Inawezekana ni kweli una hoja ya msingi..
Lakini hiki kigezo cha "drinking water" kinaonesha ni jinsi gani ulivo mjinga..
Kama kuandika Drinking water ndo kunaamanisha hayo maji ni salama basi hata yale maji ya kandoro yangeandikwa hvo ili yapate soko..
Hiyo neno Drinkng water,purified water,sparking water ni mbwembwe tu kama zile za Express your self,Kazi ni kwako etc..ni sawa useme kwanini Airtel hawasemi express your self basi mtandao wao ni mbovu..
Alaf namna unavoandika comments zako n kama mtu fulani anaeandika kwa kukomoa na kwa kupiga majungu,kama mwanamke wa pwani hivi..
NARUDIA TENA INAWEZEKANA UNA HOJA YA UKWELI KABISA LAKINI KWA UANDISHI WAKO,NI WAJINGA WENZAKO TU WATAKUSUPPORT..
Mi nakunywa KILIMANJARO.
Hapa sikusudii kukujibu wewe maana umeonyesha kuwa kiwango chako kwenye nyanja hii kiko chini sana, ila nitajibu kwasabab ya wana jf wenzetu.
Katika biashara na bidhaa huwa bidhaa zinapewa majina ili ziweze kutambuliwa na kutofautishwa na bidhaa nyingine zilizoko kwenye soko. Hivyo bidhaa "nilazima" iwe na majina mawili hasa kama ugunduzi ulishafanywa na mtu mwingine tayari huko nyuma, Trade name kama vile Kilimanjaro, Uhai, MajiPoa, dasani, sheladol, panadol, elymol, Kiwi n.k na scientific (true) name kama vile drinking water, paracetamol au dawa ya viatu. Hivyo huwezi kutumia jina lako la biashara tu bila kuonyesha pia jina halisi (scientific name) la bidhaa yako. Kama dawa yako inaitwa panadol basi lazima useme kuwa hii ni paracetamol ili mtu atakayetaka kukagua ubora wa bidhaa yako aweze kuona kama kweli ina sifa, ubora, kazi, na tabia za paracetamol halisi ambazo ni kushusha homa na kupunguza maumivu. Hivyo mwenye bidhaa hawezi kuandika Panadol kisha akasema kuwa ndani yake kuna pure paracetamol, pure life paracetamol. concode paracetamol, purified paracetamol, fever paracetamol n.k. Uhai ni jina tu la biashara lakini jina lake halisi la bidhaa hii ni maji ya kunywa (drinking water) sio pure drinking water, na maji halisi ya kunywa huwa yana viwango (sifa, kazi na tabia) vyake ambavyo vipo kwa mujibu wa sheria, utafiti na sayansi. Mfanyabiashara anao uwezekanano mkubwa wa kushitakiwa kama akiandika Uhai ni drinking water lakini maji yake hayajakidhi vigezo vya drinking water vilivyowekwa na ama na shirika la afya duniani (WHO), Europe, China, South Afrika au America. Ndiyo maana wafanyabiashara wanakwepa kuyaita maji yao moja kwa moja kama 'drinking water' kwa kukwepa mkono wa sheria. Shida inakuja pale unaponunua maji yanayokereketa kooni, machungu, yana ukakasi, yana chumvi, sukari, yana harufu ya chlorine, ammonia, majani, n.k wakati wewe ulitaka kununua maji ya kunywa ili kupoza kiu yako tu, Mtengenezaji atakwambia maji yangu hayana bacteria ndiyo maana nimeyaita pure, purified, pure Life n.k lakini sio lazima yawe na ubora wa maji ya kunywa. Maji wanayojichotea wananchi wenyewe kutoka kwenye vyanzo mbalimbali vya maji kama vile visima, mito, maziwa, mabwawa, chemchem, mvua, n.k yanaweza kutofautiana ubora wake kutokana na mazingira chanzo cha maji kilipo lakini maji ya kunywa ya kutengezezwa viwandani (processed) kama uhai, kilimanjaro, dasani, n.k yanatakiwa yafuate viwango ama vya maji ya kunywa au kuwekwa kwenye batteries, rejeta za magari na kuchanganyia dawa (distilled water), au maji ya kumsadia mgonjwa anayeharisha na kutapika, au aliyeungua moto, au anayeshindwa kula chakula, au mgonjwa mwenye shinikizo dogo la damu (hypovolmic shork) n.k. Maji yote haya huwa yana standards zake za kimataifa. Maji ya kunywa ni zaidi ya kutokuwa na wadudu na masafi.
Watu wote wanajua kuwa gari ikiitwa tipper basi ina uwezo wa kupinuka na kumwaga mzigo yenyewe, kama haifanyi hivyo hiyo sio tipper, nina uwezo wa kumhoji mtengenezaji au aliyeniuzia kwanini tipper yake haimwagi mchanga? Lakini kama atakwambia kwamba amekuuzia lori lenye muundo wa tipper na sio tipper huwezi kumhoji zaidi.
kama maji hayakati kiu yangu na yana uwezo wa kuniongezea ugonjwa wa moyo na mafigo hayo sio maji ya kunywa hata kama utayapamba kwa majina gani, kwanza kwanini aseme ni pure drinking water, nini maana yake? (hayana bacteria?, hayana kemikali, hayana harufu, hayana ladha au nini? why pure?). Kama maji ya kandoro kwenye mfuko wa rambo na kuyaandika maji ya kunywa ni juu yangu na taasisi husika kuona kama kweli hayo ni maji ya kunywa yenye kazi ya maji ya kunywa na kuchukua hatua. Lakini kama ameyaandika kandoro, pure water, purified, top water, n.k ni ujinga wako kuyanywa (drink at your own risk)