Mahari kwa wanyakyusa

Mahari kwa wanyakyusa

Bei ya ngombe dume na mkaja wa mama vinapangwa na kwa kuangalia uwezo wa muoaji.
Binti ndio anajua uwezo wa mwanaume hivyo wanaweza kutaja hata 50,000-milioni kwa bei ya ng'ombe dume. Na mkaja inaweza kua 20,000-500,000 na hata zaidi.
Heri usukumani kuna mahari ya ng'ombe mnyama na ng'ombe fedha (ambayo kidogo ina unafuu kuliko kuambiwa kuleta ng'ombe original)
 
Wanyakusya hawafai wana masharti magumu ya kuoa we acha kabisa halafu mabinti wenyewe wabishi na jeuri ukishawaweka ndani! Mke wangu ni mnyakyusa nilipoenda kuoa cha moto nilikiona. Kuna kitu wanaita mkaja wa mama, sijui kikingi, hela ya shangazi, vitenge, mablanketi, mashuka, ng'ombe 3 wawlli majike na dume moja, ukikaribishwa unalipia pale ulipokaa, wakileta msosi usidhani ni bure baada ya kula utaulipia. Mbona niliomba po at once nilijikuta km 2m zinakatika!
Kimsingi masharti sio magumu sema hali ya kiuchumi imekuwa ngumu pia mabadiliko ya mila na desturi kutokana na maendeleo tunajikuta tunaenda kuoa kwenye community nyingine mfano mpare anaoa muha n.k. hivyo ukikutana na hayo mambo miguu inakuingia tumboni. Zamani iliwezekana watu walioa kwenye the same community hivyo hata kabla ya kuoa mtu anajiandaa na isitoshe jukumu la kulipa mahari lilikuwa ni la baba mzazi hivyo kama baba wengi wao walikuiwa wanajiandaa kwa kufuga mifugo miwili mitatu mpaka vijana wake watakapofika muda wa kuoa linatoka dume moja linakwenda kumaliza issue.

Tatizo madingi wetu wametutosa siku hizi mahari unalipa wewe mwenyewe wakati yeye anaoa alilipiwa na mzee wake, pia kama hela ya sherehe asilimia kubwa utajitutumua mwenyewe though kwenye kikao cha kwanza yeye ndio anajifanya familia tuna kiwango hiki (uzoefu kwa wengi kimjinimjini except wachache)
 
Pamoja na habari hii mimi wala cjakata tamaa nipo naendelea na mnyaki wangu. Soon nitaenda kutoa mahali.
 
Habari Zenu Ndugu Zangu Wana MMU.Nilikuwa Sijawahi kuhudhuria tendo la kutoa posa kwa Wanyakyusa ila leo nimekuwa mmoja wapo wa kupeleka barua ya posa.
Swala la kupanga mahari limentoa macho kidogo huenda ni mimi kutokuwa na uzoefu.Kama ilivyo ada tumewasilisha barua vyema wakaipokea vizuri sana na baadaye tukapewa majibu kamaa ifuatavyo.
Mshenga upande wa binti kaanza kwa kusema sisi wanyakyusa huwa tunazo mahari mara mbili.(1).Mahari Ya Unyago ambayo ni non negotiable,ni kama ifuatavyo.
1.Ng'ombe Dume ambaye dhamani yake ni Tshs.500,000.Na hapa lazima utoe hela ng'ombe haitajiki.
2.Tshs.400,000 Za Mama Mzazi.
3.Blanketi 2 za wazazi.
4.Vitenge kulingana na idadi ya mashangazi.

(2)...Mahari Ya Pili ni negotiable:

1.Ng'ombe Wanne Majike.
2.Vitenge Vya Mashangazi.

Jamani nia yangu ya kuleta hili swala hapa ni kupata mtazamo wenu.
Je,Kwa Kijana wa kiume ambaye ametoka kwenye familia hohehahe ataweza kweli??

KARIBUNI MNIPE MTAZAMO WENU.

Na msingeenda na barua,mngepigwa faini!lakini huwa wanaangalia na waoaji wameendaje pale.kama mmeenda kitajiri basi mtalingana na mahari mtakayoambiwa.

Karibuni unyakyusani


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Na msingeenda na barua,mngepigwa faini!lakini huwa wanaangalia na waoaji wameendaje pale.kama mmeenda kitajiri basi mtalingana na mahari mtakayoambiwa.

Karibuni unyakyusani


Sent from my iPhone using JamiiForums

Barua ilibidi tukae sehemu tuidraft faster,
Ila bro kama kaisiwa nguvu vile maana tathmini ya haraka ni like 3.2M
Kasema hapeleki yote wakinzingua anamtosa binti wamtafutie anaelingana na kiwango hicho cha mahari.
 
Kimsingi masharti sio magumu sema hali ya kiuchumi imekuwa ngumu pia mabadiliko ya mila na desturi kutokana na maendeleo tunajikuta tunaenda kuoa kwenye community nyingine mfano mpare anaoa muha n.k. hivyo ukikutana na hayo mambo miguu inakuingia tumboni. Zamani iliwezekana watu walioa kwenye the same community hivyo hata kabla ya kuoa mtu anajiandaa na isitoshe jukumu la kulipa mahari lilikuwa ni la baba mzazi hivyo kama baba wengi wao walikuiwa wanajiandaa kwa kufuga mifugo miwili mitatu mpaka vijana wake watakapofika muda wa kuoa linatoka dume moja linakwenda kumaliza issue.

Tatizo madingi wetu wametutosa siku hizi mahari unalipa wewe mwenyewe wakati yeye anaoa alilipiwa na mzee wake, pia kama hela ya sherehe asilimia kubwa utajitutumua mwenyewe though kwenye kikao cha kwanza yeye ndio anajifanya familia tuna kiwango hiki (uzoefu kwa wengi kimjinimjini except wachache)

Daah...Aiseee Mie Namwona Bro Akimtolea Nje Binti Wa Watu,
Hivi Hivi
 
Heri usukumani kuna mahari ya ng'ombe mnyama na ng'ombe fedha (ambayo kidogo ina unafuu kuliko kuambiwa kuleta ng'ombe original)

Ni Kweli Kabisa,Afu Mshenga Upande Wa binti anaenda mbele zaidi na kusema "Not Negotiable"Hapo Aliuwa Bendi Kabisaa
 
Kama ni bidhaa vile nikinunua basi hairudi ntaoa kwa hyo hela wanayo itaka

Halafu Unashangaa After Few Months Ndoa Inavunjikaa
Hapo Lazima kitanzi kukuhusu
 
Mahali ndogo ivo unalalama,,,, huku watu tunaolewa kwa gharama fuso akiwa tajiri semi au bus

Mie Nalalama Kwa Sababu Uwezo Wetu Ni Mdogo,
Hebu Chukulia ni wewe umetolewa posa afu mchumba anashindwa kulipa mahari kwa kuwa iko juu na wazew wamegoma mazungumzo,
Kama Unauwezo hata wa kupeleka mahari ya nyumba it's well with you,ila mimi naongelea kijana ambaye hana wazazi wakumsupport anategemea nguvu zake mwenyewe.
 
Mahali inaombwa au kutolewa kutokana uwezo wa familia ya kijana.

Ni jukumu la binti kuwaeleza wazazi wake uwezo wa mkwe wao mtarajiwa ili wakati wa kupanga mahari wajue mkwe wao ni mtu wa namna gani.

Sidhani kama kuna familia inaweza kumzuia binti yao kuolewa kwa kutoza mahari kubwa!

Ni Kweli Kabisaa Bro Sahivi Yani Anamikakati ya kutoa anachoweza wakigoma anawaachia binti yao.
Binafsi Siwezi Taka Mume Wangu Mtarajiwa Akapigwa Mzinga Mkubwa Kiasi Hicho
 
Bei ya ngombe dume na mkaja wa mama vinapangwa na kwa kuangalia uwezo wa muoaji.
Binti ndio anajua uwezo wa mwanaume hivyo wanaweza kutaja hata 50,000-milioni kwa bei ya ng'ombe dume. Na mkaja inaweza kua 20,000-500,000 na hata zaidi.

Sasa Huko Si Ni Kurudishana Nyuma Kimaendeleo??
Au Ndo Mambo Ya Mitaji
 
Wewe na huyo mshenga wenu wote mna matatizo. Mnatakiwa muweke uwezo wenu wazi hamna mtu anatoka bila mke. Halafu msiogope mahali hailipwi yote hata siku moja. Mkiwa wajuzi laki tano itawatosha sana kulipia kila kitu.
 
Back
Top Bottom