Mahakama yazuia mkataba wa TANESCO, DOWANS!

Gurudumu

JF-Expert Member
Feb 5, 2008
2,349
261
Nusu saa iliyopita (2/3/2011), katika mahakama kuu ya tz Dsm, jaji Mushi ametoa hukumu kuwa Tanesco/Serikali wasifanye makubaliano au maridhiano yoyote hadi waombe idhini kutoka mahakama yake.

Uamuzi huo unafuatia maombi ya mawakili wanaowakilisha wanaharakati wanaopinga kusajiliwa na kulipwa kwa tuzo ya Dowans.

Hii hukumu inajumuisha nia yoyote ya kuingia makubaliano kuwasha mitambo ya Dowans au makubaliano yoyote yanayohusu kupunguza au kusamehe tuzo ya Dowans

Pia ametoa hukumu kwamba hatakiwi mtu yoyote kuzungumzia au kutoa ufafanuzi hadharani kuhusu Tuzo hiyo ya Dowans. Hukumu hiyo ilikuwa kwa mujibu wa mmoja wa Objectors aliyeisomea mahakama gazeti la Mwananchi la tarehe 25 February 2011 ambalo lilimnukuu Mkurugenzi wa Fedha wa Dowans (Stanley Munai) aliyekuwa anawafafanulia waandishi wa habari kuhusu jinsi hukumu hiyo ilivyokuwa halali na kwamba Tanesco hawatakiwi kukata rufaa

Kesi itatajwa tena tarehe 30 Machi 2011

KAMATI ya Bunge ya Nishati na Madini imependekeza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kuingia mkataba mpya na Kampuni ya kufua umeme ya Dowans ikiwa ni hatua za muda mfupi kukabiliana na tatizo la umeme nchini.

Hata hivyo, Mahakama Kuu imeizuia Serikali na Tanesco kuchukua hatua yoyote inayohusiana na mazungumzo au mkataba wa aina yoyote baina yake na Dowans bila ridhaa yake.

Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, Januari Makamba alisema: "Kamati imependekeza mambo 30 ikiwamo kuwashwa kwa mitambo ya Dowans haraka na serikali itoe fedha zaidi kununua mafuta mazito ya kuendeshea mitambo ya IPTL. Hatua hii imefikiwa kama suluhisho la muda mfupi la kupambana na mgawo.''

Makamba alisema pia kwamba kamati imependekeza kupunguzwa kwa megawati 50 kutoka katika migodi ya madini inayotumia umeme wa megawati 125 ili zipelekwe kwa wananchi.

Makamba ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bumbuli mkoani Tanga alisema mapendekezo hayo watayakabidhi katika Ofisi za Bunge na kwamba yatatangzwa na Spika, Anne Makinda

Lakini, wakati kamati ikitoa mapendekezo hayo, jana Jaji Emilian Mushi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam anayesikiliza maombi ya usajili wa tuzo ya Kampuni ya Dowans iliyoshinda iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara(ICC), dhidi ya Tanesco alitoa agizo kuwa lisifanyike jambo lolote kuhusu Dowans nje ya mahakama.

"Naagiza jambo lolote lisifanyike nje ya mahakama wakati ikiendelea na shauri hili. Kama kutahitajika kuwa na majadiliano yoyote basi pande husika zilete maombi mahakamani ili iweze kusimamisha kwanza mchakato huu kusubiri majadiliano hayo."

Jaji Mushi alisema: "Haitakuwa vyema mahakama kuendelea na mchakato wakati na huko nje majadiliano yakiendelea. Kama pande hizo zikiafikiana, basi zinaweza kuja ‘ku-withdraw' (kuondoa shauri) na kama zitashindwana basi ndipo tutakapoendelea na mchakato."


Source: Gazeti la Mwananchi
 
sasa huu ni moto mwingine wa mjadala umewashwa. sijui kwanini serikali haitaki kuachana na hili dudu la dowans
 
Hukumu hii itamshitua sana January Makamba na genge lake...Sijui watamjibu nini Al-Hadaiwi!...Je watamrudishia alichowakatia?
 
nawashukuru sana wanaharakati waliojitolea katika kutetea KATIBA ya nchi hususan ibara 27.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya Jamhuri ya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia kuiheshimu mali ya mtu mwingine.
(2) Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya mamlaka ya nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhilifu, na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao.

nawatakia mapambano mema katika kutetea nchi yetu ya tanzania.
 
Sasa Pinda hakujua kwamba kuna kesi mahakamani. Kweli viongoze wetu vibonzo kweli kweli. Pinda huyo huyo ndiye aliyezuia mjadala wowote wa Dowans bungeni kwa sababu kuna kesi iko mahakamani. Baada ya kikao cha bunge Pinda na January wako bize na majadiliano na Dowans!
 
Kwasababu wako juu ya Sheria na mahakama inatakiwa kuwasikia wao, hii ni ajabu sana! CDM endeleeni kutuhabarisha swala hili la DOWANS kwa hiyo operations maalum mpaka Watanzania wote tuelewe bayana kuna siri gani iliyojicha humu. LAkini pia tungependa kujua ile mikataba yote ambayo imefanyika na imekuwa siri lakini haina maslahi kwa Taifa tuijue. Kama kuna uwezekano ikachapishwa kwa Kiswahili ili wote waielewe kama shida iwekwe tu kwa kiingereza.
Hasa ile ya madini!

PEEEEEOPLES!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
sasa kazi nyingine tena inaibuka..yaani tz kila siku na jambo lake..
 
Kwenye Gazeti la Majira kuna Kibonzo kina mshiriki pale anaitwa ZIRO NAJARIBU KUTAFUTA MTU ANAYEFAA KUFANANISHWA NAYE nisaidieni wana JF Maana kila nikiviangalia vile vituko vyake naona anafanana na watu wetu muhimu.
 
Nusu saa iliyopita, katika mahakama kuu ya tz Dsm, jaji Mushi ametoa hukumu kuwa Tanesco/Serikali wasifanye makubaliano au maridhiano yoyote hadi waombe idhini kutoka mahakama yake.

Uamuzi huo unafuatia maombi ya mawakili wanaowakilisha wanaharakati wanaopinga kusajiliwa na kulipwa kwa tuzo ya Dowans.

Hii hukumu inajumuisha nia yoyote ya kuingia makubaliano kuwasha mitambo ya Dowans au makubaliano yoyote yanayohusu kupunguza au kusamehe tuzo ya Dowans

Pia ametoa hukumu kwamba hatakiwi mtu yoyote kuzungumzia au kutoa ufafanuzi hadharani kuhusu Tuzo hiyo ya Dowans. Hukumu hiyo ilikuwa kwa mujibu wa mmoja wa Objectors aliyeisomea mahakama gazeti la Mwananchi la tarehe 25 February 2011 ambalo lilimnukuu Mkurugenzi wa Fedha wa Dowans (Stanley Munai) aliyekuwa anawafafanulia waandishi wa habari kuhusu jinsi hukumu hiyo ilivyokuwa halali na kwamba Tanesco hawatakiwi kukata rufaa

Kesi itatajwa tena tarehe 30 Machi 2011


Chadema kuweni makini katika kuzungumzia DOWANS inawezekana ni mtego wa ndege tunduni.Ikiwezekana waongee kwa ufupi bila kuathiri kesi iliyopo.Yawezekana hIKI NI MOJA YA VISHINDO ALIVYOACHA JK. Dr.atahadhalishwe na wale walio karibu naye hasa kwa siku kuanzia leo
 
Chadema kuweni makini katika kuzungumzia DOWANS inawezekana ni mtego wa ndege tunduni.Ikiwezekana waongee kwa ufupi bila kuathiri kesi iliyopo.Yawezekana hIKI NI MOJA YA VISHINDO ALIVYOACHA JK. Dr.atahadhalishwe na wale walio karibu naye hasa kwa siku kuanzia leo

Hili ni muhimu sana hasa sasa hivi kwenye hizo kampeni za maandamano
 
Mitambo ya Dowans sasa kuwashwa - Waziri Mkuu Pinda
Waziri Mkuu Mizengo Pinda leo ametamka rasmi kuwa TANESCO itaingia mkataba mpya na Dowans wa kuzalisha umeme.

Amesema mitambo ya Dowans itawashwa muda wowote kuanzia sasa licha ya kesi iliyopo mahakamani kuhusu tozo ya ICC.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuhutubia mkutano ulioandaliwa na The Economist kwenye hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam, Pinda alisema kuwa ni vyema SONGAS au kampuni nyingine binafsi inakununua mitambo ya Dowans siku zijazo ili iendelee kuzalisha umeme nchini.

Alisema hivi sasa kuna upungufu wa 160MW kwenye gridi, hivyo 100MW ya Dowans ingesaidia kupunguza makali ya mgao.

Pinda alisema serikali kununua mitambo ya Dowans imeleta maneno mengi kuwa haiwezekani serikali ikanunua mitambo iliyotumika, hivyo ameona suluhisho ni kwa SONGAS au mfanyabiashara mwingine mkubwa anunue mitambo ya Dowans na aingie kwenye mkataba wa muda mrefu na TANESCO wa kuzalisha umeme.

Tayari Baraza la Mawaziri limetoa kibali kwa TANESCO kuingia mikataba ya kukodi umeme kama ya Richmond/Dowans ili kupata 260MW.

Sasa hivi inasubiriwa bodi ya wakurugenzi ya TANESCO itoe tamko rasmi kuwa serikali itaingia mkataba mpya na DOwans.

Hivi hawa mafisadi wa DOWANS wataendelea kupora pesa za wavuja jasho wa Tanzania mpaka lini?
 
Haya pinda mzee wa kupindisha ushatuambia dowans inawashwa kumbe hujafanya research yeyote kweli wewe ni kilaza!
 
Mitambo ya Dowans sasa kuwashwa - Waziri Mkuu Pinda
Waziri Mkuu Mizengo Pinda leo ametamka rasmi kuwa TANESCO itaingia mkataba mpya na Dowans wa kuzalisha umeme.

Amesema mitambo ya Dowans itawashwa muda wowote kuanzia sasa licha ya kesi iliyopo mahakamani kuhusu tozo ya ICC.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuhutubia mkutano ulioandaliwa na The Economist kwenye hoteli ya Kempinski jijini Dar es Salaam, Pinda alisema kuwa ni vyema SONGAS au kampuni nyingine binafsi inakununua mitambo ya Dowans siku zijazo ili iendelee kuzalisha umeme nchini.

Alisema hivi sasa kuna upungufu wa 160MW kwenye gridi, hivyo 100MW ya Dowans ingesaidia kupunguza makali ya mgao.

Pinda alisema serikali kununua mitambo ya Dowans imeleta maneno mengi kuwa haiwezekani serikali ikanunua mitambo iliyotumika, hivyo ameona suluhisho ni kwa SONGAS au mfanyabiashara mwingine mkubwa anunue mitambo ya Dowans na aingie kwenye mkataba wa muda mrefu na TANESCO wa kuzalisha umeme.

Tayari Baraza la Mawaziri limetoa kibali kwa TANESCO kuingia mikataba ya kukodi umeme kama ya Richmond/Dowans ili kupata 260MW.

Sasa hivi inasubiriwa bodi ya wakurugenzi ya TANESCO itoe tamko rasmi kuwa serikali itaingia mkataba mpya na DOwans.

Hivi hawa mafisadi wa DOWANS wataendelea kupora pesa za wavuja jasho wa Tanzania mpaka lini?

Usishangae kwamba tayari wameshasaini mkataba mwingine, na ukaja kuonekana kwamba ni batili na wa kifisadi. Spidi ya January na Ali Hadaiwi ilikuwa kubwa mno
 
hapa mi ndo ninapochoka na serikali ya mkwere..yaani ni vurugu tupu hakuna la maana..Pinda ndo uozo mtupu ..mkimbana sana anaanza kulia
 
hapa mi ndo ninapochoka na serikali ya mkwere..yaani ni vurugu tupu hakuna la maana..Pinda ndo uozo mtupu ..mkimbana sana anaanza kulia

Wewe muache aingilie uhuru wa mahakama akidhani yuko juu, safari hii atalia mpaka chozi la damu hatumuachii, ameokolewa na mama yao sakata la Mh.Lema
 
Back
Top Bottom