Majina ya wauza Madawa ya Kulevya: Kikwete anayo!

Wah! Tikerra hii ni post nzuri na unachokisema ni jambo ambalo lipo na vijana wengi sana huku kwetu uswazi washaumia kutoka na kutumia, kuuza au kusafirisha madawa ya kulevya. Ila ninatofautiana kuhusiana na hao uliowaita viongozi wetu walishughulikie ili swala manake wao kwao ni mtaji ni sawa sawa ulivyosikia million zaidi ya 15 zimetumika kuamisha omba omba Dar.

Tatizo la madawa la kulevya ni la kijamii zaidi kuliko linavyochukuliwa sasa kwamba ni la kijinai na hakuna jitihada za muda mrefu ambazo zinalenga kukomesha utumiaji na uuzaji wa madawa ya kulevya. Mateja wengi wamekufa kwa kujidunga, wengi pia wamepata ukimwi kwa kutumia madawa kutokana na kushirikiana vifaa vya kujidunga na zaidi na zaidi mateja pia wanakuwa mashoga (Injected drug users) na mateja wakikamatwa na kuwekwa magerezani ndio wanakuwa mabibi za watu huko kutokana na mahitaji yao ya madawa na huko hayapatikani.

Kibaya zaidi watumiaji wanakuwa na mchango mdogo sana katika jamii kama sio kuwa mzigo, mateja wamekuwa ombaomba na wezi. Addiction kupita kiasi ndio sifa kubwa ya utumiaji wa madawa. Tatizo hili ni la kwetu zaidi wana jamii kuliko hao viongozi ambao wako buzy wanajihudumia.

Ni wakati muhafaka kwa jamii forum members kutoka sehemu mbali mbali duniani kutoa uzoefu wao labda inaweza kusaidia kumaliza hili tatizo nilishawahi kusikia Uholanzi wao wameruhusu utumiaji wa madawa ya kulevya na utumiaji ukapungua. Kunamaeneo mengine wananyonga kama Singapore na China .
 
Mnakumbuka the so called list ya majina ya WAUZA UNGA about 3 years ago tukaambiwa list ishakamilika and so on?

Na kama kawaida ya JF watu walisema vya kusema ....kesi iliishia wapi?

sasa in the wake of Ufisadi left and right what makes you think kesi za siku za karibuni zitafanikiwa?

all i know its a good time kuwa Lawyer Tanzania kwa sababu ya complacency zinazoonyeshwa na upande wa mashitaka ambao unawashwa kila kukicha kuleak info za kesi

sasa sidhani kama kuna wakili ambaye hato toa hoja kuwa mteja wake hawezi kupata fair trial wakati JF na na utitiri wa magazeti unazo leaked docs muhimu ambazo zingeweza kusaidia kwenye kesi


sasa ninachosema lets take a back seat and not hold our breaths
 
Halafu akiambiwa ukweli wanajitokeza watu na kusema Raisi anakashifiwa.....
 
Mkuu GT kumbe hamjasahau tu?? Hii inaitwa off-side trick watu wanarudi na kuendelea na mabo yao.... Bongo mambo mteremko kikwelikweli, wape ishu wanasahau ya jana........
 
Umenena Mkuu GT.
Kuna masuala mengi muhimu ambayo yanapaswa kushughulikiwa, mpaka mengine yameanza kusahaulika kama hili... lakini usanii umetawala sana. Tutaendelea kupigwa mabao ya kisigino hadi 2010
 
Mkuu GT heshima Mbele,

Kuna mambo kibao sana huwa yanafumbiwa Macho.Tusiende mabli kabisa kuna maswala makuu mawili ambayo mpaka leo sijui hatma yake nini

1.Richmond Company Limited,sasa na hili tunasubiri baadaye tuje tulivumbue?walisabisha hasara kwa nchi hii wapo tu mmoja wao akiwa mavi

2.Kesi ya rada ambayo iligubikwa na Rushwa

3.Serikali iliingia mkataba wa ovyo na mpaka sasa inalipa Capacitycharge ya Human resource system pale Utumishi(Millioni 35 kwa mwezi)

Kuna uozo mtupu sana ambao ukiamua kuandika kila kitu itabidi ufukuze watu wotehuko serikalini

Kuna hili kwamba kina flani wakiguswa nchi haitatawalika,wana nguvu gani hao watu?
 
Mkuu GT heshima Mbele,

Kuna mambo kibao sana huwa yanafumbiwa Macho.Tusiende mabli kabisa kuna maswala makuu mawili ambayo mpaka leo sijui hatma yake nini

1.Richmond Company Limited,sasa na hili tunasubiri baadaye tuje tulivumbue?walisabisha hasara kwa nchi hii wapo tu mmoja wao akiwa mavi

2.Kesi ya rada ambayo iligubikwa na Rushwa

3.Serikali iliingia mkataba wa ovyo na mpaka sasa inalipa Capacitycharge ya Human resource system pale Utumishi(Millioni 35 kwa mwezi)

Kuna uozo mtupu sana ambao ukiamua kuandika kila kitu itabidi ufukuze watu wotehuko serikalini

Kuna hili kwamba kina flani wakiguswa nchi haitatawalika,wana nguvu gani hao watu?
Huyo mweye kesi ya RADA si ndiye katoa 400 m kwa chama?
 
Ndiye huyo aliyetoa hizo 400M, i wonder kwanini zilipokelewa and what kind of message was he sending. Sijui bado anatuambia kuwa anaweza kutuhonga au kutununua?
 
Leo kwenye Nipashe imeongelea kuhusu watu wanaoleta madawa ya kulevya Tanzania.

Inasemekana majina yanajulikana hata na JK na yapo majina ya wabunge, mawaziri, wafanyabiashara maarufu, watu wa dini (wachungaji, mapadri, mashee etc). Hii list ipo kwanzia 2006 na JK ajaifanyia kitu chochote.

Mtu yoyote anadata kuhusu majina ya hawa watu? or more information on this?
 
Sio inasemekana, Kikwete ameshawahi kusema kwua alipelekewa orodha ya majina ya wauza unga, inashangaza kuwa hadi leo ahtujaona hatua zozote kuchukuliwa licha ya yeye kusema kuwa ameyakabishi kwa taasisi inayohusika na mambo hayo
 
waache wayabanie hayo majina wasijeshangaa
yakining'inizwa hapa ukumbini. si wanajua makali ya jf bana.
 
Back
Top Bottom