Maisha 2070: Una nini cha kuacha kama kumbu kumbu hapa JamiiForums

Fundi manyumba

Senior Member
Nov 25, 2018
177
290
Habari zenu wana Jamii Forums, hususani jukwaa hili la "ChitChat".

Ni tumaini langu wote ni wazima.
Huu uzi yawezekana ukawa mrefu kuusoma, ila naamini kuna mtu utamsaidia sana endapo atausoma mpaka mwisho.

Kuna vitu vingi vinatokea katika maisha tunavichukulia kawaida but Ushawahi kujiuliza je 2070 takua wapi…?

Hata kama uhauitokuwepo je kuna athari gani utakua nimeacha… ?

Tuongelee kwa hapa jf tu.
Je ni watu wangapi watakuwa Jamii Forum ifikapo mwaka 2070?

Katika hali hii Fundi manyumba hapa nimepiga mahesabu yangu nikajikuta nabubujikwa na machozi ya huzuni kwani itapungua kwa kasi zaidi kuliko kawaida,

Kama kwa sasa tupo 667,812 kati ya watu milioni 29 ya wanatumia internet. kufikia mwaka 2070.
natabiri idadi ya watu jamii forum itapungua .

Mfano
Members ambao wamezaliwa 1980
Kwa wakati huo, watakuwa na umri wa karibu miaka 90 hivi. Wanaweza kuwa mashuhuda wa mabadiliko mengi katika
maisha yao, ikiwa ni pamoja na maendeleo makubwa katika teknolojia, utamaduni, na jamii.

Wakati huo, wanaweza kuwa
wamepitia vipindi tofauti vya historia na kushuhudia mageuzi mengi ya kijamii na kiteknolojia.

Lakini kwa uhalisia life
expectancy yetu kufika 90 ni majaliwa, hivo kama wewe ni miongoni mwao anza mapema kuandaa kitu humu ambacho
kwa miaka hiyo members wenzako wakukumbuke.

Kwa members aliyezaliwa miaka ya 1990 .
Wanaweza kuwa na umri mkubwa kama miaka 80 hivi lakini bado wana nafasi ya kushuhudia mabadiliko makubwa katika
teknolojia, utamaduni, ila kwa bongo bongo kufika 80 kuna changamoto ishu za macho n.k

Mybe uwe na life style nzuri hapo
utakuwa na safari ya kusisimua kushuhudia jinsi dunia itakavyo badilika katika kipindi hicho.


Kutabiri maisha mwaka 2070 moja kwa moja ni ngumu sana kwa sababu mambo mengi yanaweza kubadilika kati ya sasa na wakati huo.

Teknolojia itakuwa imeendelea sana, na mabadiliko ya kijamii, kiuchumi, na mazingira yanaweza kuathiri jinsi tunavyoishi.

Ni ngumu kutabiri kabisa mustakabali wa jamii forum, lakini inaonekana kwamba mtandao huu wa jamii forum utaendelea kuwepo kwa
miaka mingi ijayo.

Hata hivyo, inaweza kufanyiwa mabadiliko makubwa katika muundo wake, sheria za faragha, na jinsi watu wanavyoitumia.

Teknolojia mpya inaweza kubadilisha jinsi tunavyoshirikiana mtandaoni, lakini dhana ya kushiriki maoni,na picha
inaweza kuendelea kuwa sehemu muhimu ya utamaduni wetu wa kidigitali

Hivyo basi acha alama Kama ni picha sawa, Ifike siku iwe kumbukumbu kwako kwa kile ambacho ulikiweka humu ukiwa katika hali fulani.
DUNIA.jpg
Shukran
 
Back
Top Bottom