Alien pilot
Senior Member
- Dec 29, 2017
- 194
- 225
Ndugu zangu,
Kama nilivoandika kichwa cha habari mimi ni kijana niliye ajiriwa na mapato yangu kwa mwezi nikama 2,000,000 hivi.
Lakini nimekosa furaha kiasi kwamba sina furaha na maisha pamoja na watu wanaonizunguka hata hiyo pesa yote huishia kumaliza matatizo ya ndugu na kila mwanamke naingia naye kwenye mahusiano basi hata anza kuumwa kiasi pesa yote inaenda kumhudumia mgonjwa.
Sasa najiuliza nitakuwa nimerogwa au na kipindi hiki ndo nimekosa kabisa ujasiri wa maisha sasa je hiyo hali ya kawaida au kuna michezo ya kiswahili nafanyiwa na kama yupo mganga anitibie nikipona ndo namlipa maana nimeenda kwa hawa wa upako naona maigizo kabisa mtu ananiombea sijazimia ananilazimisha kuniangusha na wale wasaidizi wanashika kwa nguvu kama nina matatizo wakati nipo vizuri, ndo nikaona wote hawa maigizo.
Nimeenda kama kwa wa upako wa nne hivi wote hivohivo.
Sijui nifanye nini.
Kama nilivoandika kichwa cha habari mimi ni kijana niliye ajiriwa na mapato yangu kwa mwezi nikama 2,000,000 hivi.
Lakini nimekosa furaha kiasi kwamba sina furaha na maisha pamoja na watu wanaonizunguka hata hiyo pesa yote huishia kumaliza matatizo ya ndugu na kila mwanamke naingia naye kwenye mahusiano basi hata anza kuumwa kiasi pesa yote inaenda kumhudumia mgonjwa.
Sasa najiuliza nitakuwa nimerogwa au na kipindi hiki ndo nimekosa kabisa ujasiri wa maisha sasa je hiyo hali ya kawaida au kuna michezo ya kiswahili nafanyiwa na kama yupo mganga anitibie nikipona ndo namlipa maana nimeenda kwa hawa wa upako naona maigizo kabisa mtu ananiombea sijazimia ananilazimisha kuniangusha na wale wasaidizi wanashika kwa nguvu kama nina matatizo wakati nipo vizuri, ndo nikaona wote hawa maigizo.
Nimeenda kama kwa wa upako wa nne hivi wote hivohivo.
Sijui nifanye nini.