JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya kupinga kusimikwa Askofu mpya mteule, Geofrey Mwakihaba na kupinga kuondolewa madarakani kwa Askofu Dk Edward Mwaikali katika mkutano Mkuu wa Dayosisi uliofanyika Machi 22, 2022.
Kesi hiyo iliyofunguliwa na askofu aliyeondolewa katika Dayosisi ya Konde ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Mwaikali ilianza kuunguruma juzi Jumatano.
Leo Ijumaa Juni 3, 2022 Jaji wa Mahakama hiyo, James Karayemaha ametoa uamuzi huo baada ya kusikiliza pande zote kupitia kwa mawakili wao.
Jaji Karayemaha amefafanua kuwa upande wa mleta maombi ukiwakilishwa na wakili William Mashoke amesema ilipokea mapingamizi yote mawili yaliyosikilizwa kwa pamoja.
"Hivyo mleta maombi aliruka vipengele vya maamuzi kwa kutofuata utaratibu kwa kuzingatia Katiba ya KKKT ya mwaka 2015 ila kama hajaridhika na uamuzi wa mahakama anaweza kukataka rufaa," amesema Jaji Karayemaha.
Source: Mwanahalisi
Kesi hiyo iliyofunguliwa na askofu aliyeondolewa katika Dayosisi ya Konde ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Mwaikali ilianza kuunguruma juzi Jumatano.
Leo Ijumaa Juni 3, 2022 Jaji wa Mahakama hiyo, James Karayemaha ametoa uamuzi huo baada ya kusikiliza pande zote kupitia kwa mawakili wao.
Jaji Karayemaha amefafanua kuwa upande wa mleta maombi ukiwakilishwa na wakili William Mashoke amesema ilipokea mapingamizi yote mawili yaliyosikilizwa kwa pamoja.
"Hivyo mleta maombi aliruka vipengele vya maamuzi kwa kutofuata utaratibu kwa kuzingatia Katiba ya KKKT ya mwaka 2015 ila kama hajaridhika na uamuzi wa mahakama anaweza kukataka rufaa," amesema Jaji Karayemaha.