SEHEMU YA NNE (4)
Tulipoishia…
Yale matokeo yakafifisha ndoto zangu za kwenda Science jumla…
Tuendelee Sasa…
Familia ya pale home kwa aunt ilikua poa tu maana hakukua na challenge sana na nisingependa kugusia part hii maana sio muhimu sana.
Baada ya matokeo yale ratiba ilibadilika, ilikua hata nikitoka tuition lazima home nisome usiku, uncle (mume wa aunt) alikua lazima aje usiku kuchungulia room kwetu kama tumeamka kusoma (Kuna mtoto wa mwisho wa aunt mwingine alikua pale ma alikua primary bado ndo tulikua tunapeana kampani kusoma)
Kwa upande mwingine maisha ya kiroho pia yalikua yanakaziwa pale, kila jumapili lazima kwenda kanisani, ilikua ni lazima so nilinyooka na kuwa kijana mzuri tu, sikua na makundi kama Mwanza kule.
Turudi kwa Jane kwanza… Wakati wote ambao niko kwenye mahusiano na Jane sikua nimewahi kufanya chochote. Kuna siku tulipanga kwamba weekend twende mlimani huko ( kulikua na mlima flani una majani na miti miti na hakukuwa na nyumba karibu na maeneo yale) ukipanda huko juu unaiona Bukoba vizuri kabisaaa, mlima uko maeneo ya Buyekera karibu na shule ya msingi Buyekera. Kwa watu walioishi Bukoba mjini wanapafahamu ingawa kwa sasa mlima huo una nyumba kibao tu.
Tuliplan twende kule tukashiriki tendo wakati huo mimi ndo mara ya kwanza na mwenzangu yeye alikua ashapiga show kadhaa huko nyuma.
Maisha yaliendelea na weekend ilifika tukaenda zetu juu huko mi nilibeba maji ya kunywa tu. Tulikutana mahali na tukaanza safari.
Baafa ya muda kama 20 min tulikua kule juu tukajichimbia mahali ma story ziliendelea huku nisijue naanzia wapi.
Kufupisha, tulishiriki tendo na ndo ilikua mara yangu ya kwanza. Siwezi sema nilienjoy sana maana sikua najua mambo mengi na niliishia bao la kwanza wala sikutaka kuendelea.
Sasa baada ya yote Jane alizidi kunipenda na mimi nilikua nampenda sana kwakweli. Kule shuleni walikua wanasema tu mi napata story ila hatukuwahi kuweka wazi mapenzi yetu mbele za watu. Baadhi ya washikaji walikua na chuki na mimi kisa Jane. Jane alikua na mwili mkubwa kidogo kunizidi na alionekana kunizidi kama mwaka hivi (nilijua baadae kuwa ananizidi)
Sasa wakati penzi likikolea Jane alikua na Kaka yake ambaye nilikua tu namwona na kwa kipindi kile jamaa alikua anakula moshi (anavuta Bangi) yule Kaka yake sikuwahi kuwa karibu nae ila nilikua najua anamtaka mtoto wa aunt yule aliyefanya nijuane na Jane.
Siku natoka tuition mida ya saa 12 jioni nilikutana na kaka yake akiwa na kundi lake na wanilisimamisha nilikua naendesha baiskeli kwenda home. Jamaa alinipiga beat na kusema natoka na dada yake, atanitafuta, pale asingeweza kufanya kitu kwani tulikua road.
Asee niliogopa sana nikaenda home straight kwa Dada (yule mtoto wa aunt tumwite Tiva)
Tiva alimind sana akanambia twende, kufika kule alimfokea sana jamaa na jamaa akasema hajasema kitu kibaya kwangu na hawezi kunigusa maana sijamkosea kitu.
Kun siku tuko shuleni, muda wa break Jane alikua ananifata kwenye dawati langu na kuongozana hadi jikoni kupata chai (BUKOBA SEC ilikua na utaratibu wa kugawa maandazi na chai kwa kila mwanafunzi na ilikua buree, utaratibu uliwekwa kwa members yaani wanafunzi mnakua na makundi ya watu 12 na kiongozi ndo anafata maandazi na chai then anawagawia)
Sasa huu utaratibu sikua nimeuzoea sababu kule Mwanza hamna mambo hayo, pili sikua nimezoea sana kuongea na watu, tatu kulikua na vurugu flani hivi. Jane ndo mtu pakee alikua ananichukulia maandazi na kuniletea kwenye Table yetu pale canteen then tunakula. Siku nyingine nilikua siendi kabisa Canteen. Sasa kuna siku nilimwambia siendi yeye akatangulia then baadae akili ikanambia niende nikanunue Karanga za bubu (zilikua maarufu sana na muuzaji alikua bubu). Wakati nanunua karanga nikamwona Jane yuko Posta (Bukoba sec iko karibu na ofisi za posta) anaongea na jamaa hivi ambaye sio mwanafunzi. Wivu ukanijaa na nikachukia sana na aliniona.
Nikarudi class na sikusema kitu, jioni muda wa kutoka akaja kunichua kwa desk yangu tuindoke nikamwambia asinifate tena na asinizoee, nilikua na ujinga mwingi asee.
Jane aliondoka hakutaka kudraw atention yoyote pale maana wengi walikua hawajui kama tunadate.
Jioni alikuja home kuniulizia na akaambiwa niko Tuition. Home hawakua na wasiwasi wanajua tunasoma wote. Usiku akaja tena na nikamkazia nikasema sitaki mahusiano tena. Aliniomba msamaha na kunidanganya yakaisha.
Nakumbuka Jane alikua akiniletea pesa na vijizawadi sana.
Sasa kumbe sakata la yule kaka yake Jane kusema atanitafuta lilikua limetengenezwa na jamaa flani alikua anamtaka sana Jane ila Jane anakaza, jamaa aligundua Jane ana mahusiano na mimi.
Nakumbuka hiyo siku nikua natoka tuition, mida ya saa moja jioni giza tayari limeingia, nikiwa njiani kabisa kufika home, ile sehemu yenye shamba la miwa ambako nilikiss mara ya kwanza na jane. Nilikutana na jamaa wawili wakanisimamisha, wakati nashuka kwenye baiskeli niwasikilize asee nilipigwa ngumi moja ya uso hadi chini… Sikujua napambana nao vipi nikajikuta nimebaki chini pale kama nimezima ili wasiendelee maana wangenipasua.. Jamaa wakakimbia (mmoja alikua yule anayemtaka Jane na nilikua namjua sababu Jane aliwahi nionyesha)
Walivyokimbia nikaamka nduki nikaenda nyumbani na nilikua na uoga sana ikabidi nimwambie Aunt kuwa watu flani wamenivamia na kunipiga kisa Jane (nilikua na utoto mwingi). Aunt alichukia na akasema twende kwao Jane ila tupite kwa balozi kwanza kutoa taarifa then tukaenda kwao na Jane
Itaendelea…