Makaburi yaliyojaa yageuzwa dili mjini

Kingsmann

JF-Expert Member
Oct 4, 2018
4,448
16,313
Kwa mujibu wa gazeti la nipashe la leo, limeripoti kwamba japokuwa makaburi ya Kisutu, Kinondoni, Magomeni na Sinza kutangazwa na serikali kuwa yamejaa toka mwaka 2018, lakini yameendelea kutumika mpaka sasa.

Kinachofanyika ni unawapa tenda vijana maalumu wanaohusika kuchimba makaburi kwenye hayo maeneo tajwa, na wao watakutafutia eneo la kuzika kwa njia wanazozijua wao.

Kwenye mchakato wa kutengeneza kaburi, ndugu hawaruhusiwi kuhusika, bali mtaenda kuangalia pindi wanapomaliza kazi ya kuandaa kaburi lenu.

Kwa mujibu wa mtangazaji Zembwela wa Wasafi FM, amesema wanachofanya wale vijana wanatengeneza makaburi juu ya makaburi mengine, hasa yale ambayo hayajajengewa, ila kwenye kufukua hawaendi mpaka zile futi 6 zinazotakiwa ili wasije kuwafikia wale marehemu wengine kule chini, wanaishia futi 5 au 4.

1 (1).jpeg


 
Kawaida sana,jamaa yangu mmoja alimzika Baba yake Makaburi ya Kinondoni Mwaka 2020. Wiki iliyopita karudi kutoka Nairobi anakofanya Kazi na moja ya Mipango yake ilikuwa ni kujengea Kaburi la Mzee wake. Akatafuta fundi na kununua kila kitu kama kama matofali,Ciment,mchanga, marumaru nk. Kufika Makaburini asubuhi akashangaa kukuta Kaburi lingine palepale alipomzika Baba yake na limeshajengewa kabisa. Wa kumuuliza hakuna,zoezi likaishia hapo
 
Kawaida sana,jamaa yangu mmoja alimzika Baba yake Makaburi ya Kinondoni Mwaka 2020. Wiki iliyopita karudi kutoka Nairobi anakofanya Kazi na moja ya Mipango yake ilikuwa ni kujengea Kaburi la Mzee wake. Akatafuta fundi na kununua kila kitu kama kama matofali,Ciment,mchanga, marumaru nk. Kufika Makaburini asubuhi akashangaa kukuta Kaburi lingine palepale alipomzika Baba yake na limeshajengewa kabisa. Wa kumuuliza hakuna,zoezi likaishia hapo
Duh
 
Makaburi ni kweli yamejaa sana tena sana, na hao wachimbaji wana kawaida, endapi watakutana na mifupa ya marehemu aliyetangulia kuzikwa kwenye uchimbaji wao, basi hiyo mifupa wataikusanya, wanaweka kwenye kiroba, kisha wanatafuta kasehemu kengine wanaenda kukafukia.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kwa mujibu wa gazeti la nipashe la leo, limeripoti kwamba japokuwa makaburi ya Kisutu, Kinondoni, Magomeni na Sinza kutangazwa na serikali kuwa yamejaa toka mwaka 2018, lakini yameendelea kutumika mpaka sasa.

Kinachofanyika ni unawapa tenda vijana maalumu wanaohusika kuchimba makaburi kwenye hayo maeneo tajwa, na wao watakutafutia eneo la kuzika kwa njia wanazozijua wao.

Kwenye mchakato wa kutengeneza kaburi, ndugu hawaruhusiwi kuhusika, bali mtaenda kuangalia pindi wanapomaliza kazi ya kuandaa kaburi lenu.

Kwa mujibu wa mtangazaji Zembwela wa Wasafi FM, amesema wanachofanya wale vijana wanatengeneza makaburi juu ya makaburi mengine, hasa yale ambayo hayajajengewa, ila kwenye kufukua hawaendi mpaka zile futi 6 zinazotakiwa ili wasije kuwafikia wale marehemu wengine kule chini, wanaishia futi 5 au 4.

View attachment 2819882

View attachment 2819884
Kazikeni maeneo ya asili ya marehemu mkuu.
 
Ni wakati sasa kutathmini ardhi inayohodhiwa na Marehemu.

Tukajifunze katika tamaduni za nchi nyingine, tuje na mbinu itakayopunguza maeneo ya kuzikia.

Iwe tu new trend ipewe airtime watu wataiga tu. Kama walivyoiga eti kutokuweka udongo. Mara kujenga minara na ngazi. Hadi wakaja na msemo ati 'tafuta hela wewe, sio lazima kurudi mavumbini'

Tusipoangalia, watu wataanza kuweka AC kwenye makaburi.

Tuangalie wanaokausha, au wanaochoma au wanaozika wamesimama. Tutapata tu mbinu ya kupunguza real estate.

Lakini pia tunaweza kuamua kubadili matumizi ya eneo la makaburi. Mfano ikipita miaka kadhaa linajengwa lijumba la makumbusho kuuuuuuuuuubwa halafu majina ya hao yanawekwa katika mnara mmoja.

Kunakuwa na vidhibiti mbalimbali vya kisayansi au kijamii vyovyote tu...... lakini (here is the catch) mojawapo ya kipengele inakuwa ndugu wanaruhusiwa kuweka viukumbusho(souvenir) vya wapendwa wao hao. Yaani mfano pasi halafu inakuwa na maelezo 'pasi hii ya mkaa ya mwaka 1990 alitumia babu yetu xxxx xxxx xxxx katika ufundi cherehani' ' Hii ni chemli iliyotumika miaka ya 1996 wakati umeme ulikuwa shida, mali ya mzee xxx xxx'

Kwa hiyo hizo familia badala ya kumsahau babu yao zinapata njia nyingine ya kumkumbuka iliyo chanya zaidi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom