Mahari shilingi milioni 5?

Mahari shilingi milioni 5?

Tony Laurent

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2011
Posts
6,385
Reaction score
8,279
Leo nimemsikia mtu mmoja akisema kuwa ndugu yao anaejiandaa kuoa, amepangiwa mahari ya shilingi milioni tano. Na kwamba ndugu wameamua kuchangishana ili walipe mahari hiyo kumsaidia ndugu yao.

Kilichonifanya niilete mada hii hapa kwa majadiliano ni kuhusu kiwango hicho cha mahari, ambacho kwangu nakiona ni kikubwa sana. Je, hiyo si ni sawa na kumfanya binti kama bidhaa kweli.


 
Kamanda, hiyo mi sishangai,hii ni mara ya nne kusikia mahari hii na watu kulalamika.Kwa mfano dini yetu(Muslim) mtoto wa kike ndio anayetaja mahari, na mahari hutaja yeye kwa sababu ndio anayeolewa na kufahamu kipato cha mumewe mtarajiwa.

Kwahiyo kama binti ndio ametaja na mume mtarajiwa amekubal hakuna shida na ile inakuwa ni zawadi kwa mke,ila kama ni wazazi wamesema hiyo Mahari,duuuh wanauza mtoto hapo na kufidia ada walzomsomeshea.
 
That's too much, mi hata milioni 2 naona ni nyingi mnoooo...
 
KikulachoChako

Sidhani mkuu inategemea na malezi aliyokulia mwanaume unaweza ukatoa hata shilingi elfu kumi mahari. Lakini kama malezi uliyokulia kimtazamo juu ya wanawake bado utaona kuwa ulimnunua mkeo kwa elfu kumi na unaweza kuitumia kama fimbo ya kumchapia. Watu tulitoa ng'ombe sitini na bado wake zetu tunawaona kama delicate matter.
 
Last edited by a moderator:
Labda huo ndio utamaduni wa kabila lao, labda wasingetaja pesa wangetaja kama ng'ombe etc bei ingekuja kufikia hiyo. hapo labda wamewapunguzia na mihangaiko ya kutafuta mifugo kununua, kusafirisha.

Wengine utoa za watoto wa kike walizopokea mzungko unakuwa huo.Ila duh namuonea huruma bi harusi as wengi wanachangia mahari hiyo, duh atahudumiaje kama punda incase ni wapenda rudishiwa walichotoa.
 
Kuna maeneo hapa nchini mtu anatozwa mahari n'gombe 20 au zaidi na mbuzi juu,unashangaa ml 5?Lakini tamaduni za namna hii ni za kishenzi,pili ni udhalilishaji ni sawa na kumuuza mtu.Ndo maana ukatili wa kijinsia hautakoma.Lakini upo uwezekano wa kumchukua hata bure ukitaka,unless hakupendi
 
Hata hivyo si lazima sana uoe huyo,tafuta sehemu nyingine wapo wengi tena wa category unayotaka,tuachane na mila fake kama hizi hazina tija
 
Tembo shit! 5M is much in every walk of life!

Kama ni kurudisha gharama za kusomesha hata mume alisomeshwa,mbona wazazi wake hawadai?

Mahari is supposed to be zawadi ya muoaji kwa familia ya muolewaji. Sasa zawadi gani mnachanga ukoo mzima? Huyo mwanamke kama hawezi kuwakaripia wazee wake kua mahari hiyo ni kubwa,na akae nao!
 
5 million kwa mahari tu??
Na hizo haki sawa wanawake wanazolilia hawazipati miaka 1000!!!
 
MBONA KITU YA KAWAIDA MKUU HIYO
Hapo bado gharama za Kikao na michango hiyo harusi kuvuka 20m itakuwa si ajabu
acha mtu abebe kifaa chake na ndani ya miezi 6 ndoa kalasi (quishney)
 
5 million kwa mahari tu??
Na hizo haki sawa wanawake wanazolilia hawazipati miaka 1000!!!
Mtumishi wewe ungenitolea mi sh ngapi lol. Anyway 5m ni kubwa kama jamaa hana uwezo. Kwa wengine hiyo anaimudu. Mimi binafsi sipendi kunyanyasika, mahari ya hivyo sitaki
 
Milioni 5?Duuuuh!naona kama kukomoana jamani!Yani zote hizo ni mahari au mtaji wa biashara?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Khaa!! Huwezi kujua labda hiyo 5m ni malipo ya kufua, usafi wa nyumba, kulima, kumzalia watoto 5 kwa miaka 5 nk. Hivyo ni bora ungetuwekea mkataba wao wa ndoa kwanza ndiyo uanze kulialia -😀
 
Back
Top Bottom