MAHAKAMA ya hakimu mkazi ya SONGEA yamtia hatiani mwandishi wa habari kwa kosa la RUSHWA

moma2k

JF-Expert Member
Dec 12, 2010
1,061
1,327
Tarehe 14 June,2012 Mahakama ya hakimu mkazi ya mjini Songea mkoni Ruvuma ilimtia hatiani mwandishi wa habari wa kujitegemea KWIRINUS MAPUNDA kwa kosa la RUSHWA(corruption), ambaye amekuwa akiandikia habari zake katika gazeti la Mwananchi. Baada ya kumtia hatiani(convict) mahakama hiyo ilimpa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela au fine ya Tsh.Milioni moja. PCCB(TAKUKURU)-SONGEA(RUVUMA)ndio waliokuwa wakiiendesha kesi hiyo.
 
Alikula rushwa ya nani, ili afanye nini? Atajiju, huyo hana lake tena, maana Mwananchi Songea huwatumia waandishi wa kujitegemea. Na kwa songea huyo nje ya kambi ya Nchimbi.
 
Waandishi wengi wa habari (siyo wote) ndivyo walivyo!! Na siyo waandishi wahabari tu, rushwa nchini ni janga likiwa na mizizi yake ndani ya chama tawala!!
 
Alikuwa akiandika habari mbaya dhidi ya taasisi mojawapo, bila kwenda kupata taarifa sahihi kwa uongozi wa taasisi hiyo.
Hivyo alikuwa anaandika habari za uwongo, uzushi na uchochezi dhidi ya taasisi hiyo ili kuitisha(Habari hizo za uwongo na uzushi alikuwa akiandikia katika gazeti la MWANANCHI). Uongozi wa taasisi hiyo ulikaa kimya bila kuchukua hatua yoyote(no reaction).Baadaye yeye mwenyewe mwandishi wa habari hizo (aliyetiwa hatiani kwa kosa la rushwa) akaenda kuuona uongozi huo na kuomba aandike habari ya kuisafisha taasisi hiyo, akidai alipwe Tsh.milioni 2.5 cash kwa kazi hiyo. Alitoa sharti jingine kuwa malipo hayo yafanyike kwa SIRI KUBWA. Uongozi wa taasisi hiyo ukachukua hatua ya kwenda kuwataarifu PCCB(TAKUKURU). Siku iliyofuata PCCB(TAKUKURU) baada ya kutega mtego wao, walifanikiwa kumkamata akiwa anapokea fedha za PCCB(TAKUKURU) ktk eneo la taasisi hiyo. Ndo ukiwa mwisho wake.
 
Alikuwa akiandika habari
mbaya dhidi ya taasisi mojawapo, bila kwenda kupata taarifa sahihi kwa
uongozi wa taasisi hiyo.
Hivyo alikuwa anaandika habari za uwongo, uzushi na uchochezi dhidi ya
taasisi hiyo ili kuitisha(Habari hizo za uwongo na uzushi alikuwa
akiandikia katika gazeti la MWANANCHI). Uongozi wa taasisi hiyo ulikaa
kimya bila kuchukua hatua yoyote(no reaction).Baadaye yeye mwenyewe
mwandishi wa habari hizo (aliyetiwa hatiani kwa kosa la rushwa) akaenda
kuuona uongozi huo na kuomba aandike habari ya kuisafisha taasisi hiyo,
akidai alipwe Tsh.milioni 2.5 cash kwa kazi hiyo. Alitoa sharti jingine
kuwa malipo hayo yafanyike kwa SIRI KUBWA. Uongozi wa taasisi hiyo
ukachukua hatua ya kwenda kuwataarifu PCCB(TAKUKURU). Siku iliyofuata
PCCB(TAKUKURU) baada ya kutega mtego wao, walifanikiwa kumkamata akiwa
anapokea fedha za PCCB(TAKUKURU) ktk eneo la taasisi hiyo. Ndo ukiwa
mwisho wake.

amevuna alichopanda!
 
"PCCB(TAKUKURU)-SONGEA(RUVUMA)ndio waliokuwa wakiiendesha kesi hiyo."

PCCB tangu lini wanaendesha kesi jamani!?
 
PCCB si tu kwamba wanayo mamlaka ya kupeleleza, bali pia wanayo mamlaka ya kuendesha kesi. wana waendesha mashtaka wao.
 
Hii pia ni habari mbaya kwa tasnia ya habari!.

Hiyo inaitwa black mail!. Mwandishi anatunga au anaandika habari mbaya za mtu au taasisi fulani, wengine huionyesha habari hiyo kabla ya kutoka ili kuicompromise kwa rushwa ili isitoke na akigomewa ndipo anailipua!. Au wengine kuanza na ulipuaji kisha kujidai kutaka kusafisha na kudai chochote!.

Hakuna any justification kwa vitendo hivi vya aibu kwa waandishi wetu. Ila pia lazima nikiri kuwa huu ni ukosefu wa maadili!.

Mbona waandishi waadilifu tupo, sio tuu hatuombi rushwa bali hata kukataa zile free bies za sources!.

Uandishi ni kazi ya wito, kwa sasa fani imevamiwa!. Waandishi wenye wito tupo tukiitumikia fani kwa uadilifu mkubwa huku tukidumu pamoja na umasikini wake huku wavamizi wakizidi kuongezeka kila kukicha na kuitia doa fani yetu!.

NB. Angalizo: Msije kuchanganya mambo. Zile little brown envelopes ambazo huitwa "lunch" au " transport" zile ni haki stahili na sio rushwa!. Hizi mimi huwa nasimamia kuhakikisha waandishi wanapatiwa!.
 
Kifungo miaka 3 au fine million moja? Duu hapa mahakama...., kosa la kupokea rushwa lina fine kumbe? Mi nilikuwa cjui. Duu anabahati sana
 
"PCCB(TAKUKURU)-SONGEA(RUVUMA)ndio waliokuwa wakiiendesha kesi hiyo."

PCCB tangu lini wanaendesha kesi jamani!?

Webondo ni mbumbu wa sheria. PCCB wana mamlaka ya kupeleleza na kuiendesha kesi iliyo chini ya jurisdiction yao kwa mujibu wa sheria inayoiweka taasisi hii.
 
Mla rushwa anapigwa faini!
Kesi hii inafanana sana na ya Jerry Muro. Kumbe hata yy angepata mwanya wa kuchomokea mlango wa faini!
Tofauti ni kuwa faini yake ingekuwa ndefu
 
Alikuwa akiandika habari mbaya dhidi ya taasisi mojawapo, bila kwenda kupata taarifa sahihi kwa uongozi wa taasisi hiyo.
Hivyo alikuwa anaandika habari za uwongo, uzushi na uchochezi dhidi ya taasisi hiyo ili kuitisha(Habari hizo za uwongo na uzushi alikuwa akiandikia katika gazeti la MWANANCHI). Uongozi wa taasisi hiyo ulikaa kimya bila kuchukua hatua yoyote(no reaction).Baadaye yeye mwenyewe mwandishi wa habari hizo (aliyetiwa hatiani kwa kosa la rushwa) akaenda kuuona uongozi huo na kuomba aandike habari ya kuisafisha taasisi hiyo, akidai alipwe Tsh.milioni 2.5 cash kwa kazi hiyo. Alitoa sharti jingine kuwa malipo hayo yafanyike kwa SIRI KUBWA. Uongozi wa taasisi hiyo ukachukua hatua ya kwenda kuwataarifu PCCB(TAKUKURU). Siku iliyofuata PCCB(TAKUKURU) baada ya kutega mtego wao, walifanikiwa kumkamata akiwa anapokea fedha za PCCB(TAKUKURU) ktk eneo la taasisi hiyo. Ndo ukiwa mwisho wake.

Huyu hakuwa 'mwandishi' bali 'magumashi'
 
waandishi wa habari wasiokula rushwa ni wachache sana. nafikiri huyu aliyetiwa hatiani ni mfano mzuri, Jerry muro naye ameonyesha picha halisi ya waandishi wahabari wa tanzania na africa kwa ujumla.
 
Webondo ni mbumbu wa sheria. PCCB wana mamlaka ya kupeleleza na kuiendesha kesi iliyo chini ya jurisdiction yao kwa mujibu wa sheria inayoiweka taasisi hii.
ni kweli wanaendesha mashitaka, lakini lazima wapate consent ya dpp, hakuna sheria inayowapa moja kwa moja mamlaka wao kupeleleza kukamata na kushitaki, wao wanapeleleza, wanakamata alafu wanapeleka maombi kwa dpp yanayoambatana na jalada husika kuomba waendeshe shitaka. ukienda pale kwa dpp, majalada yaliyo mengi ni ya kwao...cha ajabu ni kwamba, ni wabovu mno wa prosecution, hata huyo mwandishi wa habari aliyekuwa convicted, ni bahati tu....skills zao za prosecution na uzoefu wao wa kazi ni mdogo sana....kesi zilizo nyingi wanashindwa, na hawataki kuonekana hawajui...hawashauriki hawa jamaa. PCCB pia ni wala rushwa wakubwa mno...
 
Hii pia ni habari mbaya kwa tasnia ya habari!.

Hiyo inaitwa black mail!. Mwandishi anatunga au anaandika habari mbaya za mtu au taasisi fulani, wengine huionyesha habari hiyo kabla ya kutoka ili kuicompromise kwa rushwa ili isitoke na akigomewa ndipo anailipua!. Au wengine kuanza na ulipuaji kisha kujidai kutaka kusafisha na kudai chochote!.

Hakuna any justification kwa vitendo hivi vya aibu kwa waandishi wetu. Ila pia lazima nikiri kuwa huu ni ukosefu wa maadili!.

Mbona waandishi waadilifu tupo, sio tuu hatuombi rushwa bali hata kukataa zile free bies za sources!.

Uandishi ni kazi ya wito, kwa sasa fani imevamiwa!. Waandishi wenye wito tupo tukiitumikia fani kwa uadilifu mkubwa huku tukidumu pamoja na umasikini wake huku wavamizi wakizidi kuongezeka kila kukicha na kuitia doa fani yetu!.

NB. Angalizo: Msije kuchanganya mambo. Zile little brown envelopes ambazo huitwa "lunch" au " transport" zile ni haki stahili na sio rushwa!. Hizi mimi huwa nasimamia kuhakikisha waandishi wanapatiwa!.
Wale wanaohongwa vyeo vya kisiasa kama tuzo kwa kuwaandikia watu habari za kilaghai unawasemaje Bwana Pasco?
 
ni kweli wanaendesha mashitaka, lakini lazima wapate consent ya dpp, hakuna sheria inayowapa moja kwa moja mamlaka wao kupeleleza kukamata na kushitaki, wao wanapeleleza, wanakamata alafu wanapeleka maombi kwa dpp yanayoambatana na jalada husika kuomba waendeshe shitaka. ukienda pale kwa dpp, majalada yaliyo mengi ni ya kwao...cha ajabu ni kwamba, ni wabovu mno wa prosecution, hata huyo mwandishi wa habari aliyekuwa convicted, ni bahati tu....skills zao za prosecution na uzoefu wao wa kazi ni mdogo sana....kesi zilizo nyingi wanashindwa, na hawataki kuonekana hawajui...hawashauriki hawa jamaa. PCCB pia ni wala rushwa wakubwa mno...
Huo kwenye alama nyekundu ni ushahidi usiosemwa na wengi!
 
Back
Top Bottom