Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

"Mwanzo walipotufukuza walituambia tukatafute vyama vingine hilo likafanyika, tulipopata vyama vya kufanyia siasa wakasema vipo kwa ajili ya kugawa upinzani, tukasema tupo tayari kuunganisha Nguvu ya pamoja kwa ajili kuiondoa CCM wenzetu pia hili hawalitaki sasa ni wajibu wenu kutambua watu gani hawataki kuiondoa CCM.

Wananchi watambue tuna nia ya dhati lakini wenzetu wanaweka ugomvi binafsi mbele ya maslahi ya Taifa. Sisi ACT wazalendo bado tupo taayari kushirikiana kwa mujibu wa misingi. Shabaha yetu ni moja tu kubomoa mfumo wa uchumi wa kinyonyaji na kifisadi ili kujenga uchumi shirikishi wa wananchi"

By Zitto kabwe kupitia Twiter
ZITTO NI mwanasiasa anayejitambua sana. Keep on moving guy, no body will stop you in this war.
 
Watanzania hatuna chuki binafsi na Zito bali tuna chuki kubwa kwa yale aliyotufanyia. Mengi yamesemwa juu yake lakini hajawahi kuyajibu kwa vielelezo. Hajawahi kueleza kwa ukamilifu hela aliyokuwa akiipokea toka CCM (kwa kupitia maofisa wa TISS) ilikuwa ya nini? Hajawaeleza Watanzania ukaribu wake mkubwa na mawasiliano yake na maofisa wa juu wa TISS yamekuwa yanahusu nini hasa. Mawasiliano na maofisa wa TISS yalioneshwa kwa vilelezo, na hasa yalikuwa wakati wa kipindi cha kampeni kuelekea uchaguzi.

Leo anapotaka kushirikiana na UKAWA, Watanzania watakuwa na uhakika gani kuwa nia yake kubwa siyo kutaka kujua mipango na mbinu za UKAWA kwa manufaa ya wale ambao amekuwa akiwatumikia siku zote, CCM?
Hakuna hoja ambayo Zitto ameshindwa kuijibu. Hata hivyo, leo hii ndani ya upinzani tuna watu walikuwa wanachama wa ccm, but still tunawaamini na tumewakabizi nyazifa kubwa sana. How do you blv them?
Kafulila alifukuzwa chadema, baadaye alitoa lugha mbaya kwa viongozi wa chadema, but today yupo UKAWA. How do you blv him?
 
mkuu kwani kumualika mtu awe mwanachama ni makosa? suala akubali kutangaza mali zake na madeni basi. na akubaliane na katiba ya kizalendo kuilinda , unakalibishwa maana hata wazambi mbele ya Mungu wana nafasi ya kutubu iweje kati yetu wanadamu?
Upo sahihi mkuu. Anayekataliwa ACT ni yule hasiyekubaliana na katiba ya ACT, unless yeyote anakaribishwa.
 
..huyu alifukuzwa.

..kwa hiyo siyo ajabu CDM kusema hawataki kushirikiana naye.

..yaani mtu afukuzwe CDM, halafu wamrudishe kwa kupitia UKAWA?

..Zitto akashirikiane na vyama vingine lakini siyo CDM.

..kwani hakuna vyama vingine vya kushirikiano navyo zaidi ya CDM na UKAWA?

..We are tired of dramas.

cc Mkandara, Kapwela, Chademakwanza, Kimbunga, Nguruvi3

Hilo la kutotaka ushirikiano ijibie Chadema tu. UKAWA sio Chadema pekee, kuna vyama vingi mle, hivyo weka akiba ya maneno.Hii ni siasa, usijeukashangaa kuelekea uchaguzi huu baadhi ya vyama vilivyo leo Ukawa vikaunda ushirikiano na ACT, haitakuwa ajabu, siasa haitabiriki.

Lakini pia Zitto anaongelea hili kujibu propaganda inayoenezwa kuwa anataka kugawanya kura, hilo ni miongoni mwa masuala muhimu kwa kundi kubwa la watu walioichoka CCM.Ni kundi muhimu kwa chama chochote cha upinzani.

Hivyo kwa ACT na Zitto kutangaza wanahitaji umoja, wamejivua hiyo dhana ya kugawanya kura, hivyo kwa sasa wananchi husika watajua sio ACT wala Zitto aliyegawanya kura bali ni hao wasiopenda umoja.Huu ndio msingi ninaouona.

Alinda, nimeona umenipa cheo, NIKUTAARIFU TU RASMI KUWA MIE SIO MWANASIASA NA SIPO KWENYE UONGOZI WA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA, NI MTANZANIA HURU MWENYE MAPENZI MEMA NA NCHI YAKE, MAWAZO YOYOTE NINAYOTOA HUMU HAYAKIWAKILISHI CHAMA CHOCHOTE HUMU BALI NI MAWAZO YANGU BINAFSI.

NA NIKAONA UMENISILIMISHA KABISA KUWA MUISLAM, NIKUTAARIFU TU KUWA MIE NI MKRISTO KAMA WEWE, KAMA UNGENISOMA KWENYE SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI UNGETAMBUA HILO.
 
mkuu kwani kumualika mtu awe mwanachama ni makosa? suala akubali kutangaza mali zake na madeni basi. na akubaliane na katiba ya kizalendo kuilinda , unakalibishwa maana hata wazambi mbele ya Mungu wana nafasi ya kutubu iweje kati yetu wanadamu?

Inshu sio kutangaza Mali tu, aujulishe umma alivyozipata.
 
Aisee Zitto ana akili nyingi zingekuwa zinagawiwa ninge muomba ampimie kilo moja Mnyika na Mbowe wagawane!

Kijana yuko makini na ni mzalendo wa kweli...

Acha viroja, ajibu hoja.Ajitokeze aseme kwa kukiri au kuyakana mamilioni ya tiss na zile namba zilizotumika kuyasambaza kwa traitors wenzake
 
Hilo la kutotaka ushirikiano ijibie Chadema tu. UKAWA sio Chadema pekee, kuna vyama vingi mle, hivyo weka akiba ya maneno.Hii ni siasa, usijeukashangaa kuelekea uchaguzi huu baadhi ya vyama vilivyo leo Ukawa vikaunda ushirikiano na ACT, haitakuwa ajabu, siasa haitabiriki.

Lakini pia Zitto anaongelea hili kujibu propaganda inayoenezwa kuwa anataka kugawanya kura, hilo ni miongoni mwa masuala muhimu kwa kundi kubwa la watu walioichoka CCM.Ni kundi muhimu kwa chama chochote cha upinzani.

Hivyo kwa ACT na Zitto kutangaza wanahitaji umoja, wamejivua hiyo dhana ya kugawanya kura, hivyo kwa sasa wananchi husika watajua sio ACT wala Zitto aliyegawanya kura bali ni hao wasiopenda umoja.Huu ndio msingi ninaouona.

Alinda, nimeona umenipa cheo, NIKUTAARIFU TU RASMI KUWA MIE SIO MWANASIASA NA SIPO KWENYE UONGOZI WA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA, NI MTANZANIA HURU MWENYE MAPENZI MEMA NA NCHI YAKE, MAWAZO YOYOTE NINAYOTOA HUMU HAYAKIWAKILISHI CHAMA CHOCHOTE HUMU BALI NI MAWAZO YANGU BINAFSI.

NA NIKAONA UMENISILIMISHA KABISA KUWA MUISLAM, NIKUTAARIFU TU KUWA MIE NI MKRISTO KAMA WEWE, KAMA UNGENISOMA KWENYE SUALA LA MAHAKAMA YA KADHI UNGETAMBUA HILO.

Nani ashirikiane na msaaliti aliyekuwa akitoa siri za mikakati ya ushindi kwa TISS?
 
Zitto kwa matendo yake tu haeleweki. Ni zitto anayetaka lowasa ajiunge na chama chake. Ni zitto aliyesema ukawa ni umoja wa wasaka tonge na wa kugawana madaraka. Pia mwenyekiti wa chama chake amewahi sema marufuku kwa mwana act kushirikiana na ukawa. Zitto ni shida jamani.
 
Acha viroja, ajibu hoja.Ajitokeze aseme kwa kukiri au kuyakana mamilioni ya tiss na zile namba zilizotumika kuyasambaza kwa traitors wenzake

Lete ushahidi wa Bank Slip
 
ZITTO NI mwanasiasa anayejitambua sana. Keep on moving guy, no body will stop you in this war.
mkuu kwa taarifa yako zitto haeleweki anataka nini.. Husema chochote atakacho bila kujali madhara yake. Aliwahi sema ukawa ni umoja wa wasaka tonge, lakini hili kasahau..
 
UKAWA wameungana na CCM B Cuf, Chama tawala Zanzibar
 
mkuu kwa taarifa yako zitto haeleweki anataka nini.. Husema chochote atakacho bila kujali madhara yake. Aliwahi sema ukawa ni umoja wa wasaka tonge, lakini hili kasahau..

Chadema walishawahi kusema Cuf ni waliberali, Slaa alisema Kafulila ni sisimizi, lakini leo wameungana, dah
 
mkuu kwa taarifa yako zitto haeleweki anataka nini.. Husema chochote atakacho bila kujali madhara yake. Aliwahi sema ukawa ni umoja wa wasaka tonge, lakini hili kasahau..

Chadema walishawahi kusema Cuf ni CCM B waliberali, Slaa alisema Kafulila ni sisimizi, lakini leo wameungana, dah
 
Hakuna hoja ambayo Zitto ameshindwa kuijibu. Hata hivyo, leo hii ndani ya upinzani tuna watu walikuwa wanachama wa ccm, but still tunawaamini na tumewakabizi nyazifa kubwa sana. How do you blv them?
Kafulila alifukuzwa chadema, baadaye alitoa lugha mbaya kwa viongozi wa chadema, but today yupo UKAWA. How do you blv him?
haa haa mkuu lini kafulila alifukuzwa cdm?
 
Upo sahihi mkuu. Anayekataliwa ACT ni yule hasiyekubaliana na katiba ya ACT, unless yeyote anakaribishwa.
hili la kukaribisha yeyote bila kujali sifa yake mbele ya jamii litaiharibu hiyo act vibaya sana. Time wil tell..
 
Back
Top Bottom