Tulizo
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 848
- 664
Kwa wabongo ni ngumu sana hatuna descipline na mpangilio na maisha yetu. wenzetu wadhungu wanaweza. Ndio maana unasikia wameenda summer holiday na vitu kama hivyo ili kuwa karibu na familia. Nina promotor wangu huyo hata siku moja hawezi kukujibu e mail ulotuma week end, na sidhani kama anafungua e mails zake za kiofisi jmosi na jpili. Akina sie hapa tunafanya kazi 24/7 hamna jmosi wala jpili na bado hatuna maendeleo. Well nachojitahidi kufanya kati ya hayo ni kutoisahau familia.
Hapo umesema 100%, ni kweli sisi ni wazembe katika kujali maisha ya familia. Ninakataa kukubali ya kwamba anachofanya mdhungu sisi tutashindwa kama tutabadili msingi wa maisha yetu. Kwa wenzetu J2 na Jumamosi ni family days..mara nyingi moja kati ya siku hizo hakuna kupika home..familia nzima inatoka na kubadili mlo kwenye restaurant. Lakini sisi baba na mama hawaoni kama ni sahihi kwani kila siku wanasimama Pub na kujichana kila siku wakisingizia foleni barabarani.
Nyumbani kuna utitiri wa Pub hadi jioni watu wanafunga barabara za uswazi na kupanga viti nje..Hebu tujaribu kukaa na watoto nyumbani tuone kama hivyo vipub vitapata wateja..Tunajifanya ni wafanyakazi..wakati tunamaliza kila siku 4 hours kwenye matanuzi kati ya saa 10 jioni hadi saa 4 usiku.. Kama tunapenda kazi kwanini tusiendelee kufanya kazi hadi saa 4 usiku na kumaliza viporo vya kesho ili tuwe free Saturday?
Mfumo mzima wa kutojali familia na sisi wenyewe ni uzembe wetu ambao tuna-uhalalisha na mambo ya uchumi, foleni, shule etc..Hatukai pamoja kama baba na mama na kujadili mambo ya family; hatukai na watoto wetu ku-observe channel gani za TV wanaangalia. Parental Control banners kwenye vipindi vya TV havina umuhimu kwetu..kwani hakuna atakayekuwa nyumbani ku-observe, kazi hiyo tumewaachia ma-house girl ambao hata kusoma hawajui..
Mimi nadhani tuanze kujibadili.. All in all, tukumbuke kuna familia ambazo tumeshavuka haya tunayoyasema..hata kwa macho tunaziona na maneno tunasikia ..kama vile .."hao wanajifanya wadhungu..yaani utamwona baba yuko busy anawaogesha watoto halafua anafua nguo...kama sio udhungu basi amerogwa na mkewe"... Basi Ndugu yangu ..ukisikia majirani wanakusema hivi..ukenue meno..ume-win game! Wewe` unaishi perfect life..na sio maisha ya uzandiki!