baharia Ar
JF-Expert Member
- Dec 1, 2013
- 837
- 316
Wajaribu kumkamata tuone this time patachimbika
Mahakama yameamuru Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila akamatwe na kufikishwa mahakamani mara moja kwa kosa la kumuita Jaji Werema mwizi. Aidha,Kafulila anashtakiwa kwa kuibua tuhuma za ESCROW bungeni kwa namna ambayo haikuwa sahihi kisheria.
MAONI YANGU:
Naona sasa CCM wameanza kuweweseka. Watulie sindano ziingie ili wajipange tena kurejea madarakani mwaka 2020.
========================
Chanzo: Nipashe
Nimependa ushauri huu!! .
.
WANA CCM NISIKILIZENI..!!
Nina ushauri kwa wana CCM wenzangu; Lowasa kuhamia CHADEMA msipaniki. Kama kweli tulimaanisha kuwa hafai, ana uchu wa madaraka, alikiuka kanuni na maadili ya chama, ni mwizi na tena ni fisadi basi inabidi tushangilie kuondoka kwake, kwani kuvuja kwa pakacha sio ndio nafuu ya mchukuzi? Ila kama tulimkata kwa maslahi ya watu wachache na ikiwa tulitumia akili ndogo kulikata jina lake basi itabidi tujilaumu wenyewe kwa lolote tusilolitarajia litakalotokea.
Na tukiendelea kutumia akili ndogo za kudhani tutashinda kwa "magoli ya mikono", basi tunakwenda na maji mchana kweupe!
.
Tukijidanganya kuwa matusi, kejeli, mipasho, maneno ya kwenye kanga na nyimbo za Komba kwamba zitabadilisha huu upepo, pia tutajikuta tunakuwa chama cha upinzani bila hata kujiandaa kisaikolojia. Mwana CCM utakuwa unajichanganya kuushambulia uamuzi wa Lowasa kuhamia CHADEMA kwa sababu kimsingi CCM yetu ilishabariki vijana kadhaa wamshambulie majukwaani ili aonekane hafai na hao vijana wakazawadiwa vyeo. Mtu tuliemuona hafai kwetu inatuuma nini akiondoka kwetu? Ukioa mke kisha ukamtuhumu mbele za watu kuwa ni mzinzi na mshirikina; kisha mkaachana na akaolewa na mume mwingine, unaanzaje kuhangaika nae tena huko alikoenda? Tuwaache wapiga kura waamue kama ni sisi CCM ama UKAWA. .
.
Hata Mh. Mwenyekiti JK alishasema kila mtu ana haki kuongoza hii nchi; tunategemea kushinda lakini haitakuwa ajabu UKAWA wakitwaa madaraka kutokana na makosa yetu kimkakati. Wana CCM tusipaniki, kukomaa kisiasa ni pamoja na kuhimili na kukubali usichotarajia!
Wenu,
Mfurukutwa wa Shina.
😂😂👆
unanini cha kufanya nchi isitawalike? huo uhuni wako wa kutembea na sumu mfukoni ndiyo ufanye nchi isitawalike we kiazi kweli.
inawezekana alikua ktk list ya watu waliokua wanataka kununuliwa sasa akakataa ndio wana mbabaisha ili akubalia!!
Mkuu nashindwa kuelewa kwani maelezo yako yanatofautiana na kiambatanishi ulichoweka toka gazeti NIPASHE.
Sasa hiyo kesi tuelewe ni ya ESCROW au lugha ya matusi.
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Hiyo habari nimeisoma on line,anashitakiwa kwa kosa la kumuita mkuu wa wilaya khadija nyembo kuwa hana maadili,pia hakufika mahakamani kwani wakili hakumjulisha.
Mleta mada ungeweka habari yote si kutunga uongo,make hata jaji welema hakuna alipoandikwa wala ishu ya escrow hakuna ilipoandikwa kwenye hiyo habari.
Mkuu nashindwa kuelewa kwani maelezo yako yanatofautiana na kiambatanishi ulichoweka toka gazeti NIPASHE.
Sasa hiyo kesi tuelewe ni ya ESCROW au lugha ya matusi.
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Mkuu nashindwa kuelewa kwani maelezo yako yanatofautiana na kiambatanishi ulichoweka toka gazeti NIPASHE.
Sasa hiyo kesi tuelewe ni ya ESCROW au lugha ya matusi.
MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
Napita tu"!!Ccm wasije leta mahafa watanzania wamechoka!!
Mtaisoma Namba cku ikifika na Fisadi wenu Mmeru aliyekataa kabila lako!!!Watanzania wamechoka na michezo michafu ya ccm na fisadi kikwete, escrow, richmond, dawasco, na kadhalika
Mtaisoma Namba cku ikifika na Fisadi wenu Mmeru aliyekataa kabila lake!!!Watanzania wamechoka na michezo michafu ya ccm na fisadi kikwete, escrow, richmond, dawasco, na kadhalika
Mtaisoma Namba cku ikifika na Fisadi wenu Mmeru aliyekataa kabila lako!!!Watanzania wamechoka na michezo michafu ya ccm na fisadi kikwete, escrow, richmond, dawasco, na kadhalika