Shida ya nchi hii iko hapo
mtu hana team ya wataalam na kama anayo haisikilizi
Sasa Magufuli hotuba tu ya kuandikiwa haisomi
anazungumza yake...jiulize team ya washauri ya uchumi ataisikiliza?
nimewahi toa mfano humu
Makamu wa Rais wa Marekani sio mtendaji..hafanyi maamuzi
lakini still ana washauri wa kila sekta
unakuta Makamu wa Rais ana mshauri wa uchumi...
Rais ana mshauri wa uchumi na kuna mawaziri husika nao wana washauri...
Sisi Rais anaibuka tu na kusema kitu hata washauri hawana taarifa nacho
Yes, you are right mkuu.
Na labda mimi nitofautiane kidogo na wachangiaji wengi humu.
Nionavyo mimi tatizo liko kwa Mr President na sio kwa waziri wake. Sema tu kwa sbb yeye ndiye mkubwa na ile dhana ya "the boss is always right" ndiyo tatizo.
Muhongo ukiachilia mbali udhaifu wake ule mwingine wa kimaadili (rejea skandali la Tegeta - Escrow Account) pamoja na chuki za kisiasa, kichwani ni mzima zaidi kuliko Magufuli!!
So long as yeye ni Rais (the boss) na kishatamka in a contradicting way, hakuna namna, a mere minister bila kujali weledi wake ataonekana takataka tu!
Otherwise, mimi Profesa Muhongo namkubali sana. Nakumbuka sana, ktk awamu ya nne aliopokuwa waziri wa hii wizara na kabla hajakutwa na dhahama ya Escrrow scandal, upatikanaji wa nishati ya umeme ulikuwa bora kabisa (sijui alikuwa anafanya nini)
Alipoondoka tu, scarcity ya nishati ya umeme ilirudi kwa kasi hadi leo ni mgawo mtindo mmoja!!!
Vinginevyo tunakubaliana kuwa kwa mparanganyiko huu wa misimamo ya viongozi wa serikali ktk sera zozote zile, hakika ni kuchanganya watu wasijue wanaelekea wapi!
Na pia tukumbuke kauli yoyote ya Rais kiongozi mkuu wa nchi iwe nzuri au mbaya, basi, matokeo ni kumwathiri kila mmoja wetu.
Muhongo is better than Magufuli upstairs. Hakurupuki ktk matendo na kauli zake though ana udhaifu wake.....he's too arrogant sometimes!!