MAJEMBE: Mnadi aliyenadi wengi, naye anadiwa!

MAJEMBE: Mnadi aliyenadi wengi, naye anadiwa!

Natamani kujua ni gari ya kampuni gani,maana kuna gari ya kampuni ninayofanyia kazi waliikamata pale Kibaha wakaiharibu sana kwa kua hawana uzoefu wa kuvuta malori,mdosi akawasusia gari kisha akawapeleka mahakamani,akasema anataka aifilisi hiyo kampuni maana inanyanyasa watu sana.Niko safarini natamani nijue
Dah,
Yaani Million 5 kwa miaka minne izae mpaka Tshs 300Mil??
Hii biashara safi sana aisee
 
Uuuuuuuuwi mnasemaje Majembe wanauzwa?
Kweli nimeamini hakuna mume wa waume sasa WANAISOMA NAMBA
 
Jamaa ni mpiga dili kakutana na mtoto wa mjini aliyemzidi maarifa,hii nchi awamu ya nne iliiaribu watu walikua wanajipatia hata visivyo stahili vyao.

Ni hukumu ya mungu walipaswa kuipata hapa hapa duniani na wameipata.
 
Wajinga sana hao Jamaa miaka kama 5 nyuma walishakamata Scania ikiwa imeharibikia njiani wakataka 300k kwa nn ipo barabaraban usiipeleke garage. Niliwauliza ni ibebe kichwani na Tani 33 au nifanyaje? Wakaona dharau mwisho wa siku wakala laki na nusu.


Afadhali
 
Serikali hii inasimamia sheria, watz wengi hatufuati sheria, hadi tuzoee kuishi kwa misingi ya sheria na taratibu za nchi wengi wataumia sana.
 
Majembe...walikuwa noma sana hawa watu kumbe kuna wababe wenzao
 
Duuuh kweli muosha huosha nimekubali. Jamaa waliwahi kamata dala dala yangu wakaninyanyasa sana kwa vile nilikuwa bd underground then wakaisweka gari humo ndani na faini kila ikilala ni bk 13 kwa siku. Daaah kweli maisha yanabadilika kwa kasi sana
hata mi nimefurahi,walikamata pikipiki yangu wakadai ten kila siku kwa siku tatu wakala 30.sina hamu nao kabisa
 
Hata mimi Inanipa shida kimahesabu. Deni la million 5 kuwa million 300 ndani ya miaka minne? Hata kama kuna riba kubwa, hesabu hizo zipo juu mno!

Kumbuka gari wanayo yard na gari kwa mwezi ilikuwa inaiingiza 8m tena hiyo 300m mbona ndogo
 
Nimepita pale naona wameamua kulimaliza jumatatu kwasababu team Majembe Vs Team Yono imekua balaa sana pale...
 
Vigu hana na hajawai kuwa ma SCANIA.Pale ni mwendo wa MERCEDES BENZ (actros,axor)na MAN.
Gari za kwanza Mbili za Vigu ni Scania. Na moja ilikamatwa na Majembe meneneo ya kibaha ikiwa imeharibika njiana wakawa na mgogoro mkubwa sana mwanzoni mwa mwaka2014.

Duc in Altum
 
Gari za kwanza Mbili za Vigu ni Scania. Na moja ilikamatwa na Majembe meneneo ya kibaha ikiwa imeharibika njiana wakawa na mgogoro mkubwa sana mwanzoni mwa mwaka2014.

Duc in Altum
Vigu zipo,na hata waliyoikamata pale Kibaha ni Scania 124
 
Hii mijamaa ni wajinga sana,sijui dharura ya gari hufanyikia wapi!,Tunalipa vibali vyote vya kutumia hizo barabara,dharura yake ni barabarani na haikupi taari kua ikifika sehemu fulani itaharibika
 
Back
Top Bottom