Maisha ni yako, usikubali kutolewa mchezoni

Intelligent businessman

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
26,123
52,861
Uzi huu nime uandika ili uwe Kama kengele ya ukumbusho, kwa kila mmoja wetu.

👉 Maana kumezuka na Mambo ambayo yame kuwa Kama kikwazo, kwa baadhi ya watu katika safari ya maisha yao.

WIVU, kila mmoja wetu ana wivu katika maisha yake.

👉Ila baadhi ya wengi wetu tumekuwa na wivu ambao si rafiki katika maisha haya.

👉Umeona mtu kajenga au ana kazi nzuri kukuzidi, mzee Pambana ufikie Malengo yako, jiulize yeye kafikaje hapo? Zidisha juhudi na si uchawi na husda.

SUALA LA MAPENZI, hapa ndo kama wabongo wengi tuliporogwa, Kama Kijana una mengi ya kuzingatia katika maisha yako.

👉USI kubali kuyumbishwa au kupoteza muda wako, eti kisa kiumbe mwenye manyoya mwili mzima.

👉Kama uhusiano huo si rafiki basi achana nao mzee, Kumbuka una mengi na watu wengi Wana kutegemea wewe mpendwa.

AMINI KATIKA WAKATI SAHIHI, ndugu haya maisha kuna watu tuna jipa stress za kipuuzi sana.

👉Eti kisa fulani ana kazi au maisha mazuri, una Anza kujiona wewe kama bwege uliye kosa mwelekeo.

👉Ina kupasa uzingatie katika barabara yako, na si njia ya mwingine.

👉Kama biashara haiendi vizuri, basi Tafuta namna ya kutafuta wateja, kwa maana Hakuna kitu kina kuwa kwa usiku mmoja.

-Learn how to hold
-Learn the right time to fold
-Learn the right time to let go.

👉 I MEAN NO MALICE TO NOBODY

FB_IMG_16954096781259436.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom