Majambazi yapora mabilioni ya shilingi

Majambazi yapora mabilioni ya shilingi

HIZI NI ML 80....SASA FANYA MARA 50...
fedha_9623f.jpg

Watakuwa wametoka BOT moja kwa moja
 
Billion 4 zibebwe kwenye DFP? A big joke! Gari za kubebea fedha zina kazi gani? That is a planned deal, pengine hata hiyo hela haikuwepo, walitaka kuthibitisha tu kuwa ilishaibiwa.

Umesema ukweli, bilioni 4 kuzihamisha tu sio shughuli ya dakika chache. Hizi zinajaza masanduku makubwa sio chini ya sita. Unless labda ilikuwa plot ya wasafirishaji wenyewe.
 
Nipo hapa mbuyuni, dar. Majambazi yamepora fedha zinazokisiwa kufikia sh bilioni nne. Zilikuwa ktk gari lenye namba za dfp. Foleni ni kubwa sana.

Gari lilikuwa likitoka mjini. Ikumbukwe kuwa hapa ni jirani na oysterbay police. Pia si mbali na benki walikopora jana asubuhi.

Kwa hakika kila mtu kashangaa hapa. Waliokuwa kwenye dfp wameonekana kuchanganyikiwa. Ukweli utajulikana.

outcome ya kupeleka vijana jkt wakimaliza warudi nyumbani, kuvunjia wamachinga vibanda na kuwanyanyasa, pia wao wanaona mafisadi wanaiba kwa maandishi bora wao watumie nguvu zao..,,mtaji wa maskini
 
Acha wachukue tu..... Hii nchi kila mtu nachukua chake mappema.... Wao nachukua meno ya tembo wengne chukuen walizokusanya.....

Wengine wanatuibia huko mjengoni Dodoma
 
Bi.mkubwa aliyekuwa kwenye lile gari walioporwa amesema wakati akihojiwa na ITV kuwa baada ya kuvamiwa na kuombwa alete hela,akatoa kitambulisho then akawapa begi lenye mkwanja.
 
Billion4 unaziibaje barabarani na kutoweka mana ni bulk kubwa sana labda uje n van au pickup

Umejua zilikuwa kwenye currency ya nchi gani? Kama ni fedha za noti kama pound ya mwingereza au euro au us dol inawezekena!
 
Jamani tuwe na uhakika kabla ya kuandika jambo. Hapa nimeangalia taarifa ya habari ITV, bado haijajulikana ni sh ngapi huyo mama alokuwa kwenye hiyo DFP ambaye alikuwa na hela hajakubali kusema ni sh ngapi ngoja tusubiri taarifa ya polisi. Huyo mama aloobiwa anasema wamekuja majambazi na pkpk aina ya boxer 4 wafaanza kufatua tairi halafu wakafyatua nyingine kwenye kioo cha nyuma wakamwambia huyo mama atoe mfuko wa hela mama wa watua akatoa kitambulisho chake amabacho kilikuwa kwenye hilo fuko la hela halafu wakaondoka zao kilaini.
Ila watanzania tumezidi kutokuwa waelewa kila ck tunatangaziwa mtu kama umeenda kuchukua mihela mingi nenda polisi utoe taarifa then wakupe polisi wa kukusindikiza ambao utawalipa hela ndogo tu kama sikosei elfu 10 kwa kila polisi badala ya kwenda kupoteza mamilioni.

Ila polisi sijui hawasikii hata milio tu tukio la juzi la wachina limetokea moroco na leo namanga maeneo yote mawili ni karibu sana na kituo cha polisi osterbay.
 
Bilioni 4 ni pesa mingi sana haiwezekani kucontain kwenye cruza (unless hiyo dfp iwe kubwa zaidi ya nijuavyo) bila kuonekana. Talking frm my experience nimecheza sana na haya makaratasi ya madafu.
Hao majambazi wameweza kupakua huo mzigo na kufanikiwa kuondoka nao na kwa usafiri upi?
Hiyo ni katanga, ntakubaliana na hii scenario mpunga uliokuwa kwenye gari ni kiasi kiduchu na amount kubwa ilipgwa kutoka ilikotoka.

zilikuwa kwenye mafungu ya dollar, uk pounds & euro!
 
Huyo mama hajasema mkuu labda tutapata taarifa baadae sana kama amekubali kusema polisi manake hata akisema haisaidii chochote hizo hela haziwezi kurudi.
 
Nipo hapa mbuyuni, dar. Majambazi yamepora fedha zinazokisiwa kufikia sh bilioni nne. Zilikuwa ktk gari lenye namba za dfp. Foleni ni kubwa sana.

Gari lilikuwa likitoka mjini. Ikumbukwe kuwa hapa ni jirani na oysterbay police. Pia si mbali na benki walikopora jana asubuhi.

Kwa hakika kila mtu kashangaa hapa. Waliokuwa kwenye dfp wameonekana kuchanganyikiwa. Ukweli utajulikana.

Kusema hapo jirani na bank iliyoibiwa jana sikweli labda unataka kupamba thread yako nzuri.
 
Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kwamba kweli hela iliyoibiwa ni bilioni saba hela za Zimbabwe ambazo zilikua noti kumi na nne ila moja ikiwa na thamani ya Zim dollars millioni mia tano. Wezi wameshazichenchi na kupata Tshs elfu tatu
.
 
Hakuna kitu kama hiko wewe 4b siyo mchezo
Nakumbuka siku moja tulipeleka Bank 250m kifuko cha saflet kilijaa pomoni
 
Huyo mama hajasema mkuu labda tutapata taarifa baadae sana kama amekubali kusema polisi manake hata akisema haisaidii chochote hizo hela haziwezi kurudi.
Mawazo ya kibongo bongo haya. Basi hamna hata umuhimu wa kusema nimeibiwa kwa sababu fedha hazirudi hata ukisema!
 
Yaaani nimewaza ivi ningegawana na washikaji yangu bi moja nw ningekuwa om na nishanunua gari jipya na nimpatia dem wangu milion kumi afanye mtaji maaana anasumbua na kesho asubuh naenda kijijin kwetu nakopi kufagia makaburi na kutia siment choo cha babu baada ya apo narud mjin kufungua banda la tigo pesa na m pesa
 
Bi.mkubwa aliyekuwa kwenye lile gari walioporwa amesema wakati akihojiwa na ITV kuwa baada ya kuvamiwa na kuombwa alete hela,akatoa kitambulisho then akawapa begi lenye mkwanja.

Hata mimi nimeona na kusikia kupitia ITV, sasa hili la 4 billions nimeshindwa kumeza kwa sababu yule mama amesema amewapa bag lililokua na pesa baada ya kukitoa kitambulisho chake, hii ina maana hilo bag ni hand bag. Pia huyo mama pamoja na mashuhuda wengine wamesema watu hao wameondoka kwa pikipiki, sasa 4B zibebwe kwa pikipiki? Hata hivyo tunashukuru kwa taarifa, lakini alitakiwa asitaje kiasi (watu makini huwa wanasema kiasi kamili cha pesa bado hakijajulikana).
 
Wakuu kias hakijatamkwa, na hata kama pesa ilikuwepo c nyingi ki ivo. Halafu ukimtazma mama aliehojiwa hana wasiwasi, m napata taaabu kweli, something z wrong somewhere! Nyie subiln tu.... Mama anaongea kama anasimlia tukio la harusi?
 
Back
Top Bottom