Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,599
Wanabodi,
Hili ni bandiko la swali, ambalo jibu lake rasmi litapatikana baada ya October 28, 2020, ila kama una majibu, unaweza kuchangia kujibu na sio lazima tusubiri hadi hiyo October 2020.
Angalizo:
Naomba kuanza hili bandiko na angalizo la mawazo masafi, tusome bandiko hili tukiwa na mawazo masafi, ukiwa ni mtu wa mawazo masafi utasoma kile kilichoandikwa na sio unachofikiria,
Mfano Katerero ni Kijijini mkoani Kagera ni Siku ya Gulio Katerero ni moja ya hadithi kwenye somo la Kiswahili Darasa la 4 enzi zetu, hivyo ukizungumzia mambo ya Kijiji cha Katerero kwa wenye mawazo masafi mtaelewana. Hii mada yangu ni kuhusu maharage ya chakula, yale ya kupika ambayo ndio kitowea kinachoongoza kutumika Tanzania.
Kuna hoja kuwa kauli huwa zinaumba, sasa kuna hii kauli ya "Maharage ya Mbeya Maji Mara Moja", Jee kauli hii ina ukweli wowote kuwa ukipika maharerage ya sehemu nyingine zote, ili yaive lazima uongeze maji zaidi ya mara moja, lakini ukipika maharage ya Mbeya, ukiweka maji, ni mara moja tuu hadi yanaiva?.
Kama kauli hii ni kweli kwa maharage ya Mbeya, maji ni mara moja tuu, jee ni kwa maharage tuu au hata kwa wana Mbeya wenyewe yaani Wambeya, nao pia ni ukiwa na shida yoyote, maji ni mara moja tuu, wanatepeta, wanalainika, na kufikia maamuzi ya kukubali au kukataa jambo lolote, mara moja tuu, kirahisi rahisi, kiulani?.
Nauliza hivi kufuatia siasa za Mbeya kuwa ni very interesting. Kwa kawaida huwa tukielekea uchaguzi Mkuu, hadi humu jf huwa kunapandishwa uzi maalum kwa "Siasa za Mbeya " kufuatia siasa za Mbeya kuwa very interesting zenye msisimko wa ajabu!.
Kipindi hiki cha miaka 4 ya awamu ya tano, tumeshuhudia harakati nyingi za wazi na za chini chini zikiandamana na changamoto za kisiasa jijini Mbeya ikiwamo kumsweka lupango Mbunge wa Mbeya, ili watu wamchukie kwa kumuona ni mhalifu, kwa hoja hizo hizo kama za maharage ya Mbeya, lakini wana Mbeya badala ya kumchukia ndio kwanza wanazidi kumpenda!.
Kikafuatia kituko cha mwaka kwa kufanya ibada ya kishetani ya kula nyama za maiti kwa kutengeneza jeneza tupu na kulifunika kwa bendera ya Chadema kisha kulizika, ili kuashiria kifo rasmi cha Chadema Mbeya, kitendo ambacho kilitafsiriwa kama kufuru kwa Mwenyenzi Mungu, hivyo wajuzi wa mambo wakabashiri kuwaka kwa hasira ya Mungu juu ya waliofanya kitendo hicho cha kufuru.
Badala ya hasira ya Mungu kuwaka kwa CCM Mbeya walikofanya uhayawani huo, ndio kwanza nyota ya CCM jijini Mbeya inavyazidi kung'aa baada ya juzi kati, Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya akiandamana na madiwani lukuki waliojitambua, walipojiengua Chadema Mbeya na kuibukia CCM Dodoma na kutangaza kujitoa Chadema na kujiunga CCM.
Leo online TV ya Ayo, imefanya mahojiano na Mbunge wa Mbeya, Mhe. Joseph Mbilinyi, Sugu na hiki ndicho Sugu alichosema.
Ila maneno haya ya Sugu, yanaongeza hamasa, shamra shamra na mashamsham ya siasa za Mbeya kuelekea October 28, 2020, haswa kwa kuzingatia kigogo mmoja wa CCM anayejipitisha pitisha Mbeya hadi na majeneza, kama ikitokea CCM ikampitisha huyo kigogo wa majeneza, halafu wana Mbeya wakampiga chini, then hii kauli ya "Maharage ya Mbeya Maji Mara Moja" itakuwa ni maharage tuu lakini wana Mbeya sio maji maji, mtepeto, bali ni wagumu kama jiwe au kisiki cha mpingo.
Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu, Kauli ya "Maharage ya Mbeya Maji Mara Moja" Ina Ukweli?, Ni Kwenye Maharage tu au Hadi kwa Wanambeya?:
Je, October 28, 2020 Wana Mbeya WaTatulia, au kwa sababu wameisha zoea shida hadi wameota Sugu hivyo badala ya KuTulia, wao wataendelea za Sugu zao walizozoea?
Kauli Huumba!, Jibu la kama WanaMbeya ni kama Maharage ya Mbeya ya maji mara moja au au hapana ni October 28, 2020!.
Mbeya Oye!.
Paskali
Update.
Ni kweli kabisa, maharage ya Mbeya, maji mara moja!. Na sio maharage mboga tuu, hata .. ya kubadili mboga, ni maji mara moja!, kubwa kuliko ni hata kwenye siasa, Wanambeya ni maji mara moja!, wameamua kuachana na kutiana Sugu na badala yake wameamua ku Tulia na Tulia!.
Mbeya Oye...!.
P
Hili ni bandiko la swali, ambalo jibu lake rasmi litapatikana baada ya October 28, 2020, ila kama una majibu, unaweza kuchangia kujibu na sio lazima tusubiri hadi hiyo October 2020.
Angalizo:
Naomba kuanza hili bandiko na angalizo la mawazo masafi, tusome bandiko hili tukiwa na mawazo masafi, ukiwa ni mtu wa mawazo masafi utasoma kile kilichoandikwa na sio unachofikiria,
Mfano Katerero ni Kijijini mkoani Kagera ni Siku ya Gulio Katerero ni moja ya hadithi kwenye somo la Kiswahili Darasa la 4 enzi zetu, hivyo ukizungumzia mambo ya Kijiji cha Katerero kwa wenye mawazo masafi mtaelewana. Hii mada yangu ni kuhusu maharage ya chakula, yale ya kupika ambayo ndio kitowea kinachoongoza kutumika Tanzania.
Kuna hoja kuwa kauli huwa zinaumba, sasa kuna hii kauli ya "Maharage ya Mbeya Maji Mara Moja", Jee kauli hii ina ukweli wowote kuwa ukipika maharerage ya sehemu nyingine zote, ili yaive lazima uongeze maji zaidi ya mara moja, lakini ukipika maharage ya Mbeya, ukiweka maji, ni mara moja tuu hadi yanaiva?.
Kama kauli hii ni kweli kwa maharage ya Mbeya, maji ni mara moja tuu, jee ni kwa maharage tuu au hata kwa wana Mbeya wenyewe yaani Wambeya, nao pia ni ukiwa na shida yoyote, maji ni mara moja tuu, wanatepeta, wanalainika, na kufikia maamuzi ya kukubali au kukataa jambo lolote, mara moja tuu, kirahisi rahisi, kiulani?.
Nauliza hivi kufuatia siasa za Mbeya kuwa ni very interesting. Kwa kawaida huwa tukielekea uchaguzi Mkuu, hadi humu jf huwa kunapandishwa uzi maalum kwa "Siasa za Mbeya " kufuatia siasa za Mbeya kuwa very interesting zenye msisimko wa ajabu!.
Kipindi hiki cha miaka 4 ya awamu ya tano, tumeshuhudia harakati nyingi za wazi na za chini chini zikiandamana na changamoto za kisiasa jijini Mbeya ikiwamo kumsweka lupango Mbunge wa Mbeya, ili watu wamchukie kwa kumuona ni mhalifu, kwa hoja hizo hizo kama za maharage ya Mbeya, lakini wana Mbeya badala ya kumchukia ndio kwanza wanazidi kumpenda!.
Kikafuatia kituko cha mwaka kwa kufanya ibada ya kishetani ya kula nyama za maiti kwa kutengeneza jeneza tupu na kulifunika kwa bendera ya Chadema kisha kulizika, ili kuashiria kifo rasmi cha Chadema Mbeya, kitendo ambacho kilitafsiriwa kama kufuru kwa Mwenyenzi Mungu, hivyo wajuzi wa mambo wakabashiri kuwaka kwa hasira ya Mungu juu ya waliofanya kitendo hicho cha kufuru.
Badala ya hasira ya Mungu kuwaka kwa CCM Mbeya walikofanya uhayawani huo, ndio kwanza nyota ya CCM jijini Mbeya inavyazidi kung'aa baada ya juzi kati, Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya akiandamana na madiwani lukuki waliojitambua, walipojiengua Chadema Mbeya na kuibukia CCM Dodoma na kutangaza kujitoa Chadema na kujiunga CCM.
Leo online TV ya Ayo, imefanya mahojiano na Mbunge wa Mbeya, Mhe. Joseph Mbilinyi, Sugu na hiki ndicho Sugu alichosema.
Kama ni kweli Katibu Mkuu wa CCM ndiye anawapigia simu kuwato..oza wahame, kiukweli hii ni aibu kubwa!.Nimemsikia mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi aka Sugu kupitia ayo tv akidai alipigiwa simu na Katibu mkuu wa CCM Dr Bashiru Ally ili ajiunge nao lakini amemkatalia.
Sugu amedai kuwa sura yake siyo ya CCM na kwamba wanaohamia chama tawala ni wale Wajinga wajinga.
Hizi lugha za kihuni hazipaswi kutumiwa na wabunge wamwachie Hajji Manara.
Maendeleo hayana vyama!
Ila maneno haya ya Sugu, yanaongeza hamasa, shamra shamra na mashamsham ya siasa za Mbeya kuelekea October 28, 2020, haswa kwa kuzingatia kigogo mmoja wa CCM anayejipitisha pitisha Mbeya hadi na majeneza, kama ikitokea CCM ikampitisha huyo kigogo wa majeneza, halafu wana Mbeya wakampiga chini, then hii kauli ya "Maharage ya Mbeya Maji Mara Moja" itakuwa ni maharage tuu lakini wana Mbeya sio maji maji, mtepeto, bali ni wagumu kama jiwe au kisiki cha mpingo.
Namalizia kwa lile swali la msingi la uzi huu, Kauli ya "Maharage ya Mbeya Maji Mara Moja" Ina Ukweli?, Ni Kwenye Maharage tu au Hadi kwa Wanambeya?:
Je, October 28, 2020 Wana Mbeya WaTatulia, au kwa sababu wameisha zoea shida hadi wameota Sugu hivyo badala ya KuTulia, wao wataendelea za Sugu zao walizozoea?
Kauli Huumba!, Jibu la kama WanaMbeya ni kama Maharage ya Mbeya ya maji mara moja au au hapana ni October 28, 2020!.
Mbeya Oye!.
Paskali
Update.
Ni kweli kabisa, maharage ya Mbeya, maji mara moja!. Na sio maharage mboga tuu, hata .. ya kubadili mboga, ni maji mara moja!, kubwa kuliko ni hata kwenye siasa, Wanambeya ni maji mara moja!, wameamua kuachana na kutiana Sugu na badala yake wameamua ku Tulia na Tulia!.
Mbeya Oye...!.
P