Umesema kweli.Kwa kawaida ya maumbile bin adam hukiri kwamba kuna muumba kabla hata ya kupata mwongozo kuhusu huyo muumba, na hili hutokana na jinsi alivyoumbwa yeye binafsi pamoja na vile vilivyo mzunguka mfano anga lilivyoumbwa au ardhi ilivyotandikwa milima miti pamoja na bahari, hivi ni vitu ambavyo bin adam aliyekamilika akijitazama yeye pamoja na vinavyomzunguka basi hukiri ni lazima kuna muumba, changamoto inakuja kwamba ni nani muabudiwa halisi, hapo ndio utakuta tunagawanyika.
Mkuu hiari ya kutenda ambapo ndio utashi unaousemea wewe; je mtu anawezaje kufanya bila kuwa na operating system (akili)?Nakuuliza tena unafahamu maana ya Utashi?
Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu ya Oxford Toleo la 3, maana ya Utashi ni hiari ya kutenda.
Wewe si unatangamana na watu katika jamii, katika kutangamana nao hebu nieleze umeshawahi kukutana na mtu mwenye limit ya hiari? Au huyu ana kiwango flani cha hiari?
Swali lako hilo tu wewe mwenyewe unalionaje?
Unafahamu ninachokiandika lakini?
Natamani watu hawa waelewe huu ukweli na waukubali,lakini kazi hii anaifanya mwenyewe Mola mlezi.Habari yako Mheshimiwa, Swali ulilouliza ni zuri na mchanganuo wake upo hivi.
Kuhusu yeye Mungu anafahamu kila kitu, ujuzi wake umezunguka kila kitu anafahamu ya kabla, ya yatakavyokuwa na baada ya yatakavyokuwa.
Tuje kwenye msingi wa swali lako, ni kweli Mungu anafahamu wa Motoni na Peponi ila si yeye aliyepanga hayo matokeo bali watahiniwa ndiyo waliyochagua hayo makazi. Msingi wa Imani yangu katika hilo upo hivi, kuna hali binadamu tumepewa nayo ni utashi wa kujiamulia mambo na katika hilo yeye Mungu hatuingilii, pengine kwa nini? Kwa sababu ametupa hekima na elimu pasipo kusahau kwamba una utashi wa kujiamulia juu ya utakayofanya. Kisha akatupa uhai ambao ndiyo huu mwisho wa siku tunarudi kwake kwa njia ya kifo.
Kwa vile yeye Mungu ni mjuzi wa yote anafahamu bwana "Fulani" atazaliwa kipindi Fulani na katika makuzi yake atashika njia iliyokuwa mbali na yangu kwa matashi yake yeye mwenyewe kwa sababu ndipo alipoamua yeye kuelekea, kwa muktadha huo amejidhulumu mwenyewe. Usisahau ya kwamba tuna Uhuru wa kuishi kwenye maisha haya, imma kumkufuru au kumshukuru ila mwisho wa siku marejeo kwake.
Na hayo yote ni kwamba Mungu anatuangalia kwa kuona ni yupi atakayetii amri yake pindi alipoiamrisha; kwa sababu akitaka utii amri yake utatii tu na huo uwezo anao, lakini haitokua utiifu bali ni kulazimisha na yeye Mungu hataki kulazimisha bali anaangalia ni yupi mtiifu kati yetu kwake yeye.
Halafu ni nani aliyekuambia akili na Utashi ni kitu kimoja raia mwenzangu?2. Akili kwa binadamu inaumbwa na Mungu ambapo wewe umetumia neno utashi, hii akili ni operating system kwa binadamu yeyote yule asa kwanini Mungu asimuumbe kila mtu awe na operating system iliyokamilika?
Swali je hayo unayoyafanya huwa unalazimishwa au huwa hifikirii ?Mkuu hivi anayemuumba mwizi, mzinifu, tapeli, n.k ni nani kama siyo yeye Mungu mwenyewe? Kitendo cha Mungu kujua kuwa mustakabali wa mtu atakuwa ni mzinzi kabla ya hata huyo mtu hajazaliwa basi inamaana kapanga yeye Mungu huyo mtu awe mzinzi. Hivi mfano Mungu angekuuliza kuwa #Hammaz# nakupeleka duniania ila utakuwa mwizi na mwisho wa siku utakufa ukiwa wa motoni je ungelikubali uletwe duniani?
Kitendo cha Mungu kujua litokealo kwa mtu kabla hata ya kuzaliwa maana yake kapanga yeye mtu aishije.
Mfano wewe ni fundi ujenzi na wakati umeezeka nyumba bati, ukaangalia juu ukaona kuna tobo ambalo mvua ikinyesha nyumba itakuwa inavuja, lakini hujaliziba lile tundu; maana yake umepanga nyumba iwe inavuja.
Nacheka sana bro. Naomba unieleze hizo law za Nature ni nini hasa na zinafanyaje kazi ?hapa upo sawa kabisa kitu kingine mtu mpaka afe ni kwamba amepingana na law za nature
kama wanadamu tungeweza kufuata sheria za nature basi tungeishi milele assumption tu lkn
😀😀😀
Yaani hapo mtu anae kufa anakuwaje amepingana na law za Nature ?hapa upo sawa kabisa kitu kingine mtu mpaka afe ni kwamba amepingana na law za nature
kama wanadamu tungeweza kufuata sheria za nature basi tungeishi milele assumption tu lkn
😀😀😀
Kuchezeshwa kama mdoli unataka wewe bro. Ukimakinika na ukafikiri kwa usahihi utaelewa na utafaidika sana.😀 😀 😀 mkuu huu ulimwengu unatuchezesha kama midoli aise...
Tizama post #186Mkuu hiari ya kutenda ambapo ndio utashi unaousemea wewe; je mtu anawezaje kufanya bila kuwa na operating system (akili)?
Kumuumba mtu ambaye anatambua kuwa atakuwa ni muovu maana yake ni kwamba amepanga awe muovu kama hakupanga awe muovu kwanini asimuumbe huyo mtu awe mkamilifu? Umezungumzia swala la utashi, je anayeumba mtu mwenye utashi mdogo ni nani?
Na kwavile Mungu alishajua kuwa huyo mtu atakuwa muovu akiletwa duniani; inamaana hata ashuke Yesu kumuhubiria au mtume Muhamad (S.A.W) ampe mawaidha kiasi gani hakutobadilisha hatima ya mtu huyo.
Kwanini ?Mkuu baada ya kifo hakuna maisha tena
Habari yako Mheshimiwa, Swali ulilouliza ni zuri na mchanganuo wake upo hivi.
Kuhusu yeye Mungu anafahamu kila kitu, ujuzi wake umezunguka kila kitu anafahamu ya kabla, ya yatakavyokuwa na baada ya yatakavyokuwa.
Tuje kwenye msingi wa swali lako, ni kweli Mungu anafahamu wa Motoni na Peponi ila si yeye aliyepanga hayo matokeo bali watahiniwa ndiyo waliyochagua hayo makazi. Msingi wa Imani yangu katika hilo upo hivi, kuna hali binadamu tumepewa nayo ni utashi wa kujiamulia mambo na katika hilo yeye Mungu hatuingilii, pengine kwa nini? Kwa sababu ametupa hekima na elimu pasipo kusahau kwamba una utashi wa kujiamulia juu ya utakayofanya. Kisha akatupa uhai ambao ndiyo huu mwisho wa siku tunarudi kwake kwa njia ya kifo.
Kwa vile yeye Mungu ni mjuzi wa yote anafahamu bwana "Fulani" atazaliwa kipindi Fulani na katika makuzi yake atashika njia iliyokuwa mbali na yangu kwa matashi yake yeye mwenyewe kwa sababu ndipo alipoamua yeye kuelekea, kwa muktadha huo amejidhulumu mwenyewe. Usisahau ya kwamba tuna Uhuru wa kuishi kwenye maisha haya, imma kumkufuru au kumshukuru ila mwisho wa siku marejeo kwake.
Na hayo yote ni kwamba Mungu anatuangalia kwa kuona ni yupi atakayetii amri yake pindi alipoiamrisha; kwa sababu akitaka utii amri yake utatii tu na huo uwezo anao, lakini haitokua utiifu bali ni kulazimisha na yeye Mungu hataki kulazimisha bali anaangalia ni yupi mtiifu kati yetu kwake yeye.
Ikiwa Mungu anajua ya kuwa Zurri akizaliwa atakuwa ni mwizi ila kamuumba hivyo hivyo, je inawezekana Zurri akaja duniani na asiwe mwizi?Swali je hayo unayoyafanya huwa unalazimishwa au huwa hifikirii ?
Ukinijibu hilo ujiandae kwa maswali mengine yatakayo tokana majibi yako.
Mkuu umedandania comments bila kuangalia msingi wa hoja yangu. Nimeuliza hivi kipi tuamini kati ya hivi vitu viwili?Kaka unauliza maswali mepesi sana. Umeshawahi kujiuliza kwanini Mola alileta mitume ?
Kwanini kwake yeye Mola kuna msamaha ?
Je kuna mtu ushawahi kumuuliza akajua yeye ni wa motoni au wa peponi ?
Tatizo lenu nyinyi huwa hamfikirii mambo kiundani.
Kaka leo kaa chini jiulize maswali haya,imekuwaje leo umejua kusoma na kuandika ?
Inakuwaje leo unatafuta hela na unapata ? Unafikiri ni kwa ujanja wako na maarifa yako ? Kama ni kwa ujanja wako na maarifa,kwa viwili hivyo mbona kuna wakati unatafuta na unakosa ?
Mola wetu ametupa neema kadha wa kadha,leo hii ona binadamu anavyo mkufuru na kumkana yeye lakini ana mpa rizki,na neema kadha wa kadha ?
Kaka kaa tenga muda ufikiri kinyume na unavyofikiri na yeye Mola anawapenda wale wenye kutumia akili.
Kauli hii huwa naitumia mara kadhaa kuwaambia wale wanaomkana Mola muumba,wajaribu kufikiria kinyume na wanavyofikiria bila shaka watambaukiwa na mengi wasiyoyajua.
Mkuu umedandania comments bila kuangalia msingi wa hoja yangu. Nimeuliza hivi kipi tuamini kati ya hivi vitu viwili?
1)Mungu mwenyewe anaamua watu gani waende peponi na watu gani waende motoni. Kwavile yeye ndiye anayemuumba mtu na pia kabla hajamleta mtu duniani anajua mwanzo hadi mwisho wa huyo mtu utakuwaje. (Anajua alichokipanda na kitakachoota)
Au
2) Mungu hajui mwanzo(kabla ya mtu kuzaliwa)na mwisho wa mtu utakuaje hivyo jitihada au makosa yaweza kubadilisha hatima ya mtu (anajua alichokipanda ila kitachoota hajui)
Hilo jibu umeliona wewe, mimi sijaona ulipojibuKaka nimekujibu vizuri sana nukta zako mbili tena kwa kuweka wazi kile kilichomo katika nukta hizo,soma tena utaelewa.