Maisha ya sasa ya msanii Saida Karoli

Maisha ya sasa ya msanii Saida Karoli

Sina chuki na Wasukuma mkuu. Ila kama umeamua kuongelea Ushamba basi dalili mojawapo ni hii ya kushindwa kutambua upi UTANI ipi CHUKI.

Sidhani kama Ushamba una uhusiano na Kabila.
Ni kweli ushamba hauna uhusiano na kabila, sasa kwanini useme ni wasukuma na siyo wale wanaotuita sisi washamba ndo wanasema hayo maneno?
 
Saida karoli na wasanii wengine kama Q chief walikubali kuuza haki zao zooote za muzikikwa maharamia.

Huyu Saida nadhani alimuuzia Felician Mutta(fm studios)

Q chilla aliuza kwa chief kiumbe haki zoote.

Hata diamond almanusura anase kwenye mitego hiyo, sema yeye alivyojitoa akaambiwa arudishe gari alilopewa
Ukimsikiliza Master J kwenye interview zake mbalimbali ndio unapata picha kwamba Hawa wanamziki wakongwe ni wajinga hawapaswi kuonewa huruma kabisa .
 
Huyu mama sidhani kama ana maisha hayo magumu....
Kwa miaka kadhaa show zake anapiga migodini na miji midogo akiwa na wasanii kama best naso.
Pia uganda anapata show sana huko.... Sina hakika na hilo ulilosema
Labda useme haonekani kwenye majukwaa makubwa
Ali jengewa nyumba nzuri mwanza, maisha ni uamuzi binafsi.
 
Completely out of point and touch.... Tunarudi kule kule ... akili ndezi za kibongo-bongo, bishana utaelewa baadae. Umeelewa point yangu? Point yangu ni kuwa uwe msanii, uwe mkulima, uwe mfanya biashara, kwa Bongo, maisha yako unapanga wewe mwenyewe. Kwa nini unataka wasanii ndiyo wapewe special treatment? Tena kama wewe ni msanii na umeajiri watu wengi, basi unatakiwa kuwa mwangalifu sana kujua kesho yako. Na nimesema hivi siyo kwa kuponda sekta nyingine, nimesema hivi kwa wajinga kama wewe kuponda sekta nyingine na kutaka wasanii ndiyo wapewe specail treatment. Mwalimu akistaafu, akiwa na maisha mabaya utasikia ametumia pension yake vibaya, msanii akivuma sana baadae akaishiwa, utasikia ''nchi ikubuke wasanii''. Bure kabisa akili matope. Na hiyo mifano uliyotoa haiendani kabisa kabisa na nilichosema! Sasa wewe huoni umekuwa fala kiasi cha kutoona kuwa mifano unayotoa inaonyesha usanii unalipa sana hivyo ni muhimu kupanga maisha yao ya baadae?
Uwe unazingatia paragraphs ukiandika.

Endelea kuamini sanaa haiingizii taifa lolote, endelea kuamini wasanii hawana mchango wowote kwenye jamii au taifa. Endelea kuamini kila uzi JF inabidi ujadili kilimo tu, tusijadili sekta nyinginezo.

Nenda na kwenye nyuzi za siasa, ujenzi, utalii jadili kilimo na wakulima wake.
 
Uwe unazingatia paragraphs ukiandika.

Endelea kuamini sanaa haiingizii taifa lolote, endelea kuamini wasanii hawana mchango wowote kwenye jamii au taifa. Endelea kuamini kila uzi JF inabidi ujadili kilimo tu, tusijadili sekta nyinginezo.

Nenda na kwenye nyuzi za siasa, ujenzi, utalii jadili kilimo na wakulima wake.
Unajua maana ya paragraph na matumizi yake? Sikuachi... japo unabadili magoli. Hoja yangu ni hii: Kwa nini unadhani wasanii tu ndiyo wanapaswa kusaidiwa na serkali wanapokwama kimaisha na siyo raia wote wakiwamo wakulima?
 
Unajua maana ya paragraph na matumizi yake? Sikuachi... japo unabadili magoli.
Ulitakiwa utumie paragraphs usiandike kama mwenye umeme mdogo kichwani.
Kama hujui maana ya paragraph tafuta mjukuu wako au mwanao akuelekeze.
Hoja yangu ni hii: Kwa nini unadhani wasanii tu ndiyo wanapaswa kusaidiwa na serkali wanapokwama kimaisha na siyo raia wote
Uzi unajadili msanii, ndio maana nilishauri anzisha uzi wa mkulima useme jinsi wanavyopinda mgongo. Usitake watu wasijadili sanaa kisa wewe ushamba wako umeishia kwenye mapera, viazi na tikiti maji.

Ukianzisha uzi wa mkulima kusaidiwa, hatakiwi kuja mtetesi wa wasanii kukuponda kwanini unajadili wakulima badala ya wasanii.
 
Ulitakiwa utumie paragraphs usiandike kama mwenye umeme mdogo kichwani.
Kama hujui maana ya paragraph tafuta mjukuu wako au mwanao akuelekeze.

Uzi unajadili msanii, ndio maana nilishauri anzisha uzi wa mkulima useme jinsi wanavyopinda mgongo. Usitake watu wasijadili sanaa kisa wewe ushamba wako umeishia kwenye mapera, viazi na tikiti maji.

Ukianzisha uzi wa mkulima kusaidiwa, hatakiwi kuja mtetesi wa wasanii kukuponda kwanini unajadili wakulima badala ya wasanii.
I know the topic is about Saida, the singer. My point is this: why do you think that artists, such as musicians, are a special group who need special treatment from the government? Don’t you think all citizens should be treated equally?
 
Unajua maana ya paragraph na matumizi yake? Sikuachi... japo unabadili magoli. Hoja yangu ni hii: Kwa nini unadhani wasanii tu ndiyo wanapaswa kusaidiwa na serkali wanapokwama kimaisha na siyo raia wote wakiwamo wakulima?
Na mimi hili uwa linanishangaza sana kibongobongo eti msanii au mchezaji mpira kwa upuuzi wake wakushindwa kupanga maisha yake akikwama eti asadiwe au serikali imemtupa , Vipi kuhusu kuhusu raia wengine??? Yale ni maisha yake binafsi apambane tu alichezea pesa kama raia wengine haitaji "special treatment".
 
Wewe mpaka mtu kapanga nyumba analipa kodi bado unamuona kapuku, mbona tunapenda kuchukuliana poa hivi?
 
Juzi kati nikipita mjini nikasikia wimbo wa Saida nafikiri na Banana, "Mpenzi nakupeeenda". Nikajisemea hivi kuna msaani wa kike mwenye kipaji kumzidi Saida? Nikawazaaa sikuona.
 
Nimerejea Bukoba kwa likizo baada ya miaka kadhaa, na kwa masikitiko makubwa nilikumbana na hali iliyonishtua sana. Nilimkuta msanii nguli wa muziki wa asili, Saida Karoli aliyewahi kutoa nyimbo zilizopata umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi, hadi kuvuka mipaka ya Tanzania akiishi maisha ya dhiki yasiyoendana kabisa na hadhi na mchango wake mkubwa katika sanaa na utamaduni wa taifa.

Kwa sasa, Saida Karoli anaishi katika nyumba ya kupanga ya vyumba viwili, katika mazingira yasiyofurahisha, hali ambayo haistahili hata kidogo kwa msanii aliyewahi kuiwakilisha nchi yetu kimataifa kwa heshima kubwa. Hali hii inanifanya nijiulize maswali mazito kuhusu mfumo wetu wa kulinda wasanii, hasa wale waliotoa mchango mkubwa kabla ya enzi ya mifumo ya sasa ya kidijitali.

Kwa wajuzi wa masuala ya commercial entertainment, je, hakuna njia ya kusaidia wasanii kama Saida Karoli kufaidika na royalties za kazi zao walizofanya miaka ya nyuma? Je, sheria na taasisi zetu za hakimiliki zinawafikia kwa vitendo, au zipo tu kwenye maandishi?

Zaidi ya hapo, tukio hili linapaswa kuwa funzo kwa wasanii wanaong’ara kwa sasa. Umaarufu ni wa muda, lakini maisha ni ya kudumu. Ni muhimu kwa wasanii wa kizazi cha sasa kupambania sera imara za kulinda kazi zao, kudai haki zao za kisheria, kusaini mikataba yenye kuwanufaisha hadi baadaye

Kwa kweli, hali niliyoikuta imenihuzunisha sana.
Saida alidhulumiwa na Mhaya mwenzake, MUTTA.

MUTTA ndio anakula haki zote za kazi za Saida.

Saida alikuwa anaishi Mwanza na kufaya shughuli za sanaa ili maisha yasonge.

Hili la kurudi Bukoba labda kama anaumwa.
 
Hamna cha ajabu hapo. Maisha yake ni jukumu lake. Hata wewe unafanya kazi kila siku kuendesha maisha yako. Kuimba nyimbo kadhaa hakuwezi kuendesha maisha yako miaka yote. Wasanii na watu wengine walijue hilo ili waacha kuwapa watu wengine lawama.
 
Lakini wasanii wenzake walijaribu kumnyanyua mwaka 2017, 2018 kuna wasananii walimshirikisha kwenye nyimbo kadhaa na kutumia nyimbo zake za zamani.

Maisha siyo tu kupewa pesa, tatizo ni akili zetu wenyewe. Ukifikiria kwa pesa hata kidogo alizopata kwenye muziki asngeweza kufanya biashara au kilimo akajikwamua kiuchumi?

Hapaswi kulaumiwa yeyote kwa maisha ya mtu binafsi, ni hali ambazo mhusika mwenyewe huzisababisha.

Maisha haya dahh!
Sahihi. Ajilaumu mwenyewe.
Saida tulikuwa na kikundi cha watu 3 tulimuita na kuzunguka nae usukumani kila show yake kipindi kile tulikuwa tunampa milioni moja gharama za chakula na maladhi juu yetu.

Na watu walikuwa wanaingilia 1000 mtu mzima watoto 500.

Lakini kila show tulikuwa tunapata si chini ya milioni1 laki8 hadi milioni2 laki3 ndo kiwango cha juu tumewahi pata.

Kwa mizunguko hiyo tulifahamiana na madancer wake wakawa wanatuambia malipo anavyo walipa kiukweli alikuwa anawalipa kidogo mno tofauti na wasani wa kisukuma amabo wao msanii akicheza show hela yote inakuwa ya kwakwe.
Show 2 zijazo za wa madancer wake.

Haijarishi yake itabuma na ya madancer ifulike na watu hawezi kubadili.

Nataka kusemahe

Kwa kipindi hicho mizunguko aliyofanya kama angejenga nyumba ingelikamlika kabisa yaani show haikuzidi wiki3 lakini aliingiza si chini ya m13-15.

Huo ni mwaka 2014 je single jenga nyumba?

Mbona sisi tulijenga japo haikufika hiyo m13 baada ya mgawo?

Akili akili
 
Sio saida peke yake kuna wasanii wengi sana sahv hali ni tete,
 
Saida karoli alikosea sehemu tatu

kuzaa watoto wengi na baba tofauti

kukosa washauri wazuri ktk uwekezaji .

kuishi miaka mingi na watu ambao sio sahihi.


kuhusu Nyumba saida karoli anayo Nyumba hapo mwanza

but , she made some mistake nadhani na kutokuwa na Elimu .

ila kwa PESA alizopata saida karoli na mpaka sasa saida karoli hakuna tukio kubwa la wahaya na serikali kagera wakakosa kumuita.


so she is not poor , na hana umasikini wowote .

ikiwa ana rent two rooms ujue kaamua na sio kuwa anakosa hela


saida karoli nyimbo zake Ruge alimsaidia akafanya marudio na zinauzwa ktk pltfm mbalimbali
 
Wasanii waache kuishi maisha makubwa kuliko uwezo wao. Chinga anasema you make your fart bigger than your assie
 
Nimerejea Bukoba kwa likizo baada ya miaka kadhaa, na kwa masikitiko makubwa nilikumbana na hali iliyonishtua sana. Nilimkuta msanii nguli wa muziki wa asili, Saida Karoli aliyewahi kutoa nyimbo zilizopata umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi, hadi kuvuka mipaka ya Tanzania akiishi maisha ya dhiki yasiyoendana kabisa na hadhi na mchango wake mkubwa katika sanaa na utamaduni wa taifa.

Kwa sasa, Saida Karoli anaishi katika nyumba ya kupanga ya vyumba viwili, katika mazingira yasiyofurahisha, hali ambayo haistahili hata kidogo kwa msanii aliyewahi kuiwakilisha nchi yetu kimataifa kwa heshima kubwa. Hali hii inanifanya nijiulize maswali mazito kuhusu mfumo wetu wa kulinda wasanii, hasa wale waliotoa mchango mkubwa kabla ya enzi ya mifumo ya sasa ya kidijitali.

Kwa wajuzi wa masuala ya commercial entertainment, je, hakuna njia ya kusaidia wasanii kama Saida Karoli kufaidika na royalties za kazi zao walizofanya miaka ya nyuma? Je, sheria na taasisi zetu za hakimiliki zinawafikia kwa vitendo, au zipo tu kwenye maandishi?

Zaidi ya hapo, tukio hili linapaswa kuwa funzo kwa wasanii wanaong’ara kwa sasa. Umaarufu ni wa muda, lakini maisha ni ya kudumu. Ni muhimu kwa wasanii wa kizazi cha sasa kupambania sera imara za kulinda kazi zao, kudai haki zao za kisheria, kusaini mikataba yenye kuwanufaisha hadi baadaye

Kwa kweli, hali niliyoikuta imenihuzunisha sana.
Wasanii ni binadamu kama ulivyo wewe.

Usiwape uspesho wowote.
 
Back
Top Bottom