Clemence Baraka
JF-Expert Member
- Sep 4, 2012
- 1,694
- 649
Tatizo kiloriti ni sumu inaathiri ubongo.Naanza kumwelewa Tb joshua,aliposema Tanzania bado haijapata rais
Tatizo kiloriti ni sumu inaathiri ubongo.Naanza kumwelewa Tb joshua,aliposema Tanzania bado haijapata rais
Rais John Pombe Magufuli achukizwa na uharibifu na matumizi mabaya ya miundombinu ya mabasi ya mwendo kasi na kuagiza mamlaka zinazohusika ziwachukulie hatua kwa wasiofuata sheria.
Amewataka wachukue magari yao na wapeleke kituoni kisha wachomoe matairi ya watuhumiwa wauze na watakuwa wamepata biashara
Naogopa kuundiwa tume Ila tafuta utapata wakati Sumaye anazungumzia kuhusu kubomoa Jengo la Tanesco Ubungo ambako huyu Bhana Nkuba alitaka kulipiga nyundo akazuiliwa na WazeeHivi alisemaje vile? Naomba kukumbushwa tafadhali.
Naogopa kuundiwa tume Ila tafuta utapata wakati Sumaye anazungumzia kuhusu kubomoa Jengo la Tanesco Ubungo ambako huyu Bhana Nkuba alitaka kulipiga nyundo akazuiliwa na Wazee
Yani uwizi utumike kukomesha makosa ya barabarani?Haya mambo ya sheria na ujinga ujinga ndo yaliotufikisha hapa, undava undava tu kama alivyosema rais ndo nchi hii itanyooka,.. Akienda kituoni anakuta hamna matairi YES next time hawezi rudia tena.. Kumpeleka sijui kwa sheria ni kupoteza muda tuu. Watz wako sugu sana.. Hapa kazi tu.
Ndiyo akili za kushikiwa hizo kwamba mtu akiandika hapa kupinga hizi sera za kukurupuka basi ana stress, wewe ndio wale wale akili fupi. Huyu fisadi kawekwa madarakani na akina Mkapa na Kikwete ili aendelee kuwalinda na maovu yao. Kama CCM ingetaka kiongozi safi basi Augustino Ramadhani alikuwa hana doa lakini Kikwete na Mkapa wakamhofa kwamba yule anaweza kuikubali rasimu ya Warioba na hivyo kuwaondolea kinga Marais waliotenda maovu madarakani.
Iko siku labda hii akili yako iliyofunga itafunguka na kuona Majanga ya huyu dikteta na sera zake za kukurupuka katika miezi saba tu kishaanza kuweweseka mara anataka kwenda chunga ndege, mara anajuta kuchukua form ya Urais na kauli nyingine chungu nzima ambazo zinawaacha midomo wazi Watanzania wengi.
Katiba hamna time nayo maana mnajua ni kiama cha CCM na itapotea rasmi na kubaki history tu.
Yote haya hayatoshi kuwa justification ya ofisi kuu ya taifa kutoa maagizo kwa polisi waibe tairi za watuhumiwa ili kukomesha uzembe barabarani.Nimecheka sana....'kisela' au 'kisera'??????najua unamananisha 'kisela' lakini hawezi kutoa kauli ya aina hiyo...Inaonyesha tu namna Rais anavyochukizwa na tabia ya baadhi yetu watanzania...Ukienda pale kwenye kituo cha DART Ubungo na Kimara, utaona vijana kwenye ngazi zile za kupandia na kushukia wameweka bidhaa zao...kahawa, soda, kashata, bodaboda, baiskeli..na wengine wamelala chini...mpaka abiria wakati mwingine baadhi wanapita kwa wasiwasi mkubwa kwa kuhofia usalama ...vijana wamevaa kapelo wako pale, wanaleta wasiwasi, wengine wanajadili mambo ya Real Madrid, wengine Arsenal, wengine Yanga, wengine 'chura' yaani kelele, mtindo mmoja....Watanzania tuna safari ndefu mno...Yaani vituo vya DART tayari vimegeuzwa vijiwe....
Ujinga hauzoeleki aisee labda hapo Lumumba.MTAZOWEA TUUUUU.....THATS MA PRESIDENT.....WANYOOSHE...
Atakaye iba apigwe mawe, atakaye baka abakwe. Dawa ya wahuni ni wahuni sio?Dawa ya wahuni Ni uhuni, watu wanajisaidia vituoni afanyajee? Hakuna namna nyingine ya kudili na watu walio haribika kama sisi Watanzania
Ni sawa lakini si lazima rais atoe kauli kama hii hadharani. Nchi inaongozwa kwa sheria na si kwa hisia za mtu. Yatosha tu kuagiza wachukuliwe hatua kali kali kali!
your prezdaaNilikuwa nasubiri wanafunzi wa UDOM nao wagome, wangeondoka wote- Rais Magufuli
Tumeleta mradi wa mabasi ya mwendo kasi lakini watu wanajisaidia humo. Mkuu wa Mkoa, Wilaya, Polisi wapo. Wapelekeni wakajisaidie gerezani-Rsis Magufuli
Badala fedha ziende kujenga maabara, madarasa na madawati, zinaenda kuwalipia vilaza.- Rais Magufuli
"Trafiki wakamate magari yanayopita barabara ya magari yaendayo kasi na kutoa matairi na wakihojiwa wajibu, lilikuja bila matairi."-Rais Magufuli
Wewe hata akikuambia ulale masaburi wazi utamuunga mkono 150%Namuunga mkono Magufuli 100%
Yote haya hayatoshi kuwa justification ya ofisi kuu ya taifa kutoa maagizo kwa polisi waibe tairi za watuhumiwa ili kukomesha uzembe barabarani.
KWANI wewe mheshimiwa unamuonajeRais hawezi kutoa tamko la kihuni namna hii labda nape
Sheria ya kufungua tairi za watuhumiwa.Inaleta matumaini kwamba watu wataifuata sheria sasa