moto2012
JF-Expert Member
- Jul 3, 2012
- 2,303
- 1,530
Wengi ni wanajeshi form four
Malizia failure!
Wengi ni wanajeshi form four
Ukisikia akili mtopea ndiyo hii. Kwamba una experience ya miaka 10, labda hilo jeshi ni la nyumbani kwenu. Kwa hiyo madaktari walipogoma Muhimbili ni form 4 waliofundishwa na mshua wako walioenda kuthibiti hali? Au walipogoma uwanja wa ndege ni hao ndugu zako walioenda? Je, waliojenga daraja la msata lilipobomoka? Haya, umechunguza ni idadi gani ya wanajeshi, polisi, magereza, usalama wa taifa, n.k walioko ktk kila chuo cha elimu ya juu nchini? Nenda kwa huyo sangoma akakuoshe tena!
huyo jamaa sio mwanajeshi wala hakupitia jeshi lolote bali anajikanyagakanyaga hapa kwa maneno ya kusikia vijiweni na kama ukitimba utatokea kwa askari yoyote mwenye degree ni ujinga wake tu wa kushindwa kufuata sheria na kanuni mbalimbali za majeshi pia graduate huwezi kukaa muda mrefu jeshini bila kuwa afisa.
hivyo mtoa mada anapiga fix tu kama vipi aje tena kwa mahojiano hapa.
So ukiritimba gan unaozungumziwa.Maana huku jeshin wasomi ndio hao wanapigiwa salute,wanalipwa mishahara mizuri,wanavyeo
Uliza pale muhimbili kipindi cha mgomo walifanya nini? Propaganda zitawapoteza. Ulimwengu wa Leo madaraja ya chuma na mbao yanafundishwa chuo gani? Njoo huku kwetu mufindi hayo madaraja tunayajenga kuvushia magogo yetu hatujioni kama wasomi
Acha ujinga ww mawazo mgando hayo ivi unajua kama kuna watu hawalali ili we uishi kwa amani na usalama waki kila.siku afu eti hawana elimu....na uende ata toi boya kweli ww
Tutajie mmoja tu wa hapa Tanzania na nini alichogundua. Kwa wenzetu kulitumikia jeshi ni fahari na uzalendo, ila hapa kwetu ni njaa na dhiki.
Wasomi wa kweli wanastahili kulala. Na asipolala kunajambo la kukumbukwa analigundua. Kwa anayejitambua hawezi kufanya kazi ya jeshi. Jeshi special kwa wavivu wa kufikiri.
Salute na mishahara vina msaada gani kwa nchi? Ningependa nitambuliwe kwa mchango wangu ktk nchi na sio salute. Salute inamaana sana kwa wajinga
Mkuu sina elimu kubwa sana ila elimu yangu ya kidato cha nne inatosha kabisa kuelewa maana ya division of labour na mwalimu wangu wa history form 2 alinifundisha kuwa division of labour inaangalia umri(age) jinsi(sex) na ujuzi au ubobezi(specialization) je unadhani majeshi yetu hasa Polisi na magereza yanawatumia wasomi kulingana na ujuzi waliosomea.
Salute na mishahara vina msaada gani kwa nchi? Ningependa nitambuliwe kwa mchango wangu ktk nchi na sio salute. Salute inamaana sana kwa wajinga
Mkuu una cheo gani na upo jeshi gani?
Una elimu kubwa umeshindwa tofautisha division of labour and specialisation, ungesoma economics form 5&6 ndo ungejua kuwa hapa umehara. Comeback to the topic jeshini kuna watu wenye elimu zao za maana na cio ww ya kwako ya magumashi 1stly u have downstairs.
Kwa experience yangu ya kufanya kazi katika jeshi moja hapa nchi kwa miaka 10 nimegundua kuwa kazi za majeshi(jw,polisi,magereza) zinawafaa watu wenye elimu ndogo tena form 4 failure maana kuna kila aina ya ukiritimba na urasimu ambao msomi hawezi kuvumilia na kama akivumilia ataishia kujilaumu kwa uamuzi wake.
Nyie bishaneni tu, mi cha 4 changu msharaha mkubwa, ninanyumba,gari na watoto wangu nasomesha shule nzuri na nimeridhika na maisha
Inaelekea unastress za kutoajiriwa.
hahaaaa!!! kuna kaukweli hapa,
nina ma friend mwanajeshi, anayoyaongeleaga kwakweli mmmh!!
mtoa mada mm nimekuelewa japo mie naona km watu wamepanik na kugoma kuelewa lile la msingi uliloliongelea.