Tarehe 14 June,2012 Mahakama ya hakimu mkazi ya mjini Songea mkoni Ruvuma ilimtia hatiani mwandishi wa habari wa kujitegemea KWIRINUS MAPUNDA kwa kosa la RUSHWA(corruption), ambaye amekuwa akiandikia habari zake katika gazeti la Mwananchi. Baada ya kumtia hatiani(convict) mahakama hiyo ilimpa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela au fine ya Tsh.Milioni moja. PCCB(TAKUKURU)-SONGEA(RUVUMA)ndio waliokuwa wakiiendesha kesi hiyo.