Majambazi Arusha: Mabomu, Bunduki, Risasi, Bastola - Hii ni Kashfa JWTZ

Mwanakijiji ,

Nnachoshindwa kuelewa ni kitu kimoja , nimesoma comments zako kwenye hii issue na kitu ambacho ninachoweza kusema ni kuwa tayari umeshawahukumu hawa polisi . Statement ulizotumia kama kumpiga mtu risasi tena akiwa amegeukia nyuma au mauaji ya wazi ni mauaji ya wazi yanathibitisha hilo .

Swali langu kwako kwa nini unakuwa mwepesi kuwahukumu hawa polisi ? Na jee una hakika gani kwamba haya majambazi yalipigwa risasi kwa nyuma ? Inakuwa ni vigumu kwangu kukubalina na lile unalolisema wakati inaonekana dhahiri you have preconceived opinion katika hii issue.

Rufiji.. unachukulia vitu nje ya context. maswali yangu yote ninayoyauliza ninayauliza kutokana na habari ambazo tayari ziko hadharani. Sijawahakumu Polisi ila ninahoji kuwa taarifa pekee za tukio hilo zimetolewa na watu pekee waliohusika na tukio hilo. Kuna ubaya gani kupata external opinion ili kuthibitisha maneno hayo ya Polisi? Kama Polisi hawakufanya lolote kinyume cha sheria si wawe wa kwanza kuiita tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora?

Hadi hivi sasa, nina wasiwasi na stori nzima ya Polisi na hayo ninayoyauliza kama ilivyoripotiwa na vyombo vya habari na Polisi wenyewe ndiyo vitu vinavyohitaji kuchunguzwa. Maoni yangu mimi hayana thamani yoyote ile ila maswali yangu ndiyo ya msingi.

Zaidi ya yote nina taarifa ambazo zinanifanya nihoji mambo haya...kwani POlisi wanafahamu kuwa watu wengi hawafahamu kilichojiri jioni ya tukio. Bahati mbaya... kuna watu waliokuwa karibu na ni wao ambao Tume ya Haki za Binadamu inaweza kuzungumza nao
 
Rufiji

Mwanakijiji alipata kigugumizi alipomuhoji Kamishna wa Polisi, tumpe benefit of a doubt, lakini hatuwezi kukubali pesa ya walipa kodi ikafanya uchunguzi ambao sio lazima kwa majangili yanayotumia silaha za kijeshi.
 
Rufiji

Mwanakijiji alipata kigugumizi alipomuhoji Kamishna wa Polisi, tumpe benefit of a doubt, lakini hatuwezi kukubali pesa ya walipa kodi ikafanya uchunguzi ambao sio lazima kwa majangili yanayotumia silaha za kijeshi.

Dua... tume ya haki za binadamu na utawala bora inalipwa ili kufanya uchunguzi wa mambo kama hayo..
 
I say waste the madha's, period. Jambazi ni Jambazi tu. Kama hajakamatwa na kuwawa wakati yuko katika action, atakapokatwa hata kama kalala dawa yake kuuawa tu. Tena inabidi ile sheria ya "shoot to kill" iwe emphasized big time. Hakuna huruma na hawa watu.

Mwamakijiji kama unaona vipi vipi, leta petition, peleka malalamiko kwenye mahakama ya umoja wa mataifa. If anything, I'll be the first to tell them (UN), they need to change a few things.
 
Kisura ,

I couldn't agree you with you more. Ni lazima tutambue ya kuwa nchi yetu ni maskini hatuwezi kupoteza hela za walipa kodi kufanya uchunguzi kujua ni nani aliyaua haya majambazi ! Haya majambazi yalikuja kwa mission moja tuu nayo ni kuuwa na kufanya unyanga'nyi thanks God tumewawahi! kama polisi wasingewawai basi maisha ya baadhi ya raia wema yangetoweka ...

Kwa wale ambao wanajua masuala ya silaha wanajua AK 47 ni kitu gani , hii sio silaha ya kawaida bali ni silaha hatari ya kivita. Haya majambazi yamekutwa na hizo silaha na sio hilo tuu ...mmoja wao alikuwa amehukumiwa adhabu ya kifo huko kenya na mpaka sasa polisi wa Kenya hawajui ametoka vipi jela . Sasa kwa nini tupoteze muda na resources kuchunguza mauaji ya majambazi ambayo yalikuwa yanatafuta njia ya kutuua sisi? Haya ndio mambo yanayowacost wamarekani huko Iraq rules of engagement , wanasema mpaka mtu akushoot ndio unaruhusiwa kumshoot ...sasa swali huyo mtu akikupiga risasi wewe utarudisha vipi wakati ushakufa ?

Narudia tena , naheshimu sana utawala wa sheria lakini inapokuja kwenye kuchagua kati ya utawala wa sheria na kuishi , nitachagua kuishi.
 
Rufiji acha kanyaboya zako hapa...utaishi vipi katika nchi amabayo haina utawala wa sheria,nenda Somalia basi ukaishi.
 
I say waste the madha's, period. Jambazi ni Jambazi tu. Kama hajakamatwa na kuwawa wakati yuko katika action, atakapokatwa hata kama kalala dawa yake kuuawa tu. Tena inabidi ile sheria ya "shoot to kill" iwe emphasized big time. Hakuna huruma na hawa watu.

Sawa. Nashauri tusimamishe Katiba kwanza na kuondoa sheria iliyounda Mahakama.

Mwanakijiji kama unaona vipi vipi, leta petition, peleka malalamiko kwenye mahakama ya umoja wa mataifa. If anything, I'll be the first to tell them (UN), they need to change a few things.

No need, nitaiambia nchi yangu kama hawataki utawala wa sheria watuambie tu. Ndiyo gharama ya kutaka kujenga demokrasia. Msingi wa kwanza ni kuheshimu utawala wa sheria. Kama tutawaachia Polisi wavunje sheria kwa "jina letu" basi tuambiane mapema kuwa Polisi wana ruhusua ya kumuua mtu yeyote ambaye inasemekana kuwa ana mpango wa kufanya vitendo vya kijambazi. Tukifanya hivyo, tutaomba na sisi raia ruhusa ya kuwamaliza wale wote ambao tunahisi na tuna ushahidi kuwa wana mipango miovu dhidi yetu. Unasemaje?
 
Sawa. Nashauri tusimamishe Katiba kwanza na kuondoa sheria iliyounda Mahakama.



No need, nitaiambia nchi yangu kama hawataki utawala wa sheria watuambie tu. Ndiyo gharama ya kutaka kujenga demokrasia. Msingi wa kwanza ni kuheshimu utawala wa sheria. Kama tutawaachia Polisi wavunje sheria kwa "jina letu" basi tuambiane mapema kuwa Polisi wana ruhusua ya kumuua mtu yeyote ambaye inasemekana kuwa ana mpango wa kufanya vitendo vya kijambazi. Tukifanya hivyo, tutaomba na sisi raia ruhusa ya kuwamaliza wale wote ambao tunahisi na tuna ushahidi kuwa wana mipango miovu dhidi yetu. Unasemaje?

That's very dangerous....
On this one, I side with Mwanakijiji. The rule of law shall be paramount.
 
Nyani, ndugu zangu hapa hawako tayari kuadmit implication of giving the Popo licence to grill and kill! If we were to allow them to act with impunity, it is the innocents who would pay the price. We can not allow that. We have decided to build a constitutional democracy where the rule of law, separation of powers, checks and balances and equal justice are to be appreciated and enjoyed by all. Matokeo ya jamii kama hiyo ni kuuliza na kutaka maelezo kutoka serikali yao. We can not let the army, magereza or police kuanza kuchukua sheria mikononi mwao kwa "jina letu".
 
Kama tutawaachia Polisi wavunje sheria kwa "jina letu" basi tuambiane mapema kuwa Polisi wana ruhusua ya kumuua mtu yeyote ambaye inasemekana kuwa ana mpango wa kufanya vitendo vya kijambazi?


Sio mtu yeyote kama ulivyosema kwani hawa hawakuwa watu wa kawaida haya ni majambazi ...nasijui kwanini unaogopa kutumia hili neno.Pili, kwa nini uzungumzii silaha walizokutwa nazo pamoja na zile bullet proof! Vile sio vifaa vya kufanyia party ! Tatu, kwa nini hauzungumzii hawa watu waliouwawa walikuwa ni watu gani ? Jee walikuwa ni raia wema huko walikotoka na walikuja Moshi kufanya biashara ?
 
Sio mtu yeyote kama ulivyosema kwani hawa hawakuwa watu wa kawaida haya ni majambazi ...nasijui kwanini unaogopa kutumia hili neno.Pili, kwa nini uzungumzii silaha walizokutwa nazo pamoja na zile bullet proof! Vile sio vifaa vya kufanyia party ! Tatu, kwa nini hauzungumzii hawa watu waliouwawa walikuwa ni watu gani ? Jee walikuwa ni raia wema huko walikotoka na walikuja Moshi kufanya biashara ?

Rufiji, Kenya ndio walikuwa na kila sababu ya kwanza kabisa ya kuhakikisha watu hawa wanakabiliana na watuhumiwa hawa. Hujajiuliza ilikuwa mtu aliyehukumiwa kunyongwa awe mitaani? Pili watu hawahukumiwi kwa "hear say" na kukutwa umesimama karibu na bunduki! Watu wanahukumiwa kwa kile walichokifanya. Hivi kama wale jamaa baada ya kuzungukwa na POlisi walipoambiwa wajisalimishe wakakubali kujisalimisha unataka kuniambia ingekuwa sahihi kuwaua anyway "kwani walikuwa watu wabaya"? Ina maana hata kama walikubali kuwa wamebambwa ina maana Polisi badala ya kuwafikisha kwenye vyombo vyenye kuamua sheria basi wachukue sheria hiyo mikononi mwao?

Rufiji... Katiba yetu iliposema "kila mtu anastahili haki ya kuthaminiwa na kutambuliwa utu wake" ilikuwa inamaanisha hivyo. Ndiyo maana inakataza kabisa adhabu za kisasi au za kumtweza mtu. Hata kama mtu ni mtenda maovu, utu wake ni lazima uheshimiwe. Ndio maana hata walipomkamata Sadamu (na kila mtu alijua watamnyonga) walifanya ionekane kuna haki fulani. Hivi hili ni gumu sana?

Mauaji ya wazi ni mauaji ya wazi.. watu 14 wameuawa mikononi mwa Polisi, tunachochunguza ni je ilikuwa justified. Niseme vizuri sina tatizo Polisi akiwa kazini akalazimika kumuua mtu.Hata hivyo anapofanya hivyo ni lazima ionekane mbele ya sheria kuwa alifanya kwa haki. Tusipohoji tutaruhusu extrajudicial killings kwa kisingizio cha kupambana na majambazi. Unfortunately that has happened before.

Nikupe mfano, leo hii nitonywe kuwa kuna watu watatu wanaopanga kuvamia nyumba yangu ndani ya siku mbili. Kwa kutumia ushirikiano na wanakijiji wenzangu, tukawatambua watu hao na kuwafuatilia. Tulipowanyemelea tukambana nao, na tukawaua wote, na tulipofanya uchunguzi tukakuta walikuwa na silaha za moto na mapanga, ramani ya nyumba yangu, picha za mke na watoto, na namba ya safe langu.

Sasa Polisi wakija kuulizia kulikoni? niwaambie kuwa nilikuwa najitetea mimi nafamilia yangu kwani hapo mtaani kumekuwa na vitendo vingi vya kijambazi hivyo nikawaelezea stori nzima na jinsi gani tuliwashtukiza na kuwaua maharamia wale ambao ikagundulika baadaye kuwa walikuwa na historia ya Uhalifu mkoa wa jirani.

Hivi unafikiri Polisi wataniachilia, au watataka nifikishwe mahakamani kuweza kuonesha uhalali wa kuwaua washukiwa hao?

Naomba ujibu swali hilo ili nielewe mtiririko wa mawazo yako.
 
Rufiji... Katiba yetu iliposema "kila mtu anastahili haki ya kuthaminiwa na kutambuliwa utu wake" ilikuwa inamaanisha hivyo. Ndiyo maana inakataza kabisa adhabu za kisasi au za kumtweza mtu. Hata kama mtu ni mtenda maovu, utu wake ni lazima uheshimiwe. Ndio maana hata walipomkamata Sadamu (na kila mtu alijua watamnyonga) walifanya ionekane kuna haki fulani. Hivi hili ni gumu sana?

Mzee Mwanakijiji, mbona wale watoto wa Saadam waliuawa wakati wanajua walikuwa ndani ya ile nyumba, mbona hawakwenda kuwakamata basi? Jibu ni kwamba, askari wale walijua kuna posibility ya kwao kuuwawa kabla hawajawakamata! Sasa polisi wetu walichofanya kina ubaya gani?

Anyhow, this is beside the point, mimi shughuli yangu ni ya hapo mjini Bongo. Haya ndio masheria niliyopigia mstari ndio yanatakiwa yawe -edited! Hivi hawa majambazi wakiua innocent victims, utu wa the victim unatambuliwa na nani? Au ukishakufa ndio hautambuliwi tena?? Hawa sorry excuse for human beings, ambao pia hawana faida zaidi ya kula oxygen ya bure hapa duniani, wanahitaji kushughulikiwa kikamilifu, hata ikibi tuwafungie mahali ambapo hatuwapi maji wala chakula mpaka watapokufa, then be it, they deserve that.Kwanza polisi hawa wamewawapunguzia maumivu. Wamesha-cause so much pain and misery!

Kama tunavyojua, ukiwa katika njia panda, bora gonga watu wawili wafe kuliko kugomba basi litaloua watu 100. Therefore, sometimes desperate times, require desperate measure, people always die, inncocent people always get caught up, they always do, but if the motto is to waste the decay of human society, so be it...
 
Kenya ndio walikuwa na kila sababu ya kwanza kabisa ya kuhakikisha watu hawa wanakabiliana na watuhumiwa hawa. Hujajiuliza ilikuwa mtu aliyehukumiwa kunyongwa awe mitaani? Pili watu hawahukumiwi kwa "hear say" na kukutwa umesimama karibu na bunduki! Watu wanahukumiwa kwa kile walichokifanya. Hivi kama wale jamaa baada ya kuzungukwa na POlisi walipoambiwa wajisalimishe wakakubali kujisalimisha unataka kuniambia ingekuwa sahihi kuwaua anyway "kwani walikuwa watu wabaya"? Ina maana hata kama walikubali kuwa wamebambwa ina maana Polisi badala ya kuwafikisha kwenye vyombo vyenye kuamua sheria basi wachukue sheria hiyo mikononi mwao?


Kwa bahati mbaya polisi wa Kenya wamefurahia mauaji hayo kwa sababu moja wa majambazi alikwisha hukumiwa kifo na akatoroka kwa miujiza. Hujawahi kuona wezi wanapigwa hadi kufa wakishikwa?

Katiba yetu iliposema "kila mtu anastahili haki ya kuthaminiwa na kutambuliwa utu wake" ilikuwa inamaanisha hivyo. Ndiyo maana inakataza kabisa adhabu za kisasi au za kumtweza mtu. Hata kama mtu ni mtenda maovu, utu wake ni lazima uheshimiwe. Ndio maana hata walipomkamata Sadamu (na kila mtu alijua watamnyonga) walifanya ionekane kuna haki fulani. Hivi hili ni gumu sana?


Hiyo haki ni kwa raia wema wasiotembea na granades mfukoni pamoja na vest za kinga ya risasi huku wamebeba AK 47.
Usijichanganye hapa Sadam alishikwa baada ya watu wangapi kufa? Hao huoni ni binadamu pia? Double standard za USA usizilete hapa mkuu! Hao marekani tunawafahamu vizuri haki za binadamu wakati wanatunyonya, kumbuka nani alianza fujo za Congo, Somalia, Angola just to mention a few.

Mauaji ya wazi ni mauaji ya wazi.. watu 14 wameuawa mikononi mwa Polisi, tunachochunguza ni je ilikuwa justified. Niseme vizuri sina tatizo Polisi akiwa kazini akalazimika kumuua mtu.Hata hivyo anapofanya hivyo ni lazima ionekane mbele ya sheria kuwa alifanya kwa haki. Tusipohoji tutaruhusu extrajudicial killings kwa kisingizio cha kupambana na majambazi. Unfortunately that has happened before.


Wali-deserve kuuawa Serikali ya Tanzania ina wajibu wa kulinda raia wake hasa pale wageni wanapoingia na silaha za kivita. Nawapongeza askari wetu kwa kazi nzuri. Mauaji yalipotokea Dar wakati raia wasiobeba granades na AK 47 tume iliundwa na kuchunguza mauaji yale sasa sioni kwa nini hawa majangiri wenye silaha za kijeshi tuendelee kupoteza pesa za walipa kodi. Na hili ni onyo kwa manyang'au wote kutoka nchi jirani wasilete silaha zao ili kuwadhulumu WTZ, tutawamaliza kwani Jeshi letu la Polisi linafuatilia vibaka kama wao kwa kila hali ndio kazi waliyotumwa na WTZ kulinda maslahi ya raia wema.

Nikupe mfano, leo hii nitonywe kuwa kuna watu watatu wanaopanga kuvamia nyumba yangu ndani ya siku mbili. Kwa kutumia ushirikiano na wanakijiji wenzangu, tukawatambua watu hao na kuwafuatilia. Tulipowanyemelea tukambana nao, na tukawaua wote, na tulipofanya uchunguzi tukakuta walikuwa na silaha za moto na mapanga, ramani ya nyumba yangu, picha za mke na watoto, na namba ya safe langu.

Sasa Polisi wakija kuulizia kulikoni? niwaambie kuwa nilikuwa najitetea mimi nafamilia yangu kwani hapo mtaani kumekuwa na vitendo vingi vya kijambazi hivyo nikawaelezea stori nzima na jinsi gani tuliwashtukiza na kuwaua maharamia wale ambao ikagundulika baadaye kuwa walikuwa na historia ya Uhalifu mkoa wa jirani. Hivi unafikiri Polisi wataniachilia, au watataka nifikishwe mahakamani kuweza kuonesha uhalali wa kuwaua washukiwa hao?
Huu mfano sio sawa na kilichotokea.
 
Halafu wewe Mzee Mwanakijiji, mbona unakubali yaishe kirahisi rahisi hivi...una yako wewe!
 
Nadhani itabidi tutumie fursa hii ili tutoe maoni yetu jnsi gani ya kukabiliana na wageni toka Kenya na hususan majambazi toka huko

Ukumbi ni wenu wana Bodi
 
Back
Top Bottom