Majibu sahihi ya swali la msingi "Nifanye biashara gani?"

Aug 25, 2019
79
80
Majibu sahihi ya swali la msingi "Nifanye biashara gani?"

Na,

Leonard julius shiganga wa mwanamatingatinga.

Watu wengi hasa wale wanaopata mtaji na kuwa na nia ya kufanya biashara mbalimbali katika maeneo yao, wamekuwa wakijiuliza sana hili swali "Nifanye biashara gani?"

# leo nimeona kuwa, ni vyema na ni jambo la busara kueleza jambo hili kitaalam ili msomaji aelewe kitu gani cha kufanya anapotaka kuanzisha biashara.

Jambo la kwanza kufahamu ni kwamba, hoja hapa sio aina ya biashara unayotaka kufungua. Hoja kubwa na ya msingi hapa ni kwamba, "How do you see yourself in that business?" kwa maana nyingine ni kwamba: ukijiangalia, kujipima, kujitathimini na kujikagua ndani mwako mwenyewe unajiona unaweza kuwa bora kwenye biashara gani kati ya biashara nyingi zilizopo duniani au zile ambazo hazijawahi kufanyika kabla?

Kumbuka kuwa, kinachofanya biashara iendelee kusimama na kukua sio jina au aina ya biashara unayotaka kufanya bali ni uelewa wako juu ya biashara ambayo unataka kufanya.

Lakini pia kumbuka kwamba, wapo watu walioambiwa biashara fulani inalipa sana na imefanya vizuri kwa watu wengi sana wamepata utajiri kupitia hiyo biashara. Lakini wao baada ya kuifanya walifeli na kushindwa vibaya sana na pia kuna watu walioambiwa kuwa, biashara fulani haifai kabisa lakini kwao iliwafaa na kufanikiwa sana.

Jambo la msingi ni kwamba, linapofika suala la kuanzisha biashara, nakushauri ujikague mwenyewe kwenye maeneo yafuatayo:

Eneo la kwanza: kagua ujuzi wako.

Eneo la pili: kagua uwezo wako.

Eneo la tatu: kagua uzoefu wako.

Eneo la nne: kagua mazingira yako:

Eneo la tano: kagua jamii yako, pale unapotaka kufungulia hiyo biashara.

Eneo la sita: kagua uwezo wa team yako ya ushindi, dhana na watu utakaofanya nao kazi.

Eneo la saba: kagua muda wako utakaotumia kwenye hiyo biashara.

Eneo la nane: kagua "Hobbies na interests" zako juu ya ile biashara unayotaka kufanya. Usije ukafanya biashara ambayo huipendi ili hali tu umeambiwa inalipa utakuwa mtumwa wa biashara na itakushinda pale utakapokutana na changamoto hata moja tu hautakuwa na moyo wa uvumilivu kuhimili changamoto kwa sababu hata biashara yenyewe huipendi.

Eneo la tisa: anza kidogokidogo kamwe usiweke mtaji wako wote kwa mara moja. Wateja wako ndio watakao kuongoza juu ya bidhaa gani wanahitaji na bidhaa gani hawahitaji. Hivyo utakuwa unaongezea taratibu kulingana na mahitaji ya wateja wako.

Eneo la kumi na la mwisho: jifunze juu ya maarifu, ujuzi, uwezo, maadili, sheria, miongozo, taratibu na kanuni zinazohitajika juu ya hiyo biashara. Kamwe, usikurupuke kuanzisha biashara ambayo hauna ufahamu nayo.

Zingatia kanuni mbili za kitaalam zinazotumika katika kuanzisha biashara.

Kanuni ya kwanza: "New or modern model of business starts up basics" kanuni hii inaitwa # imar-model.

Daima kumbuka kuwa, unapotafakari juu ya biashara kitu cha kwanza huwa ni wazo la biashara na sio mtaji wa biashara ulionao na mengine yanafuatia kwa mtiriri ufuatao:

1: I- stands for idea (wazo la biashara yako ni nini? Kwa maana nyingine, jiulize, unataka kuanzisha biashara gani?

2: m- stands for motivation (motisha), je! Unamotisha ya kufanya hiyo biashara? Je! Unaipenda?

3: a- stands for ability (uwezo), je! Uwezo wa hiyo biashara unao? Ujuzi? Maarifa? Uzoefu?

4: r- stands for resources or capital (mtaji), je! Rasilimali zipo? Na kama hazipo utazipata wapi?

Kumbuka kwamba, endapo utatumia hiyo "Model" tajwa hapo juu, hakika hutojutia katika maisha yako ya biashara. Lakini pia, unapoanza kwa kuwa na wazo la biashara ni rahisi sana kupanga namna ya kupata rasilimali zinazohitajika ili kutekeleza wazo lako.

Kanuni ya pili: "Traditional or poor model of business starts up basics", hii inaitwa#rami-model.

1: r-stands for resources or capital (mtaji)

2: a- stands for ability (uwezo)

3: m- stands for motivation (motisha)

4: I- stands for idea (wazo)

Kumbuka kuwa, endapo utatumia kanuni ya pili ni sawa na kwenda kinyume na kanuni ya kwanza, ukitanguliza mtaji "At the the top" then wazo linakuwa "At the bottom" biashara yako lazima itafeli mara baada ya siku 90 toka kuanzishwa kwako. Kwahiyo hii "Model" haifai kutumiwa na mfanya biashara mjanja anayetaka mafanikio ya biashara yake. Pia "Model" hii inaweza kukufanya utafute mtaji maisha yako yote na huwezi kupata mtaji wa kutosha kuanzisha biashara kwa sababu hata wazo la biashara yenyewe huna. Jiulize mwenyewe, kwa mfano "Wazo la biashara huna unatafuta mtaji wa nini?"

Mwisho:

Kabla hujaanza biashara yako, kumbuka kuzingatia na kufanya utafiti juu ya p tano zinazohitajika sokoni "5p in the market place"

1st p- is people or customers(poor, middle, rich) ukiligungua hili litakusaidia sana kuhusu aina ya bidhaa utakayouza na kupanga bei kulingana na "Nature" ya wateja wako.

2nd p- is place or location of your business. Utafute sehemu inayoendana na aina ya biashara unayoifanya.

3rd p- is products, your products should be unique and pecuria plus quality. Bidhaa zako ziwe bora kuendana na mazingira uliyopo.

4th p- is price, the price should be unique that will attract many customers to come and buy your products. It the quality, best and the cheapest products that win the market.

5th p- is publicity or advertisements, don't be shy in advertising you products to attract many customers.

Nb: you must have some components of faith so that when you are tested and retested in you business you find yourself firm and stronger.

I wish you all the best in your new business venture!

Shiganga2010@gmail.Com

#think and take stapes.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom