Magufuli siyo sawa na Mubarak wala Gadaffi

Magufuli siyo sawa na Mubarak wala Gadaffi

..to be honest with u mimi sijawahi kumfuatilia huyu mwanadada.

..and I am really buffled by ppl who take her seriously.

..huyu dada ana play mind game na watu.

..na leo "dingi" kaingia mzima-mzima kwenye anga za Mange na kutishia kuumiza watu watakaomuunga mkono.

..I think that is exactly what Mange wanted to achieve.
Joka
Where is your logic?
Mange inspires people peaceful
JPM using threats and the barrel of the gun!

Obvious I shall opt for Mange, she has brains!!
 
Hii ishu naona inatrend saana iwe kwenye media mikutanoni,vyombo vya usalama,watawala nk!
Hivi nani katangaza kuwa kutakuwa na maandamano?Lini yatafanyika?Kwa lengo lipi?Wapi yatafanyika?Kisije kikawa aidha mtu au kikundi cha watu kimeamua kutuhamisha kama Taifa kwenye reli kwa ajili ya agenda zao!
 
Mikakati ya hao wanaopanga kuandamana ili hatimaye wamuondoe ikulu rais Magufuli ni mibovu sana.

Huwezi kumlinganisha rais Magufuli na hao akina Mubarak au sijui Gadaffi. Majitu yaliyokaa kwenye madaraka miongo na miongo.

Rais Magufuli kachaguliwa kidemokrasia [hata kama wengine hawakukubaliana na matokeo].

Tena kachaguliwa kihalali.

Rais Magufuli hata miaka mitatu madarakani hajafukisha.

Sasa unapoandaa maandamano yenye lengo la kumpindua, jua hakuna kundi, taasisi, au yeyote yule mwenye akili timamu atakayekuunga mkono.

2020 siyo mbali kivile. Kwa nini usisubiri hadi wakati huo ili umtoe kupitia nguvu ya kura?

Okay, utasema kuwa labda CCM wataiba kura.

Sawa, kama wataiba kura kweli hapo ndipo itakuwa muda muafaka kabisa wa kuitisha maandamano nchi nzima na kupinga yaliyotokea kwenye uchaguzi.

Hapo hata jumuiya ya kimataifa itakuwa na nafasi nzuri ya kukuunga mkono.

Lakini hii ya kupiga makelele mtandaoni na kushindana kumtukana mtu aliyechaguliwa kihalali haitofanikiwa kamwe.

Itaanzania na kuishia mtandaoni tu.

Hivyo shime wote msiompenda Magufuli. Pangeni mikakati mizuri. Acheni kupayuka na kulialia mitandaoni na mjipange ili 2020 ikifika mnamrudisha Chato huyo msiyempenda.
Kwa kilichofanyika juzi Siha na Kinondoni bado unasimama hadharan na kuudanganya umma kuwa alichaguliwa kihalali?
 
Mohamedi Morsi aikuwepo kabla ya Alsisi Misri hakua amekaa miaka mingi, alichaguliwa kihalali, kidemocrasia lkn watu hawakumuelewa wakafanya maandamano wakamtoa na sasa yuko jela....Hivyo issue ya kukaa muda mrefu au kuchaguliwa kidemocrasia sio tatizo...mtu akizingua watu wanahaki ya kupambana nae tu
 
Ndiyo.

Bado naamini kabisa kuwa rais Magufuli yashamshinda.

Naamini kwamba rais Magufuli hana sifa za uongozi wa ki-urais.

Lakini, licha ya mapungufu yake ya kiuongozi bado kuna baadhi ya mambo ambayo nakubaliana naye.

Kwa hiyo msimamo wangu bado uko palepale.

Atakapokosea mahali, basi nitamkosoa kama ambavyo nimeshafanya mara nyingi tu humu [na ushahidi upo].

Nitakapoona kuna mahali kapatia, nitamuunga mkono na kumpa pongezi.

Vivyo hivyo kwa CHADEMA na vyama vingine vya upinzani.

Vikichemsha, nitavichana bila huruma.

Vikipatia, sitokuwa mchoyo wa pongezi.

Jana tu nimetoka kumpongeza Mh. Freeman Mbowe kwa maneno yake ya hekima na busara kwenye taarifa aliyoitoa kuhusu maendeleo ya Tundu Lisu.

Sasa kilicho kigumu hapo kueleweka ni nini?
 
Back
Top Bottom