Magufuli: Nikiondoka watakaokuja wataweza?

Magufuli: Nikiondoka watakaokuja wataweza?

Bora deni likue tu lakini tunaona miradi kama hiyo, kwani hakuna nchi isiyodaiwa waulize USA wana deni kiasi gani kwa wachina.
Ni vizuri ungesoma ni kwa nini China aliikopesha USA,sio kwamba USA alikuwa na shida ya hela mpaka akopeshwe na China na sio kwamba China amemkopesha USA kwa kupenda la hasha ni sababu ya sheria za kiuchumi.
Mwaka ambao China alimkopesha USA in kwamba China alikuwa na over surplus budget-hivyo huwezi kuiacha maana itasababisha matatizo mengine ya kiuchumi lazima ui loan out kwa mwenye riba kubwa ili uweze kupata faida kubwa badaye
 
Hii sasa kaiona kama nchi yake yani hafikirii mtu mwingine kuongoza yeye akiwa hai.
Ninaomba mungu iwe hivyo. Akae sana tupate maendeleo. Hii ndivyo ilikuwa kwa Singapore ilipo mpata kiongozi wake aliyewaletea maendeleo. Alikaa zaidi ya miaka 10. Malaysia vile vile. Nyie mnafuata hao wazungu wanaofadika tukiendelea kuwa masikini. Wanaohusudu na kushangilia viongozi wetu (wa kiAfrica) wakiwa mafisadi. Hao wanawasifia sana na kuwalinda! Hawaandiki mabaya yao kwenye magazeti yao. Tumeisha mpata mkombozi kwanini tumutake afuate mi
 
Eeh Mungu tuonee huruma ili muda wa huyu mzee utakapowadia, akubali kuondoka madarakani kwa mujibu wa katiba. Maana iwapo atajiamulia kututawala milele, hakika kama Taifa tutapoteana! Unatambua fika mtawala wetu huyu hana hulka ya kujali na kuthamini haki za wengine.
 
Raisi Yuko sahihi mtu mwingine akija so lazima aendeleze hayo hayo anayofanya.Mfano kazindua uwanja mpya wa ndege na kanunua ndege anayekuja aweza Sasa fanya kazi ya kuwawezesha watanzania kwa kuwapa ajira wengi , kuongeza mishahara wafanyakazi na Bei za mazao ili watanzania wengi Wawe na Uwezo wa kupanda hizo ndege alizonunua na kuutumia huo uwanja .Pia mwingine akija so lazima ajenge mabarabara yeye aweza kuja na mkakati wa mfano kuondoa ushuru wa magari au kupunguza Kodi ili watanzania wengi waweze kumudu kumiliki magari binafsi mengi watumie kwenye hizo barabara alizojenga.Hospitali na zahanati nyingi aluzijenga mwingine akija so lazima ajenge aweza kipau mbele chake kujaza ajira za madaktari na manesi na madawa kwenye hizo hospitali alizojenga kuhakikisha zinakuwa na madaktari na manesi was kutosha .Uraisi kila moja hufanya kivyake hakuna was KU.kopi kwa mwenzie.Yeye akiondoka anatakiwa ajue kabisa kuwa ajaye nyuma yake SI lazima afanye Kama alivyofanya yeye.Yeye Kama Raisi afanye chake ya mengine akiondoka awaachie wengine.
 
Hii sasa kaiona kama nchi yake yani hafikirii mtu mwingine kuongoza yeye akiwa hai.
Ninaomba mungu iwe hivyo. Akae sana tupate maendeleo. Hii ndivyo ilikuwa kwa Singapore ilipo mpata kiongozi wake aliyewaletea maendeleo. Alikaa zaidi ya miaka 10. Malaysia vile vile. Nyie mnafuata hao wazungu wanaofaidika tukiendelea kuwa masikini. Wanaohusudu na kushangilia viongozi wetu (wa kiAfrica) wakiwa mafisadi. Hao wanawasifia sana na kuwalinda! Hawaandiki mabaya yao kwenye magazeti yao. Tumeisha mpata mkombozi kwanini tumutake afuate mihula miwili? We are shooting ourselves in the feet.
 
Bashite wewe usituzingue.Mi na kwambia ukiongeza hata saa1 ikuku nakukill.
Ninaomba mungu iwe hivyo. Akae sana tupate maendeleo. Hii ndivyo ilikuwa kwa Singapore ilipo mpata kiongozi wake aliyewaletea maendeleo. Alikaa zaidi ya miaka 10. Malaysia vile vile. Nyie mnafuata hao wazungu wanaofaidika tukiendelea kuwa masikini. Wanaohusudu na kushangilia viongozi wetu (wa kiAfrica) wakiwa mafisadi. Hao wanawasifia sana na kuwalinda! Hawaandiki mabaya yao kwenye magazeti yao. Tumeisha mpata mkombozi kwanini tumutake afuate mihula miwili? We are shooting ourselves in the feet.
32604cb3808e4a05a659e5b0bee26d60.jpeg
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] imebidi tu nicheke maana kuna vitu vingine mtu anapofanya au kuongea sijui anakua anafikiria nini, sasa kama yeye anajiona ni bora na ame exist kwanini wengine wasiwepo au ndio ile kujikuta wewe ni bora kuliko wengine
 
Ameshaonja utamu wa madaraka. Kuachia kwake ngazi mmmm. Kuna kitu nyuma ya pazia. Inamaana Watz wote sio Wazalendo isipokuwa yeye pekee?? Kwa imani hiyo imekula kwake kwani Watz sio Wajinga.

Kama neno Umaskini kwake ni Mbaya kisa linatamkwa na Wengine vp Yeye kujinasibu kuwa ni Rais wa Wanyonge yaani Rais wa Watz Masikini?? Yeye ningependa hilo neno kwanzia leo asirudie tena kulitamka. Kwani haiwezekani Serikali anayoiongoza iende kwa Wanyonge kudai KODI kwa mtutu wa Bunduki.
 
Back
Top Bottom