Mahari shilingi milioni 5?

Mahari shilingi milioni 5?

Mahari haiwezi kuwa kipimo cha thamani ya mwanamke bali wazazi na walezi watakuwa na maana kama watamlea mtoto wao katika misingi ya maadili mema ili aweze kudumu kwenye ndoa..na sio kutanguliza mahari kubwa na kumfanya binti yao aonekane kama ng'ombe aliyetunzwa ili apelekwe mnadani....
 
Kwako mahari halali iwe pesa ngapi labda?
Na kwa kigezo kipi?
 
Wanawake wanaopigania usawa wa jinsia wangeanza kupiga vita hili suala la mahari. Dhana ya kwamba mwanamke ananunuliwa inaleta madhara katika ndoa/uhusiano. Najua kuna pengo kubwa kati ya vijana wa sasa na wazazi wanaotaka kudumisha mila. Kwa wengine si suala la mila ila uchumi. Kazi tunayo!
 
Ukatili dhidi ya wanawake hautakoma maana mtu kila akifikiria mahari aliyolipa ndio anazidi kuongeza kichapo kitakatifu........

Kujazilizia hapo kaka,, pia hii nadhani hupigia chapuo vitendo vya uhuni kati ya waoaji na waolewaji..
Maisha yetu watanzania tunajua, huo ujasiri wa kutamka tarakimu hiyo mtu anautoa wapi.?
Nikiambiwa hii ni biashara sitashangaa,, lakini kama ni kuhusu ndoa moja kwa moja huu ni utumwa na mtumwa yupo sokoni..
OVER.
 
Mahari haiwezi kuwa kipimo cha thamani ya mwanamke bali wazazi na walezi watakuwa na maana kama watamlea mtoto wao katika misingi ya maadili mema ili aweze kudumu kwenye ndoa..na sio kutanguliza mahari kubwa ili hali binti yao ana matabia ya ajabu...

Matabia ya ajabu ndio yamemvutia muoaji hadi kukubali kulipa hiyo mahari kubwa.
Sio kashaoa kwa uchungu wa mahari yake ajidai eti mitabia ya ajabu.
 
Wanawake wanaopigania usawa wa jinsia wangeanza kupiga vita hili suala la mahari. Dhana ya kwamba mwanamke ananunuliwa inaleta madhara katika ndoa/uhusiano. Najua kuna pengo kubwa kati ya vijana wa sasa na wazazi wanaotaka kudumisha mila. Kwa wengine si suala la mila ila uchumi. Kazi tunayo!

Wanaume mnataka kuuza nafasi yenu.
Bora kusiwe na mahari ili iwe KUOANA.
 
Hiyo Milion 5 Labda Kama Naoa Na Mama Mkwe!!! hapo si napandisha msingi kabisa....
 
Pesa ya kufanyia party ya sendoff mkienda mtakunywa pombe na kula kwa pesa yenu. Wengi wanatumia hi hivyo kusaidia kama wanachangisha basi wanaongezea na sherehe inafanyika... Uamuzi tu.

Utamaduni hautakufa nchini, ila wanaooana ndio wanaoweza kushawishu wazazi na inatokea mtu anapunguziwa akitaka tena sana tu.
 
Hiyo Milion 5 Labda Kama Naoa Na Mama Mkwe!!! hapo si napandisha msingi kabisa....

Du hii nayo kari 😳😳😁😁😃😃😃
Nina dogo mjeshi alikwenda kuulizia Mahari wakamwambia milioni 2.5. Yeye akasema ana laki sita tu, hakuna cha nyongeza wala nini. Wakasema haiwezekani, akamwambia mke wake mtarajiwa awambie wazee wapunguze, bi dada akajibu yeye anasikiliza wazee wake. Dogo kauchuna mwezi wa kwanza, wa pili, tatu eh jamaa wakaanza kupiga simu oh ongeza kidogo. Jamaa a kawa na msimamo mwisho wanakubali hiyo laki sita.
 
Wanaume mnataka kuuza nafasi yenu.
Bora kusiwe na mahari ili iwe KUOANA.

Kulipa mahari ni sehemu ya mfumo dume mnaopinga kwa nguvu zote. Naona ni contradiction kupinga mfumo dume lakini kutaka mahari iendelee kuwepo! Terminology ya kuoa/kuolewa/kuoana inaweza kupotea pia. Wengine wanasema wanafunga ndoa!
 
Mtumishi wewe ungenitolea mi sh ngapi lol. Anyway 5m ni kubwa kama jamaa hana uwezo. Kwa wengine hiyo anaimudu. Mimi binafsi sipendi kunyanyasika, mahari ya hivyo sitaki


Mtumishi wewe ningekutolea vyote nilivyo navyo..lol
Lakini kusema kweli kwa watz wengi 5M ni kiasi kikubwa mtumishi. Hapo bado hujamvalisha pete, sherehe za harusi hujagharamia...
Ona sasa mtu anachangisha ndugu ili alipe mahari, kuna uwezekano wakaanza maisha na madeni...
 
Yaani wajanja wengi siku hizi ndio maana wanawapa mimba mabinti halafu ndio wanaenda kubargain mahari.Pindi binti anapokuwa na mimba ukienda kwa wazazi wake mahari muoaji ndiyo unajichagulia unaweza kutoa shilingi ngapi!!!?
 
Uyo mzee wana muuza mtoto wao na si vingne mil 5.....aaaaah ila km pakeee ipo n amount ndogo xana
 
Hapo ni sawa na kununua papuchi kwa mil 5,sijui hiyo papuchi ina ubora gani
 
Mahari ilipaswa iwe jambo la kudumisha mahusiano baina ya koo zinazoungana ila kwa hali ya kufikia kuchangishana naona kuna hatari ya kuharibu mahusiano.
Sitashaangaa baada ya hiyo ndoa mume asitoe msaada wowote ukweni.
 
mbona wazee wa zamani walikuwa wanatoa ng'ombe 60 ...mbuzi 30.....kuku....etc......sasa hivi hizo gharama za ng'ombe na mbuzi zimewekwa kwenye pesa......

na shida nyingine hata ukipewa mahali kidogo....mwisho wa siku utamsema tu......wazazi walimchoka ndiyo maana aliozwa kwa mahali ndogo.....
 
Yaani nalipa milioni 5 mahari! Wajiandae na kesi za kuchakazwa kinyeo kwa mwanao...
 
Back
Top Bottom