kimatire
JF-Expert Member
- Nov 27, 2008
- 371
- 93
Ushiboy; Umenena mengi sana lakini yale yaliyo hadharani tu, Yale ya ndani ukiacha hayo ya kukung'utwa bado mengi yasiyosemeka huna unayoyajua.Kwani ndoa ni ya wawili tu.Yapo Winnie atasema kuhusu Mandela lakini Mandela naye angekuwa nayo yanayomhusu Winnie,Hapo ndo tungeweza kung'amua yupi alistahili na kwa wakati gani hakustahili msamaha.Upande mmoja hukumtendea haki Mandela kwani alitangulia mbele ya haki na siri yake moyoni.Umeonyeshwa kuguswa na Winnie kutokupata msamaha ili hali ukilaani mfumo dume.Misingi ya ndoa hasa ya Kikristo ambako mimi nina uzoefu nako,Haitoi nafasi kwa mwanamke kutafuta usawa na mwanaume ,Kwa hiyo neno harakati za kujikomboa na mfumo dume ni jambo lisilozungumzika katika ndoa za Kikristo ,Kwani biblia takatifu inaelekeza kuwa , mwanamke na amtii mume wake si vinginevyo.:A S crown-2: