HUMAN CLONING: Kuna ukweli hapa au Nyambu?

2 of Amerikaz most wanted

JF-Expert Member
Jan 13, 2023
1,328
3,691
HUMAN CLONING?

Hiki ni kitendo cha kutengeneza kiumbe kingine (Binadamu/mtu) chenye mfanano na kiumbe/mtu wa mwanzo ambaye ni halisi na kitendo hiki hufanyika kwa kutumia DNA ya mtu halisi kisha anatengenezwa mtu mwingine ambaye watafanana kwa Asilimia 99.9 na atawekewa kumbukumbu za zote za Yule wa awali. Kitendo hiki hufanyika kwa kumuua binadamu halisi na kuutumia mwili wake uleule au kutengeneza mwili mwingine, lakini kumbukumbu zinarudi zilezile.

HUMAN CLONING ilianza miaka ya 1960s hivi na wanashutumiwa CIA ndo wanafanya hii ishu na mwaka 1967 walishawahi kupigiwa kelele na bunge la Marekani kwa kufanya majaribio ya human cloning. Japokuwa ukweli ni kuwa mchezo huu upo chini ya utawala wa UZAYUNI, CIA ni mtoto anayetumwa kufanya kazi Fulani , ikumbukwe hii cloning ni tofauti na genetic splicing ambayo watu weupe walitokana nayo kwa KUCHUKUA viasili na vinasaba vya Mbwa, Nyani na mtu mweusi Kisha kizazi mseto kutokea tulishaona mchezo huo uliofanywa na Jehoval na Yahwe viumbe kutoka sayari inayofichwa iitwayo Nibiru.

Hivyo secret societies wanatajwa kuwa ndo wahusika wakuu wa hii project wakiwa na lengo la kuwa na watu wakuwatumikia katika kukamilisha mipango yao. Wanakuwa wanawaua watu ambao wanapingana nao kisha kuwa-clone ili waendane na itikadi zao. Kuna baadhi ya mastaa wakubwa wanahusishwa kwenye kufanyiwa cloning. Watu kama kina Michael Jackson, Dr. Dree , Eminem, Hillary Clinton n.k. Twende sawa hapa; kwa wake wapenda muziki fahamu kisanga hiki👇

A: Dr. Dre pamoja na yeye kufanyiwa human cloning lakini pia anatajwa kuhusika kwenye cloning ya watu wengine. Anahusishwa na kumfanyia cloning The Game ambapo inasemekana ali-cloniwa wakati alipokuwa gerezani, amekuja kutoka akiwa na tofauti ya kabla hajaenda jela ikiwepo nywele, tatuu yake, hata macho pia. Japokuwa kuna wengine wanadai The Game alicloniwa mwaka 2002 alipoteza fahamu kwa siku 3 mfululizo kisha kupelekwa hospitali na kulazwa, baadaye madaktari hawakumkuta wodini na walipojaribh kufuatilia CCTV zilimuonyesha Dr. DREE na 50 Cent walifika na kumtorosha baadaye akarudi lakini alipouulizwa alikuwa wapi jamaa hakusema.

Kwa upande wa Eminem anahusishwa Dr. Dree kutokana na ule wimbo wao wa CALL ME A DOCTOR Kuna mashairi Eminem anasema"Niitie daktar aje kuyarudisha maisha yangu", lakini pia mistari kama "ulinichukua ukanipa maisha mapya na sasa unayamiliki maisha yangu". Inadaiwa Eminem wa kweli alifariki mwaka 2006 baada ya kutumia madawa kupita kiasi kisha kupelekwa ICU inasemekana pale ndo ilichukuliwa DNA yake na kisha kuundwa upya. Ukitazama picha za zamani za Eminem na wa sasa ni tofauti hasa sura, pua, kichwa, nywele hata macho yake kutoka kuwa mekundu hadi blue fulaani hivi. Lakini kupitia mistari ndani ya wimbo wake wa CINDERELLA anasema "Wamemtuma mtu jeuri aje kuucheza/kuumaliza mchezo, ndani ya plastic amezaliwa kutoka kuzimu, lakini hajafika kukusumbua na stori za Cinderella" Lakini pia mara kadhaa amerekodiwa akisema "Every mammals is nice except me".

B: MICHAEL JACKSON wa kweli inasemekana alifariki mwaka 1984 ambapo aliugua ghafla na kufariki lakini wakaficha siri na kisha kumtengeneza Michael Jackson mpya kupitia hii human cloning project. Baada ya hapo ndo alitoa ngoma kama BAD, Thriller akiwa anasifia ushetani. Na inaelezwa kifo chake cha mwaka 2009 kilitokana na kuanza kuwasaliti na kutaka kwenda nao kinyume, na ukinyume huu ulianzia mara baada ya kutoa ngoma ya BLACK OR WHITE ambapo anaonekana ananawa miko kwenye maji matakatifu baada ya kupiga magoti kisha anonekana shetani akiwa amekasirika. Walimibembeleza aache lakini alikataa then wakamuua. Haya ni baadhi kuhusiana na HUMAN CLONING.

Kuhusu Mandela👇

Huyu Mandela aliyeiongoza South Africa alikuwa Feki alitengenezwa na Makaburu, Makaburu walimuua Mandela halisi halafu Wakamtengeza wa kwao ili awe Kibaraka wao hapo SA (Afrika Kusini). Watu wanauliza Kwamba iweje Mandela aliyefungwa miaka 27 Jela halafu akatoka na kuwasamehe Mabeberu?

Wazungu huwa hawapendi Viongozi wa Africa wenye Misimamo mfano hawakumpenda Mugabe, Gaddaf nk lakini walimpenda Mandela na Wanamsifu Mandela kama Kiongozi bora Afrika wanampa sifa ata ambazo hapaswi kupewa.

Mandela halisi aliuawa Tarehe 8/5/ 1985 akiwa na miaka 67 ndio maana South Africa kuna sherehe inaitwa Dkk 67 za Mandela. Baada ya hapo Makaburu wakamtengeza Mandela wao. Mandela alipoingia jela alikuwa na Kidoti upande wa kulia wa Pua lakini alipotoka alikuwa na Kidoti Upande wa Kushoto.

Baada ya Mandela kutoka Jela Winnie Mandela hakutaka kuendelea kuwa Kimapenzi na Mandela Feki maana Mchongo mzima aliujua kwa hiyo ikatengezwa Zengwe kimakubaliano kwamba amechepuka halafu Mandela akapata hasira akampa Taraka.

Mandela halisi alifungwa Jela baada ya Kutaka kuingiza Askari Msituni ili kupambana Kuwaondoa Makaburu South Africa hapo ndio Makaburu wakamdaka na Kumfunga yaani Mandela lengo lilikuwa kumuondoa kwa Mtutu Mkaburu South Afrika arudi kwao.

Lakini huyu Mandela Feki alivyotoka Jela akaja na Sera za Amani kupinga Ubaguzi kwamba Watu Weusi Wasiwabugue Makaburu na Makaburu Wasiwabague Weusi baada ya Hapo Wazungu wakamkabidhi Tuzo ya Amani. Akapewa Uraisi wa South Africa. Wazungu wakampa Sifa Duniani kuwa ni Kiongozi bora Afrika na mpaka leo huyu Mandela kibaraka wao huyu Duniani kote anatambulika kama hero wa Africa.

Jiulize Mandela alikuwa Kiongozi bora Afrika kwa lipi? Kwa kuipatia Uhuru South Africa au kisa kukaa jela kwa kile wanachodai miaka 27? Nyerere amezisaidia nchi zaidi ya 10 kupata Uhuru lkn haheshimiki lakin Mandela wao Feki anaheshimika kisa kuhubiri Wazungu kutobaguliwa wakija Afrika lkn si tukienda kwao tunabaguliwa.

Huyo Mandela Feki jina lake halisi ni Gibson Makanda.

👉Swali linakuja kwanini mtu atengenezwe kisha walingane umri mfano Huyu Gibson au alikuwa ni mtu Mwingine,swali la pili kwanini watengenezwe Kisha baadae wengine WAFANYE usaliti❓

💊JIBU ni kuwa Gibson ni binadamu tofauti aliyetokana na viasili, viambata, vinasaba vya Mandela kinachotokea walimkuza hii inaitwa (speed growth race) Ila hii ni teknolojia ya usiri wa Hali ya juu na imeua wengi kwani wengi walifanya kupata Ile ya Kurudisha nyuma Rika wakafa na kugombana Vikaki chini ya usimamizi wa familia 13 zinazotawala dunia, ngoja nipaache hapo) cha msingi anakuzwa Hadi kufikia makadrio ya umri Husika narudia sayansi hii ni hatari mno, hivyo Gibson alikuzwa hadi kufikia umri ambao akitoka gerezani watu wataamini ni umri sahihi aliotokanao, teknolojia ya kukuza hukuzwa kila baada ya Miezi 6 kwa muda wa kukaa ktk machine siku 28 huku kumbukumbu zako zikitunzwa, vifo vyao kwa 99% Huwa ni kupooza na kupata kansa ya Ubongo na kwa kujibu swali la pili, wanachofanya nikushindwa kupandikiza kwa 100% akili inayowafuata wao kwa kila kitu Kwa sababu teknolojia hiyo imeanza Juzi mwaka 2015 ambapo kwa 95% tu ndio wanaweza kukucontrol lakini huko nyuma ilikuwa ni 85% tu kukucontrol Kwa sababu huyo ni BINADAMU sio robot kwakuwa anatokana na viasili na vinasaba vya mtu hivyo huwezi kumdhibiti BINADAMU kwa 100% Bali kwa 95% kwa teknolojia ya tangu 2015 ambayo inatarajiwa kufanyika upya na Kwa mabavu kupitia chanjo za covid-19 achana na hizi za kutuandaa kisaikolojia tu hizo zitaenda kupakua Kwenye Tezi penuel kwa 95% kwa kuweka utashi Mpya kupitia mfumo wa teknolojia ya 5G nilishatoa SoMo hili mwaka 2020

Yule aliyeweza kutazama movie ya will Smith iitwayo GEMINI Yani mapacha utanielewa kirahisi au movie iitwayo EQUILIBRIUM ya Emilly Watson ni mfano Mzuri kuhusu mabody guard/walinzi wa viongozi WAKUBWA Duniani kuwa sio binadamu wa kawaida. Tuzidi kujifunza mengi ya Ukiroho lakini pia Siri za hii Dunia. Naligia Mninoi ✍️

FB_IMG_16878880769138712.jpg
_20230627_205509.JPG
 
Pumzi wanatoa wapi za kuwapatia hao clones?
Mtoa mada anaonekana hajui ABC za cloning, au labda ameamua kutupa stori za hollywood movies. Ni vyema atafute soft copy ya hiki kitabu

In his image: The cloning of a man: Rorvik, David M

Ninayo hard copy yake ila akiingia PDFDRIVE.COM anaweza kukipata. Cloning is real na mpaka sasa inafanyika kwa wanyama bila kikwazo chochote, ila si kwa namna aliyoielezea mtoa mada.
 
Nada fikilishi, ninachoamini human clonic inawezekana vzr tu,ila namna ulivyoeleza ya kupandikiza kumbukumbu? Mmh labda baadhi ya tabia za kurithi na inawezekana kabda mtu ajapiteza maisha,ila akifa hapana, the same principle ya wanyama unaweza kutumia kw binadamu.
 
Soma biblia ikupe akili na from biology point of view kuna vitu javiwezekani kama kukipa kitu uhai et maiko jackson afe wamtengeneze mwingne aiseee bangi hizi, nyie nyie ndo mnaamini mambo ya kitahira kila kitu from wazungu mnaamini ety mara allieni pale area 51 mara human cloning yaaan kimsingi kama huna degree ya biology, MD, embryology, au hujui chochote kuhusu human anatomy nyamaza bhna alaaaah.
 
Back
Top Bottom