Kimsingi masharti sio magumu sema hali ya kiuchumi imekuwa ngumu pia mabadiliko ya mila na desturi kutokana na maendeleo tunajikuta tunaenda kuoa kwenye community nyingine mfano mpare anaoa muha n.k. hivyo ukikutana na hayo mambo miguu inakuingia tumboni. Zamani iliwezekana watu walioa kwenye the same community hivyo hata kabla ya kuoa mtu anajiandaa na isitoshe jukumu la kulipa mahari lilikuwa ni la baba mzazi hivyo kama baba wengi wao walikuiwa wanajiandaa kwa kufuga mifugo miwili mitatu mpaka vijana wake watakapofika muda wa kuoa linatoka dume moja linakwenda kumaliza issue.
Tatizo madingi wetu wametutosa siku hizi mahari unalipa wewe mwenyewe wakati yeye anaoa alilipiwa na mzee wake, pia kama hela ya sherehe asilimia kubwa utajitutumua mwenyewe though kwenye kikao cha kwanza yeye ndio anajifanya familia tuna kiwango hiki (uzoefu kwa wengi kimjinimjini except wachache)
Ni Kweli Kabisaa Bro Sahivi Yani Anamikakati ya kutoa anachoweza wakigoma anawaachia binti yao.
Binafsi Siwezi Taka Mume Wangu Mtarajiwa Akapigwa Mzinga Mkubwa Kiasi Hicho
Walla hata hana huo uwezo wa kuilipa yote,Na Kukopa Hawezi,Ikishindikana Anaghairi Kuoa Unyakyusani
Mie Nalalama Kwa Sababu Uwezo Wetu Ni Mdogo,
Hebu Chukulia ni wewe umetolewa posa afu mchumba anashindwa kulipa mahari kwa kuwa iko juu na wazew wamegoma mazungumzo,
Kama Unauwezo hata wa kupeleka mahari ya nyumba it's well with you,ila mimi naongelea kijana ambaye hana wazazi wakumsupport anategemea nguvu zake mwenyewe.
Wapi huko nije kujitwalia mmojayaani ni kama milioni 4 mahari gani hio.! Nashukuru kwetu mahari haizidi laki 6 huwa laki 2, 3 ikienda sana 4.
Tena wao wakati unaenda kutoa mahari kwao ni kama umemaliza zoezi na mke unaweza kubeba kabisa na kwenda kumalizia kwa ustadhi au kanisani au bomani kuirasimisha hata kama bila shereheYani Wachaga hakuna gharama za kutiliana hasara,
Vitu ni affordable na havimuumizi muoaji