Maisha yanachanganya sana

Maisha yanachanganya sana

Fanya nilichokushauri, kama unajuwa kuendesha gari na pikipiki ingia mtaani utanikumbuka.

Bodaboda sasa hivi ndio wanaotesa mtaani, wana quick money za kuhonga kina Mwajuma nchokonowe.

Ukiwa driver ni rahisi kupata mishe za driving project kila siku zipo zinahitaji madereva.

Cha msingi sasa hivi upate take off kianzio kwanza.

Halafu ninayekushauri mwenzako ni jobless nina mke na watoto wanasoma English medium, kuna bill ya Dawasa, luku, Dstv, takataka, ulinzi shirikishi na daily nourishment.

Bongo ya sasa usiwaze kuajiliwa, ajira itakufuata ukiwa tayari upo golini kwako maisha yanasonga.
Kaka ww umeyawezaje maisha ya mtaani🤔
 
Mkuu kuna sehemu inaitwa Kisenvule,ipo Mkoa wa Pwani wilaya ya Mkuranga ni kilometre chache kutoka Mbagala Rangi tatu.
Una weza kwenda na kurudi kwani Magali yanapatikana k/koo pale na nauli yake kwasasa 850 mpaka huko.
Kisenvule ni Mji wa Viwanda,kuna viwanda vingi sana.%kubwa ya wakazi wake ni wafanyakazi wa viwandani,
Fika asubuhi na mapema utakuta Umati wa Watanzania wanaelekea viwandani waulize hao kazi zinaendaje watakujuza.
Kuhusu malipo inategemea na kuwinda ila malipo ya chini ni 5000 per day
Huko kisemvule Kuna viwanda vya kutengeneza bidhaa gani na bidhaa gani hasa
 
Ninachokiongea sio kitu cha kutunga na hizi ndio baadhi ya vitu anavyomiliki brother
Hiki ulichokifanya sio kizuri...Kama Kuna uwezekano wa kufuta futa.sio sawa kuanika Mali za Kaka yako mtandaoni ni hatari halafu hapa jf watu wengi so wanaweza kuona huu Uzi na hii picha wakampa taarifa bro..utaonekana limbukeni
 
Inasikitisha sana, labda anakupima uvumilivu wako, akili na upambanaji wakati anakuandalia kitu kikubwa cha kukutoa coz naamini damu nzito kuliko maji.
Sijui lakini sina imani na hicho unachokisema maana mara nyingi amezoea kusema kwamba pesa zake katafuta mwenyewe na hiyo kauli huwa anamwambia sana mama pale anapomsihi awasaidie sisi ndugu zake
 
Hakuna Jiji hatari Africa na huenda duniani kwa ujumla kama City of Johannesburg, lakini watu ili wasurvive maisha nimeona pale wageni wengi tu wanachangamkia kazi za security ambayo ni most dangerous job katika mji ule maana wakija huwa wanauwa tu.

Successful is for risk takers.
Sawa kaka nimekuelewa
 
Hiki ulichokifanya sio kizuri...Kama Kuna uwezekano wa kufuta futa.sio sawa kuanika Mali za Kaka yako mtandaoni ni hatari halafu hapa jf watu wengi so wanaweza kuona huu Uzi na hii picha wakampa taarifa bro..utaonekana limbukeni
Nimeshafuta mkuu
 
Nipo fizikali fiti kaka na malipo yao huwa yapoje
Kwa wastani ni elfu kumi kwa siku (maana kuna vitengo mbalimbali), siku moja nenda ukajiridhishe (kwa kuuliza kazi zilizopo na malipo yake) kwanza kisha ndo uchukue maamuzi ya kuanza hicho kibarua
 
Nakazia hapa naufahamu mziki wake hahahaha kibeba viroba kutoka kwenye mkanda wa mashine s mchezo bado matusi ya wakongwe pale
Kuna jamaa angu wa karibu alikwenda pale alinipa habari za pale na namna alivyokua (alianza kuumwa mwili hasa mgongo na mabega), nilighairi kujiunga nae pale kiwandani baada ya kuona naweza kukata moto hivi hivi, maana yeye alikua baunsa 6 pack flani afu mi one pack
 
Asee, Familia zetu za kiswahili roho mbaya zinaanzia hata kwa walokusomesha, mzazi ana uwezo ila ni bandidu hatariii, sijui anadhan akinisaidia nitampita!
Inasikitisha sana kaka na ndio maana familia zetu hizi kukuwa kiuchumi inakuwa ngumu sana
 
Kwa wastani ni elfu kumi kwa siku (maana kuna vitengo mbalimbali), siku moja nenda ukajiridhishe (kwa kuuliza kazi zilizopo na malipo yake) kwanza kisha ndo uchukue maamuzi ya kuanza hicho kibarua
Ahsante kaka kwa kunipa mwanga kesho nitaenda huko
 
Kuna jamaa angu wa karibu alikwenda pale alinipa habari za pale na namna alivyokua (alianza kuumwa mwili hasa mgongo na mabega), nilighairi kujiunga nae pale kiwandani baada ya kuona naweza kukata moto hivi hivi, maana yeye alikua baunsa 6 pack flani afu mi one pack
Kaka mbona unanivunja moyo aisee maana mimi sina six pack hata moja yani ni half pack sasa sijui hizo kazi ntaziweza kweli
 
Kaka mbona unanivunja moyo aisee maana mimi sina six pack hata moja yani ni half pack sasa sijui hizo kazi ntaziweza kweli
Hapana mkuu sina lengo la kukuvunja moyo ila nilikua namdadavulia huyo jamaa kitaswira zaidi. Unaweza kua one pack au half ila ukazimudu hizo kazi maana kinachotumika ni nguvu zaidi na si unajua kila mwanadamu ana nguvu tofauti na mwenzie, jitahidi hiyo kesho uliosema utaenda ukajiridhishe. Pia kumbuka nilisema vitengo vinatofautiana hivyo utakuta kuna vitengo vina unafuu na utumiaji wa nguvu so sana kama vitengo vingine.
 
Mdogo wangu nishakuleta mjini tayari na mji ushaujua sasa usikae tu home inabidi ujichanganye hata mimi nilianzia maisha duni sana nililala nje lakini leo mambo yangu yamenyooka hivyo nawewe anza kujitafuta mapema, kuhusu kulala nitakusimamia mimi ila vitu vingine inabidi ujitafutie mwenyewe ili akili yako ikae sawa na pia uanze kujitegemea mapema maana ushakuwa mtu mzima, Sifanyi hivi ili nikutese hapana nafanya hv ili nikusaidie na usiwe tegemezi
Mkumbushe huyo ^nduguyo^ ajfunze kuweka nukta kila baada ya sentensi moja kamili. Au ndivyo anakufundisha kujichanganya mjini, maana nawe ushamwiga tayari?
 
Kila la kheri, ngoja waje kukupa miongozo...
 
Matatizo mengi ya ajira katika nchi yetu yanasababishwa na vijana kung'ang'ania dar badala ya mambo kuyaendea kombo kuna jamaa mmoja alipata kazi serikalini akapangiwa shinyanga akasema mi kijana siwezi kuishi porini huko wanaishi wazee kipindi hicho anafanya kazi private sector mkataba private umeisha kaja boss mpya hajamuongezea sasa hivi anataka kazi yoyote na mke na watoto.

Tusing'ang'anie dar maana mpaka tukija kushtuka mda umeenda na tumeshachelewa.
 
Hapana mkuu sina lengo la kukuvunja moyo ila nilikua namdadavulia huyo jamaa kitaswira zaidi. Unaweza kua one pack au half ila ukazimudu hizo kazi maana kinachotumika ni nguvu zaidi na si unajua kila mwanadamu ana nguvu tofauti na mwenzie, jitahidi hiyo kesho uliosema utaenda ukajiridhishe. Pia kumbuka nilisema vitengo vinatofautiana hivyo utakuta kuna vitengo vina unafuu na utumiaji wa nguvu so sana kama vitengo vingine.
Ahsante mkuu ntaenda kujiridhisha
 
Back
Top Bottom