Maharamia wa Kisomali na majumba mapya Mbezi

.

Tanzania Tanga kambi ya wakimbizi Chogo wilaya ya Handeni ina wakimbizi wengi wa kisomali cha kushangaza wote wamepewa uraia kwa mkupuo.Mlipuko wa mabomu nchi Kenya [stand ya bus Nairobi] ulifanywa na raia wa kisomali aliyepewa passport ya Tanzania kutokea kambi ya wakimbizi Chogo !!!!!!!!!!!!.


Mkuu Ngongo kwenye suala la chogo serikali haikukurupuka....hawa wasomali Wadigo ...mababu zao yapata miaka 100 iliyopita walitoka eneo hilo kwenye normal african migration ya wakati ule[trek]..na wakati huo somalia ikiwa na neema ..wakaenda Somalia kuweka makazi kwa sababu moja au nyingine.....na walikuwa wakiongea hicho kidigo[au kisambaa] hadi huko uhamishoni na kiswahili pia.....mwaka 1992 baada ya machafuko kufuatia kukimbia kwa Siad Barre.....walikaa kidogo yalipowazidi ..na kwa kuwa wanakumbuka asili yao hadi kijiji ambacho koo yao ilitoka ..wakajikusanya wakiwa kama 3,000 na kuanza safari ya kurudi kwenye kijiji chao cha asili huko Tanga...walipofika ..na kwa kuwa miaka ilishaenda ..ikawabidi wafikie kwenye ukimbizi....uchunguzi na utambuzi ukafanyika kwa kushirikisha wazee wa eneo hilo ..na ukizingatia bado kumbukumbu za koo yao zipo na ndugu zao wengine waliobakia huko zipo...basi ...ikawa kama vile mwanampotevu kurudi nyumbani...wakatafutiwa eneo la wazi [chogo] na kuanzisha upya kijiji...kwa kifupi wale jamaa ni ndugu zetu..........

NI mfano kama huu ungeweza kutokea iwapo Tanzania ingekuwa kwenye vita sugu...na somalia ina amani...ni wazi kuwa watanznaia wenye koo zao kule ...wenye asili ya kisomali ...wangerejea kule na wangepokelewa......kwani wengi wao baba zao tangu wamehamia hawana miaka 100 ..you can trace easily ..unlike migration za watu kama Wangoni-Nguni speaking people [south africa]miaka 500 iliyopita...,wasukuma et al-ABantu speaking people [congo] miaka 500 iliyopita...Wachagga[wasambaa,meru..akamba,Kikuyu],Masaai,Iraq etc...migrating from Ethiopia,sudan etc...coming down via the great rift valley...and mountanous region of mout kenya,meru and mount Kilimanjaro..etc
 
Wacheni kuja na hoja za kijinga... mlianza na waarab mkaja wahindi sasa mmewavamia wasomali wasio na nchi yenye amani? fanyeni kazi uvivu muache uvivu... pesa zenu kwani hizo? zenu mmeshindwa kuwapokonya mafisadi mwazionea gere za wenzenu wacheni kumwaga mapovu...

Kweli ni pesa zao (lakini za uharamia yaani chafu) nchi na aridhi ni yetu. Paradise iliyotiwa kiberiti Bagamoyo nakulipwa insurance chap chap muulize JK anajua na ni kwao na ni si ajabu ni mbia wao
 
Heshima kwako Phillemon Mikael.

Mkuu nashukuru kwa mchango wako maridhawa.

Naomba kuweka kumbukumbu sawasawa natambua wapo baadhi ya Wazigua [si wadigo] waliokimbilia Somalia miaka mia moja iliyopita.Bahati nzuri nimekaa,nimezungumza nao kwa kirefu sana.Nilijaribu kufanya utafiti sababu ziliwafanya wahifadhi Lugha ya kizigua na Kiswahili kwa muda wote walikuwa Somalia [miongo kumi].Sababu kubwa ni ubaguzi waliokumbana nao huko Somalia hawakuruhusiwa kuona na wasomali wa asili.Nywele na pua zao zilikuwa kero kubwa.walionekana watu wa tabaka la chini kabisa.Hawakupewa fursa sawa na wasomali.

Nirejee kwenye mada husika nimesema natambua wako wazigua waSomali,Lugha hata maumbile yao hawana tofauti na wazigua wa Tanga.Mkuu kwenye msafara wa mamba kenge wapo.Wazigua wa asili ya Tanzania walirejea na waSomali wa asili ya Somalia kabisa hawa ndiyo nilikuwa nawazungumzia hawajui kiswahili wala kizigua maumbile yao ni kama waSomali unaowajua.Kambi ya wakimbizi Chogo inajua hilo waliwagwa kabisa kwasababu moja kubwa waSomali kwa maana ya waSomali haswa bado walikuwa na ndoto za kurejea Somalia hali ya amani na utulivu ikirejea ajabu idara ya wakimbizi kwa msukumo wa kigogo wa kisomali hila ilifanyika wakimbizi wote wakapewa uraia wa Tanzania.Asilimia kubwa ya waSomali wa asili ya Somalia kabisa wako mitaani wanajishuhulisha na uratibu wa kuwaingiza raia wa Somalia walioko Kenya na Somalia.

Mkuu ninaposema serekali ya Tanzania lazima ikae macho sitanii,wengi wamejiingiza vijiji vingine kuanzia Holili,Himo,Same,Hedaru,Makanya,Mombo,Korogwe,Segera,Kabuku,Mbwewe hadi Chalinze kazi yao kubwa nikuratibu wahamiaji haramu from Somalia na Kenya.Ukisikia wamekamatwa ujue kuna msomali mwenzao karushwa hela kaamua kurongosha Uhamiaji.
 
jamani hawa wanaafali walituajiri pale bagamoyo ndugu, na c kama kuchkuch,japokuwa hawapo km watz on ma side siwachukii saaaana kama wahindi
 
Mji wa Mombasa nchi Kenya vijana raia wa kenya wenye asili ya kisomali wengi wamejiunga na jeshi la wapinzani wa serekali inayotambuliwa na AU kwa ujira wa chini ya dola u$ 50.Wengi wamekufa vitani kwasababu ya mafunzo duni na wakati mwingine maradhi.Vijana wengi hawana kazi wakidanganywa hata kwa maslahi duni ni rahisi kuhadaika.

Tanzania Tanga kambi ya wakimbizi Chogo wilaya ya Handeni ina wakimbizi wengi wa kisomali cha kushangaza wote wamepewa uraia kwa mkupuo.Mlipuko wa mabomu nchi Kenya [stand ya bus Nairobi] ulifanywa na raia wa kisomali aliyepewa passport ya Tanzania kutokea kambi ya wakimbizi Chogo !!!!!!!!!!!!.

Ninaposema Raia wa Tanzania wenye asili ya kisomali ni hatari sibahatishi hata kidogo.Mikakati ya kuwasafirisha,kuwahifadhi na kuwatafutia maeneo ya uwekezaji inafanywa na Wasomali wazawa wa Tanzania.
.


Watanzania ni wabaguzi sana, ukiangalia karibu sehemu nyingi duniani kuna watanzania wanaoishi na kufanya kazi huko. Wana jumuia zao pia, wana position nzuri tu. Kwa mfano Botswana. Hii inatokana na nchi waliotoka na nchi wanayoenda na mfumo walioukuta huko. Kwa mfano. Wasomali wachakalikaji, wakija tz huwezi kuwabadilisha wawe walalaji kama tulivyo sisi, wataendelea la spirit yao hiyo.
Ingekuwa ubaguzi tunoufanya wamarekani wangeufanya Obama asingekuwa presdaa kule usa leo hii.
Nchi yoyote inaendeshwa ki sheria, hata mnigeria akiongoza tz hatoweza kutoa uraia wa mnigeria mwenzake kinyume na taratibu za nchi. Kiubwa watz hatuna uzalendo.
 
Kweli ni pesa zao (lakini za uharamia yaani chafu) nchi na aridhi ni yetu. Paradise iliyotiwa kiberiti Bagamoyo nakulipwa insurance chap chap muulize JK anajua na ni kwao na ni si ajabu ni mbia wao
Bug Up Mkuu, kuna watu hawajui kwamba pesa si kila kitu na kuwa nchi yetu watu wa kuilinda ni sisi wenyewe.
Niliacha nisimjibu huyu member Duduwasha, ili apate kujielimisha na hoja.
Wacheni kuja na hoja za kijinga... mlianza na waarab mkaja wahindi sasa mmewavamia wasomali wasio na nchi yenye amani? fanyeni kazi uvivu muache uvivu... pesa zenu kwani hizo? zenu mmeshindwa kuwapokonya mafisadi mwazionea gere za wenzenu wacheni kumwaga mapovu...
 
Watanzania ni wabaguzi sana, ukiangalia karibu sehemu nyingi duniani kuna watanzania wanaoishi na kufanya kazi huko. Wana jumuia zao pia, wana position nzuri tu. Kwa mfano Botswana. Hii inatokana na nchi waliotoka na nchi wanayoenda na mfumo walioukuta huko. Kwa mfano. Wasomali wachakalikaji, wakija tz huwezi kuwabadilisha wawe walalaji kama tulivyo sisi, wataendelea la spirit yao hiyo.
Ingekuwa ubaguzi tunoufanya wamarekani wangeufanya Obama asingekuwa presdaa kule usa leo hii.
Nchi yoyote inaendeshwa ki sheria, hata mnigeria akiongoza tz hatoweza kutoa uraia wa mnigeria mwenzake kinyume na taratibu za nchi. Kiubwa watz hatuna uzalendo.

Heshima kwako Mzizi,

Mkuu sipingi waSomali kuwa jumuiya zao tatizo ni mission za hizo jumuiya.Zinafanyakazi haramu ndani ya ardhi ya JMT.Mkuu taratibu za kupata uraia wa Tanzania ni tofauti kabisa na USA.Tanzania waziri wa mambo ya ndani kapewa mamlaka makubwa ya kutoa uraia ndani ya katiba yetu mbovu.Ebu fuatilia sakata la Hussein Bashe utaelewa jinsi ilivyo rahisi haramia kupewa uraia wa Tanzania.
 
ni kweli mkuu wale wa mafia walikamatwa kibahati tu....ila nenda isilii (east leigh) hapo nairobi ndo utajua nguvu ya hiyo ransom money..ila jamaa wanachokifanya watakuja kudominate east africa yote kwa huo ubabe wao tuweni makini.

Si wasomali wote ni wabaya, hao jamaa wanamatatizo makubwa yaliyosababishwa na wana siasa wao. Hawakuwa hivyo hapo awali! Labda tatizo lao kuwa ni wateka meli, ila sisi tuna wabaya zaidi hapa kwetu, hawa ni wateka maisha ya watu masikini, ambao ni mafisadi wa mali za umma! Waongo, wanafiki na wanaotumia ujinga wa wananchi kwa maslahi yao binafsi. Hao ndio tatizo, kwani ndio wanaowabeba hata hao wasomali tunaowaita tatizo!
Kuhusu hao waliokamatwa mafia hawakuwa maharamia, ila ni kukurupuka tu kwa viongozi wetu wa serikali! Maharamia hawawezi kuwa mia moja, wanawake na watoto, niliwashuhudia hao jamaa, mwisho wake wakawa gharama kwa serikali. Kwani jamaa walikuwa na documents zao zote za ukimbizi, na walikuwa wanaelekea msumbiji kwenye kambi yao ya UN huko
 
Watanzania ni wabaguzi sana, ukiangalia karibu sehemu nyingi duniani kuna watanzania wanaoishi na kufanya kazi huko. Wana jumuia zao pia, wana position nzuri tu. Kwa mfano Botswana. Hii inatokana na nchi waliotoka na nchi wanayoenda na mfumo walioukuta huko. Kwa mfano. Wasomali wachakalikaji, wakija tz huwezi kuwabadilisha wawe walalaji kama tulivyo sisi, wataendelea la spirit yao hiyo.
Ingekuwa ubaguzi tunoufanya wamarekani wangeufanya Obama asingekuwa presdaa kule usa leo hii.
Nchi yoyote inaendeshwa ki sheria, hata mnigeria akiongoza tz hatoweza kutoa uraia wa mnigeria mwenzake kinyume na taratibu za nchi. Kiubwa watz hatuna uzalendo.

Mkuu unaishi dunia ipi? Suala la Obama kuwa au kutokuwa rais wa marekani halihusiani na topic inayozungumzwa hapa, mind you Marekani haina mwenyewe. Kuhusu watanzania kuwa na nafasi nyeti hasa Botswana, nikusaidie tu, Watswana ni wavivu sana kutokana na utajiri walionao, hivyo kama wewe ni msomi na nchi inahitaji wataalamu, ni rahisi sana kupata kazi as well as nafasi nyeti!
Changanya na zako utaelewa ninamaanisha nini?
 
Si wasomali wote ni wabaya, hao jamaa wanamatatizo makubwa yaliyosababishwa na wana siasa wao. Hawakuwa hivyo hapo awali! Labda tatizo lao kuwa ni wateka meli, ila sisi tuna wabaya zaidi hapa kwetu, hawa ni wateka maisha ya watu masikini, ambao ni mafisadi wa mali za umma! Waongo, wanafiki na wanaotumia ujinga wa wananchi kwa maslahi yao binafsi. Hao ndio tatizo, kwani ndio wanaowabeba hata hao wasomali tunaowaita tatizo!
Kuhusu hao waliokamatwa mafia hawakuwa maharamia, ila ni kukurupuka tu kwa viongozi wetu wa serikali! Maharamia hawawezi kuwa mia moja, wanawake na watoto, niliwashuhudia hao jamaa, mwisho wake wakawa gharama kwa serikali. Kwani jamaa walikuwa na documents zao zote za ukimbizi, na walikuwa wanaelekea msumbiji kwenye kambi yao ya UN huko

Mkuu pamoja na huruma yako kwa wasomali, allegiance yako lazima iwe kwa utaifa wako first and foremost.
Hata wakipata shida kwao tusiyelete matatizo yao huku kwetu-na hilo ndo suala lenyewe.
Leo mabomu yanalipuka Nairobi kutokana na kiungiliwa na makundi hayo ya kigaidi.
Kuna mwanasiasa aliwahi kusema , weka wasomali wawili kisiwani, na wataishia kupigana for the slimliest reason.
These people are as wild as they can possibly get.
Hawatawaliki, period.
Not that I hate them, lakini mifano ya kuunguzwa Paradise na kulipwa chap chap is a calling card to speak of.
 
Jamani tuache kukurupuka Paradise group wapo zaidi ya miaka 30 na Tansoma pia yakwao,lile jumba refu Mbezi ni la raia wa Djibouti na pia kuna wawekezaji wa Kisomali raia wa Ulaya na Marekani wanaowekeza nchini kwakuwa hawana nchi ya kuwekeza kwao kwa sababu ya vita.Hawa ni wakuwasifu kwa kuchagua nchi yetu kuwekeza.Ni kweli wameona kuna faida katika kujenga majumba ya kuishi.

hela za hawa Maharamia ziko Dubai,na sasa zinakuja Bongo!
Organised crime,UWT hawana uwezo,wao ni kushughulikia wapinzani tu
 
Watanzania ni wabaguzi sana, ukiangalia karibu sehemu nyingi duniani kuna watanzania wanaoishi na kufanya kazi huko. Wana jumuia zao pia, wana position nzuri tu. Kwa mfano Botswana. Hii inatokana na nchi waliotoka na nchi wanayoenda na mfumo walioukuta huko. Kwa mfano. Wasomali wachakalikaji, wakija tz huwezi kuwabadilisha wawe walalaji kama tulivyo sisi, wataendelea la spirit yao hiyo.
Ingekuwa ubaguzi tunoufanya wamarekani wangeufanya Obama asingekuwa presdaa kule usa leo hii.
Nchi yoyote inaendeshwa ki sheria, hata mnigeria akiongoza tz hatoweza kutoa uraia wa mnigeria mwenzake kinyume na taratibu za nchi. Kiubwa watz hatuna uzalendo.

hatutaki wanigeria au wasomali,ni nuisance
 
Watanzania ni wabaguzi sana, ukiangalia karibu sehemu nyingi duniani kuna watanzania wanaoishi na kufanya kazi huko. Wana jumuia zao pia, wana position nzuri tu. Kwa mfano Botswana. Hii inatokana na nchi waliotoka na nchi wanayoenda na mfumo walioukuta huko. Kwa mfano. Wasomali wachakalikaji, wakija tz huwezi kuwabadilisha wawe walalaji kama tulivyo sisi, wataendelea la spirit yao hiyo.
Ingekuwa ubaguzi tunoufanya wamarekani wangeufanya Obama asingekuwa presdaa kule usa leo hii.
Nchi yoyote inaendeshwa ki sheria, hata mnigeria akiongoza tz hatoweza kutoa uraia wa mnigeria mwenzake kinyume na taratibu za nchi. Kiubwa watz hatuna uzalendo.

Kaka watanzania walio Botswana ,Angola ,South Africa,Zimbabwe,Namibia,Mocambique etc wana haki kabisa kupata wanayoyapata na kuheshimiwa....angalia historia ya Taifa letu ..kote huko ni nchi ambazo Mwalimu Nyerere alituma vikosi vyetu kwa namna moja au nyingine ..kupigania uhuru..yaani kote huko kuna damu za watanzania zilimwagika hadi wao wakawa huru,,,,....tena Watanzania tumezubaa...lakini tunastahili kupata fursa nyingi za kiuchumi kuliko raia wa nchi ambazo sisi askari wetu walipokuwa wakipigania uhuru huko .....nchi zao zilikuwa zinashirikiana na mabeberu....
Watanzania tunastahili kuringa ...we have the special place in Africa..the mistake Nyerere need or even because alikuwa mjamaa sana is ...alitakiwa kila nchi aliyopeleka vikosi kupigania uhuru...apeleke na watanzania kunufaika na fursa za kibiashara kama wafanyavyo wamarekani..leo hii tungekuwa mbali.....
 
Heshima kwako Duduwasha,

Mkuu ni vyema kama hujui jambo kaa kimya ujuzwe.
Kusamabaratika kwa serekali ya Somalia mwanzoni lilionekana kama tatizo la Afrika au pengine tatizo la kikanda zaidi.Mashirika yote ya kijasusi ya nchi za magharibi yanatambua yalikosea sana Somalia sasa ni tatizo la kudunia linahitaji kushughulikiwa kimataifa tena kwa uangalifu wa hali ya juu sana.

Mapato yatokanayo na utekaji wa meli yamemiminika eneo lote la Afrika mashariki,Kenya wamekuwa waanga wa mwanzo pengine sababu za kijiografia zilisaidia zaidi.Wasomali wamenunua maeneo sehemu mbali mbali kwa bei kubwa kwaajili ya ujenzi wa mahotels na majumba ya biashara.Benki kuu ya Kenya imekiri kuingia kwa fedha nyingi sana nje ya mfumo wake rasmi wa fedha.Tanzania nayo haikubaki nyuma miji ya Arusha,Tanga,Dar es Salaam imevamiwa na hizi fedha za uharamia.

Zipo athari kibao ambazo nchi za EA zimeanza kuona moja kubwa nikitisho cha ugaidi kuongezeka matukio ya mlipukowa mabomu nchini Kenya na Uganda ni uthibitisho jinsi haliitakavyozidi kuwa mbaya siku za usoni.Wasomali wamefanikiwa sana kupenyeza wasomali wenzao ndani ya mfumo wa siasa na utawala nchini Kenya ili kulinda maslahi ya wasomali hasa kuwahakikishia usalama wa mali zao walizowekeza nchi humo.Tanzania imeanza kunyemelewa hasa kipindi hiki ambacho ombwe la uongozi/utawala limetamalaki.Kuna mikakati ya maksudi na siri ya kuwasaidia raia Tanzania wenye asili ya kisomali kukamata nafasi za uongozi ndani ya vyombo vya maamuzi.Ni rahisi sana kufanikisha mkakati wa aina hii kwasababu chaguzi zetu zimetawaliwa sana na matumizi makubwa ya fedha[hakuna udhibiti wa matumizi ya fedha]. Bashe Hussein,Aden Rage na A Kinana ni aina ya viongozi wanaowatumikia magaidi ya wa kisomali kwa kuwapatia mikakati mbali mbali eg kujipenyeza ndani ya vyombo vyetu vya ulinzi na usalama [miradi ya kiuchumi] tenda.Tanzania isipokuwa makini hakika uchaguzi wa mwaka 2015 idadi ya wabunge wasomali lazima itaongezeka maradufu kwakuwa tayari maharamia wa kisomali wanazo fedha za kuwafadhili.

Kinana aliwahikushika wadhifa wa spika wa bunge la EAC,anajua nje ndani jumuiya hiyo inavyoendeshwa hivi sasa zipo juhudi na mikakati ya kuiingiza Somalia ndani ya EAC bila kujali sehemu kubwa ya Somalia inashikiliwa na wapinzani wa serekali.Watu wazima hawajawaza wasomali watakavyopata uwanja mpana [eneo la nchi za EAC] wa ugaidi.

WaTanzania wenye asili ya Somalia ni tishio kubwa la usalama wa Tanzania na eneo lote la Afrika.
Wacha Kuishi kwa Tetesi na hofu... Hili ni Tatizo kubwa la Mashabiki wa Yanga, Arsenal na Taifa Stars Game ikianza hadi Inaisha Kujamba jamba tu Mtapatwa na magonjwa ya Moyo na Kuweweseka....
 
[/I said:
Duduwasha;2084618]Wacheni kuja na hoja za kijinga... mlianza na waarab mkaja wahindi sasa mmewavamia wasomali wasio na nchi yenye amani? fanyeni kazi uvivu muache uvivu... pesa zenu kwani hizo? zenu mmeshindwa kuwapokonya mafisadi mwazionea gere za wenzenu wacheni kumwaga mapovu...


Hizi tetesi zipo kwenye circle za watu wa Intelligence...hasa zinatokana na kukamatwa kwa maharamia wa kisomali ...mwanzoni mwa mwaka huu kwenye pwani ya Mtwara baada ya mapigano na JWTZ Navy..na wale waliokamatwa kimya kimya Mafia baada ya kuwa wameishiwa maji na chakula deep sea.....kwenye mahojiano na watu wa TISS na jwtz.....jina la Mohamed N....r ...,lilitajwa .....kama moja ya GOD FATHERS wao hapa....huyu jamaa yupo connected kwenye jeshi ..na huko Tiss...,baada tu ya hizi tetesi kumfikia ....aliamua kubandua bango la TANSOMA kwenye hotel yake ya Gerezani....
..........
..........
Pia watu wanaotuhumiwa kuwa nao tuwe makini sana nao hasa pale tunapowashirikisha kwenye kufanya kazi na serikali...itaonekana kama vile serikali inaunga mkono uharamia...at any given time idara zetu ziwaweke kwenye surveillance na wakipatikana na ushahidi wowote basi wapelekwe mahakamani....

Mkuu ninaposema serekali ya Tanzania lazima ikae macho sitanii,wengi wamejiingiza vijiji vingine kuanzia Holili,Himo,Same,Hedaru,Makanya,Mombo,Korogwe,Segera,Kabuku,Mbwewe hadi Chalinze kazi yao kubwa nikuratibu wahamiaji haramu from Somalia na Kenya.Ukisikia wamekamatwa ujue kuna msomali mwenzao karushwa hela kaamua kurongosha Uhamiaji.


Ninaposema Raia wa Tanzania wenye asili ya kisomali ni hatari sibahatishi hata kidogo.Mikakati ya kuwasafirisha,kuwahifadhi na kuwatafutia maeneo ya uwekezaji inafanywa na Wasomali wazawa wa Tanzania.
.
[/I said:
Duduwasha;2088973]Wacha Kuishi kwa Tetesi na hofu... Hili ni Tatizo kubwa la Mashabiki wa Yanga, Arsenal na Taifa Stars Game ikianza hadi Inaisha Kujamba jamba tu Mtapatwa na magonjwa ya Moyo na Kuweweseka....


Wakuu nilipouliza swali nilitegemea kupata majibu kutokana na tetesi zilizopo mitaani.
Hii ni nchi yetu na si somalia nyingine.
Tofauti kati ya mimi mjinga wa kuuliza swali na yule mpumbavu ni kuwa mimi nilikuwa sifahamu , sasa najua.
On e other hand mpumbavu hajui, hachukui juhudi yoyote kufahamu, na hata akielimishwa hurudi na kuridhika na kutofahamu kwake.
Huyu hatuna cha kumsaidia.
Hata hivyo upande wa pili ni kama mpumbavu huyo anafaidika na tatizo lililopo la uharamia na wasomali.
Nimngemsihi huyu mtu aende kuwasaidia Kampala na Nairobi waliolipata tatizo la ugaidi, katika kujamba.
Tumeonywa tumesikia.
 
Duduwasha weka wazi nafasi yako katika jamii.
Je wewe ni Msomali?
Wa kuhalalishwa(wakuja) au wa kuzaliwa Tanzania?
Ni vyema tukakuelewa kutokana na msimo wako wenye utata.
 
Tamaa ya fedha kwa watendaj wetu ndio itatumaliza,lakini hata leo kuna gazet limeripot kua tanzania kuna raia wengi wa kigen ambao wanaish kinyume na sheria na wanajihusisha na UKAHABA,pamoja na uuzaj wa madawa ya kulevya
 
LOLE GWAKISA & PHILLEMON MICHAEL...!
I GIVE YOU HONOURARY DOCTORATE DEGREE FOR THIS THREAD....!
SO...Dr. Gwakisa and Dr. michael......TANZANIA is our country, and above all ...there are many people who have sensitive and important informations on different matters done against our beloved country.No matter what....but as GOOD CITIZENS we should report these things to the SERIOUS AUTHORITIES which they cant hesitate to take measures against them...!
MY REQUEST:
Most of us (no research done),do not know where we can tell our heart's secrets and still remain HEART'S SECRETS...! Can we have somewhere (people/offices) where sensitive issues could be dirrected to?
REGARDS....!
 
Asante Mkuu Ngogo,let sleeping dogs lie.Lakini kwa nchi yetu inabidi tuwe macho kwa influx hii ya pesa haramu, pesa ni tamu lakini hawa wasomali lazima wataunda utaratibu wa kuilinda pesa hiyo hapa nchini.Na hapo ndo nakubaliana na wewe kuwa vyombo vyetu viwe makini na long term repercursions za "uwekezaji" huu.Tusije sema hatukuliona hili, swala ambalo sasa lipo peupe kabisa.
Lole, pole bwana unaoneka kabisakabisa unauchungu na nchi yako....lkn vyombo unavyovitaka viwe makini kwasasa haviioni kabisa hatari hii!Wao hatari kwa nchi yetu ni Chadema! Ndiyo wako bize kutuma majasusi usiku na mchana kuwafuatilia huku adui hasa akiachwa ajiimarishe!
 
Hizi Chuki zisizo na Mbele wala Kichwa hazitufikishi popote pale....

Wangekuwa wasomali Ombaomba barabarani sijui tungesemaje...? Watu wanachakarika sisi Tunaumiya mioyo...Hii ni Mioyo ya Hasadi kuona wewe huna, basi na mwezio nae awe hana.

Hivi hizi pesa zinaitwa za Utekaji meli...zinafika kiasi gani...? Tuweni wakweli...?...kuna Kiasi wanachohitaji waporaji meli na Kuna kiasi halisi wanachopewa...!!!....Yule Mtanzania aliekuwa Jambazi kule London mbona hawasemi watanzania wote ni wezi...?

Unajua wakati wa Vita kunakuwa hakuna serikali ya kusimamia.Hivyo watu wanafanya biashara watakavyo. na si kusema eti wasomali wanafanya biashara haramu...Assume pale bandarini kungekuwa hakuna hakuna serikali/TRA...bei za vitu vingekuwa kama hizi za sasa?

Tuache Chuki na Hasadi zisizo na Maana. Sisi Watanzania tuna Uvivu na majungu miongoni mwetu. Hata ndugu zetu waliopo nje ya nchi wengi wao wapo hivyo. hawana business ya maana wanayofanya.
 
Back
Top Bottom