Maisha yanachanganya sana

Maisha yanachanganya sana

Matatizo mengi ya ajira katika nchi yetu yanasababishwa na vijana kung'ang'ania dar badala ya mambo kuyaendea kombo kuna jamaa mmoja alipata kazi serikalini akapangiwa shinyanga akasema mi kijana siwezi kuishi porini huko wanaishi wazee kipindi hicho anafanya kazi private sector mkataba private umeisha kaja boss mpya hajamuongezea sasa hivi anataka kazi yoyote na mke na watoto.

Tusing'ang'anie dar maana mpaka tukija kushtuka mda umeenda na tumeshachelewa.
Ni kweli kaka ahsante pia kwa ushauri mzuri
 
Ndio sasa kashaamua mi nitafanyaje na jamaa ni mtu mwenye taasisi kubwa ya kielimu kwa watu wanaofaham kuwa ni kaka yangu wananiita boss, wakishua ila hawajui ugumu wa maisha naopitia. Kifupi sijawahi kupewa hata elfu 10 tu ya kununua suruali toka nifike hapa dar, kuhusu mavazi yote najitegemea na pesa ya kula huwa naachiwa kiduchu sana na kingine huyo kaka yangu bado ajaoa tunaisho wawili tu mimi na yeye. Najiskia vibaya sana maana mtaani watu wanajua nina hela nyingi kumbe sina hata shilingi sometime naona hata aibu kujichanganya hapa mtaani kupiga vibarua coz cv ya brother inatisha na itafanya jamii ishangae kuona mafanya kazi vibarua wakati ndugu yangu yupo njema.
Kingine pamoja nayeye kumiliki idadi yote hiyo ya magari ajawahi kuniruhusu hata kujifunza kuendesha gari mpaka watu huwa wanamwambia kwanini usimuachie dogo mashine nae avimbe mtaani siku moja moja anaishia kucheka tu.
Una ndugu nae vipi ?

Hii si kawaida
 
Huko kisemvule Kuna viwanda vya kutengeneza bidhaa gani na bidhaa gani hasa
emoji1666.png
[emoji16vi

Huko kisemvule Kuna viwanda vya kutengeneza bidhaa gani na bidhaa gani hasa
Viatu yeboyebo,mabegi,mikanda,Nondo, plastic material,pikipiki , gypsum, Tiles,mabati,maji,cement
 
Fanya nilichokushauri, kama unajuwa kuendesha gari na pikipiki ingia mtaani utanikumbuka.

Bodaboda sasa hivi ndio wanaotesa mtaani, wana quick money za kuhonga kina Mwajuma nchokonowe.

Ukiwa driver ni rahisi kupata mishe za driving project kila siku zipo zinahitaji madereva.

Cha msingi sasa hivi upate take off kianzio kwanza.

Halafu ninayekushauri mwenzako ni jobless nina mke na watoto wanasoma English medium, kuna bill ya Dawasa, luku, Dstv, takataka, ulinzi shirikishi na daily nourishment.

Bongo ya sasa usiwaze kuajiliwa, ajira itakufuata ukiwa tayari upo golini kwako maisha yanasonga.
Sasa kama ni jobless unaweza vipi kulipa bills zote hizo
 
Ndio sasa kashaamua mi nitafanyaje na jamaa ni mtu mwenye taasisi kubwa ya kielimu kwa watu wanaofaham kuwa ni kaka yangu wananiita boss, wakishua ila hawajui ugumu wa maisha naopitia. Kifupi sijawahi kupewa hata elfu 10 tu ya kununua suruali toka nifike hapa dar, kuhusu mavazi yote najitegemea na pesa ya kula huwa naachiwa kiduchu sana na kingine huyo kaka yangu bado ajaoa tunaisho wawili tu mimi na yeye. Najiskia vibaya sana maana mtaani watu wanajua nina hela nyingi kumbe sina hata shilingi sometime naona hata aibu kujichanganya hapa mtaani kupiga vibarua coz cv ya brother inatisha na itafanya jamii ishangae kuona mafanya kazi vibarua wakati ndugu yangu yupo njema.
Kingine pamoja nayeye kumiliki idadi yote hiyo ya magari ajawahi kuniruhusu hata kujifunza kuendesha gari mpaka watu huwa wanamwambia kwanini usimuachie dogo mashine nae avimbe mtaani siku moja moja anaishia kucheka tu.
Unaweza kukuta hela za masharti hizo unamlaumu bure bro. We achana naye kama zipo mishe usione noma.
 
Njoo urafiki unakunjia post au nichek kesho tuende wote ukapate kazi kiwanda cha mifuko wanalipa vzr ila mlipo ni wiki kwa wiki nichek inbox nikusaidie
 
Akili za wabongo ziko demented , yaani eti anamshauri mtu akabebe viloba Kwa bakhresa wakati Kaka take huyo mtu anauwezo Tu WA kumpa kianzio cha hata biashara ndogo Huyu ndugu hapa , Huu ujinga Huu ndio maana wananchi hii nchi wanaishi kama manamba (kutumikishwa zaidi ya punda tena Kwa ujira mdogo Sana ) , aliyewahi kufanya kazi kwenye viwanda vya makanjibai na wachina ataelewa ninaloongea hapa .
Tuache akili za kimasikini waTanzania
Unauhakika ni ndgu yake wa tumbo moja? au ww hujui unaweza kusaidiwa na mtu ambaye hata sio ndg yako kwa urahisi zaidi kuliko wa tumbo moja?
 
Ni kaka yangu tumbo moja namaanisha ni baba na mama mmoja na ana gari tatu za school bus na noah moja ya kutembelea na hizo school bus zote kaajili watu lakini mimi ndugu yake nipo mtaani naangaika
Utakuwa na tatizo sehemu jiangalie
 
Daaah!! Maisha yanachanganya sana.

Nipo dar takriban miez 6 sasa nililetwa na ndugu yangu toka mkoani kwa ajili ya mchongo flani ila kwa bahati mbaya mambo hayakwenda kama tulivyopanga nikawa nimefeli.

Ndugu yangu sio kinyonge ni mtu mwenye maisha yake safi tu sio tajiri ila ana magari kama matatu hv na taasisi yake inayojishughulisha na maswala ya elimu.

Sasa Baada ya ule mchongo kufeli ndugu yangu huyo jana akaniweka chini akaniambia,
"Mdogo wangu nishakuleta mjini tayari na mji ushaujua sasa usikae tu home inabidi ujichanganye hata mimi nilianzia maisha duni sana nililala nje lakini leo mambo yangu yamenyooka hivyo nawewe anza kujitafuta mapema, kuhusu kulala nitakusimamia mimi ila vitu vingine inabidi ujitafutie mwenyewe ili akili yako ikae sawa na pia uanze kujitegemea mapema maana ushakuwa mtu mzima, Sifanyi hivi ili nikutese hapana nafanya hv ili nikusaidie na usiwe tegemezi.

Nikamwambia sawa kaka nimekuelewa wazo lako nitalifanyia kazi.

Sasa ndugu zangu hili swala nimelileta kwenu mnisaidie idea, mawazo yoyote ni vipi nitaweza kusurvive hapa mjini, hata kama kuna viwanda vinavyotoa kazi za kulipwa kwa siku mnielekeze vinapatikana wapi. Maana mimi bado sijawa mwenyeji sana hapa jijini. Kiufupi ni kwamba sichagui kazi yoyote ili mradi tu nisiwe nimevunja sheria za nchi.

Naombeni mawazo yenu ndugu zangu kiukweli napitia nyakati ngumu sana, sijui nianzie wapi kutafuta hata pesa yakula natanguliza shukrani na karibuni kwa mawazo yenu.
Tafuta mkaa na jiko Kisha tafuta mahala palipochangamka ,choma kuku Kwa moto wa makaa,mwambie huyo bro akupe mtaji,fanya hii kitu nyakati za usiku

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Maisha ya Dar ukipata sehem ya kula na kulala wew tayar umetoboa.
Rafik yangu wa mtaani Zombie alinipeleka kiwanda cha kutengeneza kanga, vitenge na Mashuka cha NIDA njia panda ya kwenda Tabata. Hakika alinifunza mengi sana.
Haki
 
Ushauri wangu rudi kijinini kwenu Tafuta panga jipya jembe jipya na uwe na mkebe wako wa chakula na maji pitia mashambani omba vibarua au kama kwenu mnaeneo anza kilimo cha mchicha na ujenge mahusiano mazuri na wamama wa sokoni
 
Back
Top Bottom