wetu wakiwa bize katika misele yao ya kipaparazi, walimuona Juanita akitoka ndani ya taksi na kuingia kwenye duka moja, linalouza vifaa mbalimbali kwa matumizi ya nyumbani, Kariakoo.
Mapaparazi wa Ijumaa, walishtushwa na kelele za Wamachinga, waliokuwa wakizomea na kupiga miluzi, hivyo kugeuka na kumshuhudia Juanita akijitahidi kutembea kwa aibu kabla ya kumfuata na kufanya naye mahojiano.
Huko nyuma, mwandishi wa gazeti hili amewahi kuzungumza na Efrancya ambaye alisema kuwa makalio yake ni ya kawaida, kwani familia yao yote ipo hivyo.
Hata mama yangu yupo hivi, najua kuna watu wanaamini mimi natumia dawa za kichina lakini siyo kweli, alisema Efrancya.
Kilio cha Juanita na makalio ya kichina, kinakuja baada ya miezi miwili iliyopita kutokea kifo cha Miss Argentina 1994, Solange Magnano aliyefariki dunia alipokuwa akifanyiwa upasuaji wa kupunguza makalio.
Solange, 38, alifariki baada ya kukumbwa na tatizo la kuziba kwa mishipa ya damu (pulmonary embolism) akiwa kwenye hospitali moja iliyopo jijini Buenos Aires, Argentina.
Mbali na tukio hilo, lipo lingine la dada mmoja tuliyemnasa kwa jina moja la Semala, anayeishi Keko Magurumbasi, Dar ambaye anahaha kupunguza tumbo lake ambalo linakua kila siku.
Habari kutoka kwa mtu wake wa karibu zinasema kuwa Semala alitumia dawa za kuongeza tumbo matokeo yake kuzidi kipimo alichokihitaji, hivyo kuwa kubwa zaidi.
Ni kubwa sana, anatumia dawa za kupunguza wapi, alisema mtoa habari wetu.
Maimartha na Dida, kwa muda mrefu wamekuwa wakituhumiwa kuuza dawa za kichina za kuongea au kupunguza maumbile, ingawa muda wote wamekuwa wakikanusha.
Watangazaji hao wenye majina makubwa, wamewahi pia kukaguliwa na maafisa wa serikali, kutoka mamlaka zinazohusika lakini hakuna dawa ya kichina wala harufu yake iliyokutwa kwenye maduka yao.
Gazeti hili linawaasa warembo kujihadhari na matumizi ya dawa ambazo hazijapitishwa kitaalamu, kwani zimebainika kuwa na athari hasi kubwa kuliko chanya. Ni vema wakajiamini na kujikubali kulingana na jinsi Mungu alivyowaumba, kwani kinyume chake ni kuchukua uamuzi mbaya ambao baadaye unageuka ni mateso. Mhariri.
http://www.globalpublisherstz.com/2008/06/17/kumbukumbu_ya_bongo.html
</td></tr></tbody></table>
</td> <td class="news1" align="right" width="150">
</td> </tr> </tbody></table></td> </tr> <tr> <td bgcolor="#999999">
Juanita, aliyasema hayo alipokutana na waandishi wetu, Kariakoo, Mchikichini, Dar es Salaam, alipokwenda kufanya shopping ya vitu vyake binafsi.
Alisema, makalio yake yanampa mateso makubwa, kwani mara kwa mara amejitahidi kuyapunguza lakini hakuna mafanikio yoyote ambayo ameyapata mpaka sasa.
Jamani haya si makalio yangu, ni ya kichina, alisema Juanita huku akitoa machozi na kuongeza: Sijui ni lini Mungu atanisaidia kuondokana na mateso haya.
Juanita aliendelea kusema: Wakati mwingine nashindwa kutembea barabarani, kila nikionekana machoni kwa watu naonekana kituko, watu wananishangaa na kunizomea.
Fikirieni wenyewe haya ni mateso kiasi gani, sina raha lakini nimeyataka mwenyewe. Nimejitahidi kutumia dawa kupunguza hayapunguziki.
Akiongea in & out juu ya ishu yake, Juanita alisema, alishawishika kuanza kutumia dawa za Kichina ili kukuza makalio baada ya kuanza kuchekwa na wenzake mtaani kuwa ni kimbaumbau na hana wowowo.
Alisema, kutokana hali ya kuchekwa mara kwa mara, aliona ni vema afanye juu chini ili kuitengeneza heshima yake, ndipo alipoamua kujiingiza kwenye matumizi ya dawa za kuumua makalio ambazo zimemfikisha alipo sasa.
Nilianza kutumia mwaka juzi, mabadiliko yakawa ya ghafla, mtaani watu wakawa wananipongeza kuwa nina shepu nzuri, hipsi safi lakini haikuishia hapo, makalio yangu yaliongezeka kila siku.
Mwaka jana ilikuwa hatari, nikaanza kujiona ni binadamu wa peke yangu, nikawa naona aibu lakini kuna siku mtu aliniletea picha ya yule mshiriki wa Maisha Plus, Efrancya Mangi, nikaambiwa naye anatumia.
Aliyeniletea hiyo picha aliniambia, Juanita usidhani upo peke yako, akaongeza, mbona Efrancya naye anatumia dawa za kichina lakini yupo kawaida na umbo lake ni kubwa kuliko langu? Nilimkubalia na kujiona kumbe mimi si wa ajabu, alisema Juanita.
Aliongeza: Baadaye nikapigwa na butwaa baada ya kusoma habari gazetini kuwa Efrancya yeye makalio yake si ya kichina, bali ni umbo lake halisi, kwa kweli kuanzia hapo niliumia sana na kila siku naona yanakua kiasi ambacho kama mnavyoniona, hata huyo Efrancya ni cha mtoto.
Kuhusu mtindo wake wa maisha kwa sasa, Juanita alisema kuwa analazimika kupunguza pirika za maisha kwa sababu mitaani watu wakimuona wanamzomea hasa akipita Kariakoo.
Alisema, maisha yake ni magumu lakini hulazimika akiwa na safari akodi taksi kwa sababu akipanda daladala watu huacha mazungumzo yanayowahusu na kumjadili yeye waziwazi kitu ambacho alikielezea kwamba huwa kinamuuma.
Hata nyumbani mimi naonekana mtu mzima wakati ni mdogo, wazazi wangu wanajitahidi kunifanya niwe na furaha lakini uwezo wao ni mdogo, ila pamoja na umbo langu lakini ni mwepesi mpaka huwa najishangaa, alisema Juanita.
Alipoulizwa dawa hizo za kichina alinunua hapa Bongo kwa nani, kati ya Maimartha Jesse au Khadija Shaibu Dida ambao wamekuwa wakihusishwa na biashara hiyo, Juanita alijibu kuwa hajanunua kwao, isipokuwa aliletewa na rafiki yake kutoka China.
Huyo rafiki yangu huwa anaziuza Morogoro, sasa alikuwa ananiletea na zilifanya kazi haraka, lakini za kupunguza zimeshindwa, hivi sasa ameniahidi akienda tena anatinunulia, alisema Juanita.
Awali, waandishi wetu wakiwa bize katika misele yao ya kipaparazi, walimuona Juanita akitoka ndani ya taksi na kuingia kwenye duka moja, linalouza vifaa mbalimbali kwa matumizi ya nyumbani, Kariakoo.
Mapaparazi wa Ijumaa, walishtushwa na kelele za Wamachinga, waliokuwa wakizomea na kupiga miluzi, hivyo kugeuka na kumshuhudia Juanita akijitahidi kutembea kwa aibu kabla ya kumfuata na kufanya naye mahojiano.
Huko nyuma, mwandishi wa gazeti hili amewahi kuzungumza na Efrancya ambaye alisema kuwa makalio yake ni ya kawaida, kwani familia yao yote ipo hivyo.
Hata mama yangu yupo hivi, najua kuna watu wanaamini mimi natumia dawa za kichina lakini siyo kweli, alisema Efrancya.
Kilio cha Juanita na makalio ya kichina, kinakuja baada ya miezi miwili iliyopita kutokea kifo cha Miss Argentina 1994, Solange Magnano aliyefariki dunia alipokuwa akifanyiwa upasuaji wa kupunguza makalio.
Solange, 38, alifariki baada ya kukumbwa na tatizo la kuziba kwa mishipa ya damu (pulmonary embolism) akiwa kwenye hospitali moja iliyopo jijini Buenos Aires, Argentina.
Mbali na tukio hilo, lipo lingine la dada mmoja tuliyemnasa kwa jina moja la Semala, anayeishi Keko Magurumbasi, Dar ambaye anahaha kupunguza tumbo lake ambalo linakua kila siku.
Habari kutoka kwa mtu wake wa karibu zinasema kuwa Semala alitumia dawa za kuongeza tumbo matokeo yake kuzidi kipimo alichokihitaji, hivyo kuwa kubwa zaidi.
Ni kubwa sana, anatumia dawa za kupunguza wapi, alisema mtoa habari wetu.
Maimartha na Dida, kwa muda mrefu wamekuwa wakituhumiwa kuuza dawa za kichina za kuongea au kupunguza maumbile, ingawa muda wote wamekuwa wakikanusha.
Watangazaji hao wenye majina makubwa, wamewahi pia kukaguliwa na maafisa wa serikali, kutoka mamlaka zinazohusika lakini hakuna dawa ya kichina wala harufu yake iliyokutwa kwenye maduka yao.
Gazeti hili linawaasa warembo kujihadhari na matumizi ya dawa ambazo hazijapitishwa kitaalamu, kwani zimebainika kuwa na athari hasi kubwa kuliko chanya. Ni vema wakajiamini na kujikubali kulingana na jinsi Mungu alivyowaumba, kwani kinyume chake ni kuchukua uamuzi mbaya ambao baadaye unageuka ni mateso. Mhariri.
http://www.globalpublisherstz.com/2008/06/17/kumbukumbu_ya_bongo.html
</td></tr></tbody></table>