Mahakama ya Kisutu yawaachia huru Masamaki na wenzake watano

Sijawahi kuwaamini hawa mapopoma wa sheria wa serikali hii! unawaachiaje watu mlituaminisha wana nyumba sabini na ngapi sijui
Nyumba sabini sii zakwake alijenga na mshahara wake,kwani alishikiliwa kwa ajili ya nyumba? Mtu kafanya kazi tangu miaka ya themanini atashindwaje kujenga nyumba sabini nyumba zenyewe nje ya mji Kiwanja hela kumi alinunu kwa milioni tano?mchanga lory huko 30,000?
 
hawajapona hawa kesho wanarudishwa kwa mashitaka 45 kama miaka yao, hapo walikurupuka hawakuwa na ushahidi wa kutosha Magu hawezi kuwaacha hivi hivi
 
Siasa za hii miaka hasa 2015/20 ni kutafuta kiki. Hakuna mambo yanayofanyika kwa uhalisia wake. Walikamata wakawaaminisha watu wote kuwa hawa watu wamehujumu nchi kisha mwaka tu baadae unasema hakuna kesi. Ujinga kabisa huu. Sema tu watanzania nao ni mafala

Sent from my SM-J200H using JamiiForums mobile app
 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemuachia huru aliyekuwa Kamishna wa TRA, Tiagi Masamaki na Wenzake watano waliokuwa wakishtakiwa na makosa ya uhujumu uchumi na kuisababishia serikali hasara ya sh. Bilioni 12.7.

Washtakiwa hao wameachiwa na Hakimu Mkazi Huruma Shahidi baada ya upande wa mashtaka uliokuwa ukiongozwa na wakili wa Serikali Mwandamizi, Timon Vitalis kuiomba mahakama kufanya hivyo chini ya kifungu cha 91(1) ya makosa ya jinai (CPA) kuwa DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa hao.

"Mheshimiwa Hakimu kesi hii leo imekuja kwa ajili ya kutajwa, hata hivyo tuna maombi, DPP amewasilisha Nolle Prosque, hana nia ya kuendelea na mashtaka dhidi ya washtakiwa", amesema Wakili wa Serikali Timon Vitalis.
Hakimu Shahidi alikubaliana na ombi hilo na kuwaachia huru washtakiwa.

Mbali na Masamaki, washtakiwa wengine waliokuwa katika kesi hiyo iliyotokana na sakata la makontena 329 ni Meneja Kitengo cha Huduma za Ushuru TRA, Habib Mponezya (45) na Meneja Msimamizi na Ufuatiliaji wa Forodha, Burton Mponezya (51).

Msimamizi Mkuu Kitengo cha Ushuru wa Forodha ICD Azam, Eliachi Mrema (31), Mchambuzi Mwandamizi wa Masuala ya Biashara TRA, Hamis Omary (48), Meneja wa Oparesheni za Usalama na Ulinzi ICD, Raymond Adolf Louis (39) na Meneja wa Azam ICD, Ashrafu Khan (59) na Haroun Mpande (28) wa kitengo cha Mawasiliano ya Kompyuta ICT TRA.

Hata hivyo, DPP amewafutia mashtaka watuhumiwa watano tu ambao ni,Tiagi Masamaki, Eliachi Mrema, Habibu Mponezya, Burton Mponezya na Ashraf Khan.

Hata hivyo, Raymond Louis, Haruni Mpande na Khakis Ally Omari wameendelea kushikiliwa na kusomewa mashtaka mapya pamoja na watuhumiwa wapya, Khalid Yusuph Hassan na Benson Vitalis Malembo.

Chanzo: Michuzi Blog
Kuna uwezekano mkubwa Kwa hao walioachiwa kuwa wametoa ushirikiano Kwa serikali Kwa kukubali mali zao kuwa mali Za serikali Na kwenye Kesi ya msingi wao watakuwa mashahidi, Na wafanyabiashara husika kutakiwa kulipa hizo kodi
 
Mahakama mafisadi nicheke mie na tanzania ya maskini wa akili na roho

Sent from my SM-J200H using JamiiForums mobile app
 
Hao wanachezewa mchezo, DPP kaona kafungua vibaya kesi hiyo ameifuta ili awakamate tena nakuifungua vzr....kweny serikal hii hutaachiaa kirahis

Sent from my GT-I9105P using JamiiForums mobile app
 
Uwaga wana kamata watu bila ya kujenga kesi kwanza.

Ndio ujue ata Rugemalila na PAP kikubwa ni wivu tu lakini kisheria escrow ni hela yao.
 
Ndio mana Nyoka mwenye makengeza na vijisent, hela za mboga mboga nk wanaendelea kudunda.,

Hii nchi itahitaji ata miaka 1000 zaidi kutoka hapa ilipo angalau kupiga hatua 1 mbele.
 
Nadhani serikali imeshachukua chake kutoka kwao kwa kuwafilisi mali walizokuwa wanamiliki,kwahiyo "nahisi" wanarudi uraiani kuanza moja,Magufuli hawezi kuwaachia watu waliokula mabilioni ya pesa kiurahisi hivo.
Unahisi?? Mbona mlitaka front page, mkasema wana nyumba sabini, semeni mmezitaifisha ili mpate tena front page

Sent from my SM-J200H using JamiiForums mobile app
 
kuna uwezekano mkubwa hii kesi ikawa drafted upya ili kuipa uwezo wa kisheria mahakama ya mafisadi kuwafunga hakina masamaki.
DPP ameona loopholes zilizopo kwenye sheria za mahakama za kawaida kabla ya kuundwa kwa mahakama ya mafisadi. So ameamua aondoe kesi huku ili ashitakiwa kwenye mahakama ya mafisadi. If this is true then it is a good move.
huwezi kushitaki mtu kwa kutumia Font fage za magazetini ama mitandaoni,
inatakiwa ushahidi,

masamaki ni sawa na umkamate mkuu wa wilaya kwa wizi wa dawa kwenye hospital ya wilaya,badala ya kumkamata mtunza store na mlinzi wa store,
huwezi kumfunga japo lokapu utamuweka,
 
Kwahiyo kumbe hawakuwa na kosa kama serikali ya ccm ilivyoaminisha watu. Serikali iache kukurupuka kutafuta attention na mwisho kuambulia aibu.
 
Back
Top Bottom