Ruvuma: Jela miaka 60 kwa kosa kubaka na kumpa mimba Mwanafunzi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
3e61792b-c0fa-49e8-8330-43c72934f1f0.jpeg

Mahakama ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma October 18, 2023 imemhukumu kifungo cha Miaka 60 Jela, Faraji Milanzi Yasini, (20), mkulima na mkazi wa Kijiji cha Ruanda - Mkowela Wilayani Tunduru baada ya kupatikana na hatia kwa kosa la Kubaka na kumpa mimba Mwanafunzi wa Darasa la Saba.

Akisoma hukumu hiyo kesi namba 62 ya mwaka 2023 Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Mhe. Kando alisema Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Novemba 10, 2022 huko Kijiji cha Ruanda - Mkowela na kufikishwa mahakamani October 10, 2023 ambapo alipatikana na hatia la makosa hayo.

Mtuhumiwa huyo alitiwa hatiani kwa makosa mawili ya Kubaka chini ya K/F 130 (1)(2) (e) na 131(1) Sheria ya kanuni ya adhabu Sira ya 16 R.E 2022 na kosa la Kumpa mimba mwanafunzi chini ya K/F 60A (1)(3) cha sheria ya Elimu Sura ya 363 iliyofanyiwa marekebisho madogo no. 2 mwaka 2016 na baada ya kutiwa hatia mtuhumiwa alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kila kosa.
 
Hakuna kesi nyepesi na hauwezi kufungwa kwa Africa kaa ya ubakaji japo kesi zote huwezi kufungwa kaa una hela lakini yaubakaji imekaa simple mno kwasisi maskini kwakuwa ina dhamana nanirahisi ukipewa dhamana ukiwa kitaa kuelewana nawenye familia yote kwayote jamaa ndugu walimchoka

R.I.P DITOPILE
 
Hii sio sawa, miezi 6 tu inatosha, maana huyo mwanafunzi unaweza kuta ana miaka 20 na yupo form 6. Hivyo tafsiri ya kubaka inapungua nguvu, maana amekubali mwenyewe kushiriki, japo kisheria bado ni ubakaji.
 
Mahakama ya Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma October 18, 2023 imemhukumu kifungo cha Miaka 60 Jela, Faraji Milanzi Yasini, (20), mkulima na mkazi wa Kijiji cha Ruanda - Mkowela Wilayani Tunduru baada ya kupatikana na hatia kwa kosa la Kubaka na kumpa mimba mwanafunzi.

Akisoma hukumu hiyo kesi namba 62 ya mwaka 2023 Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Mhe. Kando alisema Mahakama imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha na ushahidi uliotolewa pasipo shaka yoyote na kumtia hatiani mtuhumiwa huyo.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Novemba 10, 2022 huko Kijiji cha Ruanda - Mkowela na kufikishwa mahakamani October 10, 2023 ambapo alipatikana na hatia la makosa hayo.

Mtuhumiwa huyo alitiwa hatiani kwa makosa mawili ya Kubaka chini ya K/F 130 (1)(2) (e) na 131(1) Sheria ya kanuni ya adhabu Sira ya 16 R.E 2022 na kosa la Kumpa mimba mwanafunzi chini ya K/F 60A (1)(3) cha sheria ya Elimu Sura ya 363 iliyofanyiwa marekebisho madogo no. 2 mwaka 2016 na baada ya kutiwa hatia mtuhumiwa alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kila kosa.
Mbona umri wa mwanafunzi haujatajwa?
Na je, ni mwanafunzi wa shule ya msingi, sekondari au chuo?

Na je, wamepima DNA kujiridhisha kuwa mimba ni ya mtuhumiwa? Maana kuna mabinti humiliki walaji kadhaa, lakini mimba hubambikia mmoja wao!

Seems kesi imerindima kwa wiki moja tu mtuhumiwa akagaragazwa kwa mvua za hatari !!!

Let's hope hajabambikiziwa!
 
Siku hizi mwanamke unampata mpk Kwa kipande Cha muhogo wa kukaanga inakuwaje unabaka!
hajabaka ila wametongozana tu hao mkuu sema kisheria ndio inasema amebaka na hawajaeleza mwanafunzi ni wa shule ya msngi ,sekondari au vp
 
Bora maelewano kuliko kulea toto usojua tabia za bab’ake sasa ambazo piga ua lazima zirithiiwe huku.

Sasa hapo huyo kahukumiwa huku wazazi mzigo wa matunzo ya mtoto unawasubiri na mjukuu wao

Na jamaa hadi akitoka kesha kuwa mzee tena asiye na mbele wala nyuma ramani hazisomi hata nukta.


Kwangu mimi bora mkaishi pa1 mtajua wenyewe mtakavoishi si mmekuwa watu wazima hadi mkafanya ya wakubwa nyambafu
 
hii sheria ingeangaliwa upya, ni kweli adhabu ziwepo lakini sio kiasi hicho, mvulana mwenyewe bado mdogo sana wala hajui kama kuna kufungwa. sheria iangaliwe upya
 
Back
Top Bottom