USHINDI KWA LOWASSA (UKAWA, CHADEMA)NI LAZIMA, MAANA NI MPANGO WA MUNGU.
Maana MUNGU anasema hivi, Kwa sababu hiyo, MIMI nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, "kazi ya ajabu na muujiza " na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa. Isaya 29:14.
Kazi ya ajabu ni kama vile alivyowavusha Israeli katika bahari ya sham.
Ayubu 42:2~ imeandikwa, Najua yakuwa waweza kufanya mambo yote, Na makusudi yako hayawezi kuzuilika. Anamaanisha, anachopanga MUNGU mwanadamu, kwa nafasi yake, akili yake, kwa nguvu zake, kwa hekima yake ya kidunia, kwa jina lolote alilonalo katika dunia hii kamwe hawezi kuzuia kusudi la MUNGU kutimia kwa aliyemkusudia, hata mumchafue kivipi!
Ndiyo maana anasema tena hivi, Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni "nguvu ya MUNGU". Kwa kuwa imeandikwa, Nitahiharibu hekima yao wenye hekima,
Na akili zao wenye akili nitazikataa.
Ina maana yeyote atakaye waza au kutaka kubadili matokeo halali ili kuzuia kusudi la MUNGU, akili hizo atazikataa, na hiyo hekima ya kibinadamu ataiharibu. 1Korinto 1: 18-19
Mwenye sikio na asikie Roho anasema na Watanzania.
Amani ya Yesu iwatawale mioyoni mwenu