Majaji wanatakiwa kuzingatia sheria.

Majaji wanatakiwa kuzingatia sheria.

mhizika

Member
Joined
Jun 2, 2018
Posts
8
Reaction score
4
Dar es Salaam. Jaji mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Benard Rwanda amewataka majaji na mahakimu nchini kutumia busara, kuzingatia sheria na miiko katika kutoa haki mahakamani.

Amewataka kutojaribu kumtia hatiani mtu kwa kuwa tu wanajua tabia yake ni mbaya, bali wafanye hivyo baada ya kujiridhisha kuwa mhusika ametenda kosa.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Julai 27, 2018 katika hafla ya kumuaga pamoja na mwenzake Jaji mstaafu Sauda Mjasiri iliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu, jijini hapa.

Ametoa miiko 10 kama wosia kwa majaji na mahakimu na kuwataka kuhakikisha wanatumia busara na kuzingatia sheria inavyosema kwa kuwa mahakamani kila hatua ni sheria.

Ameitaka mahakama kujenga imani kwa wananchi, akieleza kuwa imani hiyo ndio nguzo muhimu ya mahakama na si sheria pekee.

“Wananchi wasipokuwa na imani na mahakama itakuwa ni hatari. Hapa majaji na mahakimu wafanye kazi kwa kufuata miiko na wajaribu kuangalia wasifanye vitu ambayo ni vya ajabu ajabu,” amesema.

Amewataka majaji na mahakimu kutokwepa majukumu yao katika kutoa maamuzi ya haki.

Akiwazungumzia wastaafu hao, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amesema Jaji mstaafu Rwanda ametumikia mahakama kwa miaka 37 huku Jaji Mjasiri akikitumikia chombo hicho cha Dola kwa miaka 15.

Source: Mwananchi
 
Bado Mahakama hasa majaji nina imani nao sana.
Dunia mzima majaji na mahalama ni tumaini kubwa la wanyonge.
Mara nyingine matatizo yapo mahakama za chini kwa mahakimu mana bado wanatafuta sifa toka kwa wanasiasa.
Lakini Majaji kwa kweli Wanasimamia haki kwa kiwango kikubwa sana.
 
Dar es Salaam. Jaji mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Benard Rwanda amewataka majaji na mahakimu nchini kutumia busara, kuzingatia sheria na miiko katika kutoa haki mahakamani.

Amewataka kutojaribu kumtia hatiani mtu kwa kuwa tu wanajua tabia yake ni mbaya, bali wafanye hivyo baada ya kujiridhisha kuwa mhusika ametenda kosa.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Julai 27, 2018 katika hafla ya kumuaga pamoja na mwenzake Jaji mstaafu Sauda Mjasiri iliyofanyika katika ukumbi wa Mahakama Kuu, jijini hapa.

Ametoa miiko 10 kama wosia kwa majaji na mahakimu na kuwataka kuhakikisha wanatumia busara na kuzingatia sheria inavyosema kwa kuwa mahakamani kila hatua ni sheria.

Ameitaka mahakama kujenga imani kwa wananchi, akieleza kuwa imani hiyo ndio nguzo muhimu ya mahakama na si sheria pekee.

“Wananchi wasipokuwa na imani na mahakama itakuwa ni hatari. Hapa majaji na mahakimu wafanye kazi kwa kufuata miiko na wajaribu kuangalia wasifanye vitu ambayo ni vya ajabu ajabu,” amesema.

Amewataka majaji na mahakimu kutokwepa majukumu yao katika kutoa maamuzi ya haki.

Akiwazungumzia wastaafu hao, Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma amesema Jaji mstaafu Rwanda ametumikia mahakama kwa miaka 37 huku Jaji Mjasiri akikitumikia chombo hicho cha Dola kwa miaka 15.

Source: Mwananchi
TUNAOMBA MIIKO HIYO KUMI, NI MUHIMU ANA KUIJUA
 
Bado Mahakama hasa majaji nina imani nao sana.
Dunia mzima majaji na mahalama ni tumaini kubwa la wanyonge.
Mara nyingine matatizo yapo mahakama za chini kwa mahakimu mana bado wanatafuta sifa toka kwa wanasiasa.
Lakini Majaji kwa kweli Wanasimamia haki kwa kiwango kikubwa sana.
mwandiko wako unafanana na mhadhiri mmoja wa chuo kikuu kitivo cha sheria mahali fulani Tanzania.
 
Mzee Ruanda mbona anaonekana kijana sana. Hongera sana Mhe. Jaji miaka 37 si mchezo.
 
Kwaio alisubiri mpaka astaafu ndo atoe kauli kama hizo?
 
Back
Top Bottom