Jugado
JF-Expert Member
- Oct 28, 2021
- 1,449
- 3,134
Habari.
Nina miaka 37. Sifurahii maisha katika umri huu. Kama kuna mtu anaweza kutoa ushauri wa kunikomboa asisite, Mshana Jr n.k. Mtiririko wa matukio ni kama ufuatavyo;
1. Ninafanya kazi Serikalini mshahara take home ni 1.3 m, hapo nina mkopo wa miaka 5 NMB.
2. Kazi nimeanza tangu 2012, hivyo nina miaka 9+ kazini.
3. Naishi Dar es Salaam.
4. Nina mke na watoto wanne, mtoto wa nne bado ni kichanga.
5. Tangu nianze kazi sijui pesa zangu zinapoenda, sina kiwanja, sina akiba, bado nimepanga, kodi laki tatu kwa mwezi.
6. Mahusiano yangu na mke siyo mazuri sana kwa sababu ya ugumu wa maisha, lakini bado tunasonga.
7. Mke hana kazi, hana biashara.
8. Nakunywa pombe mara kwa mara.
9. Siendi kanisani kabisa ila kwa matukio maalum mfano ndoa, ubatizo wa mtoto, n.k.
10. Sina gari, nilioanza nao kazi wana nyumba kubwa na magari mawili, moja la mke.
Nahisi nina mkosi, nifanye nini? Yapo mengi kuonesha hasara ninayoihisi. Kazini napata marupurupu ya hapa na pale, ila najiona sitoboi. Wadogo zangu wenye mshahara wa laki tano wametoboa mi nipo nipo tu mpaka mama yangu amekata tamaa. Faraja yangu iliyobaki ni binti zangu ambao hawaelewi chochote kwenye hii Dunia ya vita.
Nina miaka 37. Sifurahii maisha katika umri huu. Kama kuna mtu anaweza kutoa ushauri wa kunikomboa asisite, Mshana Jr n.k. Mtiririko wa matukio ni kama ufuatavyo;
1. Ninafanya kazi Serikalini mshahara take home ni 1.3 m, hapo nina mkopo wa miaka 5 NMB.
2. Kazi nimeanza tangu 2012, hivyo nina miaka 9+ kazini.
3. Naishi Dar es Salaam.
4. Nina mke na watoto wanne, mtoto wa nne bado ni kichanga.
5. Tangu nianze kazi sijui pesa zangu zinapoenda, sina kiwanja, sina akiba, bado nimepanga, kodi laki tatu kwa mwezi.
6. Mahusiano yangu na mke siyo mazuri sana kwa sababu ya ugumu wa maisha, lakini bado tunasonga.
7. Mke hana kazi, hana biashara.
8. Nakunywa pombe mara kwa mara.
9. Siendi kanisani kabisa ila kwa matukio maalum mfano ndoa, ubatizo wa mtoto, n.k.
10. Sina gari, nilioanza nao kazi wana nyumba kubwa na magari mawili, moja la mke.
Nahisi nina mkosi, nifanye nini? Yapo mengi kuonesha hasara ninayoihisi. Kazini napata marupurupu ya hapa na pale, ila najiona sitoboi. Wadogo zangu wenye mshahara wa laki tano wametoboa mi nipo nipo tu mpaka mama yangu amekata tamaa. Faraja yangu iliyobaki ni binti zangu ambao hawaelewi chochote kwenye hii Dunia ya vita.