COTANGENT
JF-Expert Member
- Nov 24, 2012
- 444
- 243
Kuna kitu wengi hamkukielewa..Alichopinga Magufuli ni mikataba mibovu yote ya dharura ya kuzalisha umeme kama hii ya IPTL, AGRECO, SYMBION e.t.c kwamba shirika lipambani lizalishe umeme wa kutosha.Wale mliomsikia Rais Magufuli alichosema leo kuhusu sera ya nishati ya umeme
mtakubaliana na mimi alichofanya leo Magufuli ni 'kumpinga waziwazi'
waziri wake wa nishati ndugu Muhongo....
nimewahi kuleta thread humu nikiuliza anayoyasema Muhongo ndo aliyotumwa
na Magufuli?Anayoyasema Muhongo katumwa na Magufuli?
Tunaweza kusema sasa kuwa Muhongo alikuwa 'ana sera zake binafsi'
za nishati alizokuwa anazitekeleza na sera za Rais Magufuli ni tofauti
na za Muhongo
Muhongo toka ateuliwe amekuwa anazungumza kuhusu 'wawekezaji binafsi'
kuzalisha umeme na Tanesco kununua tu
akisema ndo solution ya matatizo ya umeme Tanzania
Leo Rais Magufuli kasema hataki kusikia tena biashara za kununua umeme na kukodisha
mitambo na mambo ya mikataba na kampuni binafsi
Tanesco ijiimarishe izalishe yenyewe....
Sasa najiuliza je hii sio confusion now?
why Muhongo aendelee kuwa waziri?
why Magufuli asimteue anaemuona anaelewa sera zake?
Je wawekezaji waliomsikiliza Muhongo waki invest mabilioni wakiwa
na imani kuwa 'muelekeo ni Tanesco kununua tu na si kuzalisha yenyewe si wataingizwa mkenge?
Niseme ingawa binafsi naona Magufuli yuko sahihi kwa hili
lakini hii 'confusion' inaweza leta shida huko mbele....
Kama Muhongo anatofautiana kimtazamo na Rais Magufuli kwenye sera za nishati ni bora
aondoke au aondolewe haraka asije sababisha 'mkanganyiko' huko mbele
Na Rais Magufuli awe very clear na sera ya nishati
tueleweke muelekeo ni upi? ili hata TANESCO nao wajipange huku wakijiamini kuwa
wapo sawa kisera na mkuu wa nchi
Kuliko kuwa na waziri anaewaambia 'wajiandae kuachia uzalishaji'
huku Rais anawaagiza 'wajiimarishe kwenye kuzalisha'
hii confusion ni jipu kubwa
Yapo makampuni binafsi mengi tu kama vile migodi na baadhi ya viwanda vikubwa vya Cement ambavyo huzalisha umeme wao wenyewe either kwa kutumia gas au vyanzo vingine. Tanesco pia huwa na mikataba ya kununua umeme wa ziada toka kwenye viwanda hv kwenda kwenye grid ya Taifa..Sasa hili ndilo Muhongo aliliongelea kwamba company hz ziongezeke na na Tanesco inunue umeme wote surplus toka kwenye hv viwanda