Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

Majibu ya Zitto kwa Wana-CHADEMA

“mwanzo walipotufukuza walituambia tukatafute vyama vingine hilo likafanyika, tulipopata vyama vya kufanyia siasa wakasema vipo kwa ajili ya kugawa upinzani, tukasema tupo tayari kuunganisha nguvu ya pamoja kwa ajili kuiondoa ccm wenzetu pia hili hawalitaki sasa ni wajibu wenu kutambua watu gani hawataki kuiondoa ccm.

Wananchi watambue tuna nia ya dhati lakini wenzetu wanaweka ugomvi binafsi mbele ya maslahi ya taifa. Sisi act wazalendo bado tupo taayari kushirikiana kwa mujibu wa misingi. Shabaha yetu ni moja tu kubomoa mfumo wa uchumi wa kinyonyaji na kifisadi ili kujenga uchumi shirikishi wa wananchi”

by zitto kabwe kupitia twiter

nguvu za soda, ushoga utakwisha oktoba ambako kila mtu atakuwa na lake
 
Zitto umenena ni rais ng'ombe kutikisa mkia lakini si rahis mkia kumtikisa ng'ombe ukawa tutakutana october
 
Kila ukifungua kwenye "New Posts" unakutana na thread 3-5 page ya 1 zinazomzungumzia Zitto au ACT! Kuna zinazoanzishwa na CCM+ACT (Kusifu), za CDM kuponda na za Neutral kuponda au kusifu!

Chama kinapata airtime ya kutosha kwa mtindo huu.
 
Mimi ni shabiki wa kutupwa wa cdm na kura zangu wataendelea kuzipata kama ambavyo wameshazipata. Ila kwenye hili la kujibizana na Zitto kama chama nadhani inabidi waliangalie sana. Kwa huku mitandaoni hakuna namna ya kulidhibiti kwani wengi wanaingia na ID fake hivyo mtu anaweza kujifanya cdm na kumtusi Zitto/Act ili ionekane ni mwanacdm. Ikumbukwe jirani/mfanyakazi wako akianzisha biashara kama yako huna haja ya kujibishana naye hata kama atafungua ili achukue wateja wako, cha muhimu wewe ni kuhakikisha ubora wa bidhaa yako.

CDM wasijaribu kabisa kama chama kujibizana na Zitto/ACT ila wao wasonge mbele na kuhakikisha wanasimamia lengo la kuitoa ccm madarakani na kuja na sera bora zaidi zitakazobadili maisha ya mwananchi. Halafu katika huo umoja wao wa Ukawa ni lazima vyama vyote vinavyounda umoja huo viende kwa wananchi aidha kama Ukawa au chama kimoja kimoja kuhakikisha wananchi hawavurugwi na siasa mfu. Ki ukweli naona vyama vingine kama Cuf, Nccr na NLD ni kama vimechoka kwenda kwa wananchi ama wanategemea historia kuwafanya wapate kura. CDM kwa kweli kwa kiasi kikubwa wanafanya haswa kazi ya siasa. Kwa hiyo nawaomba muachane na Zitto kabisa kwani mpaka sasa katika mikutano yake bado anasimama kama brand ya cdm japo yuko ACT. Halafu hakuna cha kushangaza jamani kwani hata bidhaa mpya ikiingia sokoni matangazo lazima yawe makubwa ili kupata wateja lakini kumbukeni bidhaa bora ndio hudumu sokoni.
 
Msimamo mzuri sana kumpokea Zitto ni sawa na kufuga chatu ndani ya nyumba kuna siku atakula kuku,akimaliza atakuala watoto mwisho atakumeza wewe mwenyewe.
 
Mkuu itakuwaje kama NCCR, NLD na CUF watataka kushirikiana na ACT? Tatizo mnaifanya UKAWA kama CDM na CDM kama UKAWA. Hapo ndipo penye shida kubwa.


Mkuu hakuna kamba iliyofungwa kwa hivyo vyama iwapo vitataka kufanya ushirikiano na ACT, ila kiukweli cdm ni chama kili/kinachofanya kazi ya siasa kuliko hivyo vyama vyote vilivyo kwenye ukawa. Mikutano na kufikia wananchi ukiweka kwa takwimu nadhani cdm itakuwa kwa huku bara itakuwa na asilimia 80 wakati hivyo vingine vyote vilivyo kwenye ukawa havifiki hata 30%. Huo ndio ukweli na vyema ujue wenye maamuzi ya juu ni wale hasa walio na nguvu kubwa na ushawishi na waliofikia wananchi wengi. Angalia hata kwenye umoja wa mataifa Marekani ndio yenye nguvu kuliko nchi nyingine zote kwani hata mchango wake ni mkubwa kuliko nchi nyingine zote kuanzia zenye kura ya veto mpaka zile nyinginezo. Sikatai umoja kwani umoja ni nguvu ila kila mbuzi atakula usawa wa kamba yake.
 
Mtu aliyeonekana hafai anaweza vipi kugawa kura za upinzani?? Mkia hauwezi kumtikisa ng’ombe ila ng’ombe anaweza kutikisa mkia hahahahaha., mkuu panic iko wapi hapo?

mtu alliyeonekana hafai na kufukuzwa kwenye chama kwa usaliti atakaribiswa vipi tena kwenye umoja wa wanamageuzi wa ukweli??
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom