Magufuli na Muhongo, hii sio confusion?

Magufuli na Muhongo, hii sio confusion?

...kwangu mimi credibility ya Muhongo ilipotea tangu wapige escrow....haya mengine yote ni matokeo tu....Nilishangaa sana huyu mtu kuwepo kwenye baraza la JPM...maana hata bunge lilimuhukumu kwenye yale mapendekezo ya bunge dhidi ya wapiga escrow(ikiwemo IPTL)...
...huwa ninajiuliza sana...kama kuna mawaziri kama Tibaijuka waliadhibiwa kwenye escow...ilikuwaje huyu jamaa akapona na hata kurudishwa uwaziri?...mi naona kuna mengi nyuma ya pazia yanafichwa kuhusu huyu jamaa...maana wala hajali kauli zake....mfano wakati ule akiwa kwenye baraza la mkwere alisema wazawa hawana jeuri ya kuwekeza kwenye nishati/gesi....leo akiwa kwenye baraza la JPM anaimba wimbo wa wazawa kuweza kuwekeza kwenye nishati...

...ifike mahali sasa viongozi vigeugeu hawa wasutwe live na bunge...kama mteuzi wao atawakalia kimya....
 
Tatizo ccm wamejichojrea duara lazima wazunguke ndani yake, ukitoka nje ya duara, Kolimba style inakuhusu hakuna jipya la kutegema kwa hawa jamaa.
Kabisa!!! Sijui ni laana au ni nini hata sielewi?
 
Kabisa!!! Sijui ni laana au ni nini hata sielewi?
Himaya ya kuficha maovu yao mkuu wanajuana hawa hakuna asie na kasoro, na kuliko waumbuane ni bora wanyamazishane, ccm ni kama ukoo wa kichawi lazima kurithishana ndumba kizazi hadi kizazi, ukikataa mikoba tu unamalizwa.
 
Magufuri anadhani uprofesa wa Muhongo ndio ufumbuzi wa matatizo ya nishati ya nchi hii,elimu ya Muhongo ni ya shule sio ya kutenda.Muhongo tangu aingie kwenye siasa hana hata miaka 3 lakini amekuwa mpiga siasa kuliko hata Mzee Kingunge,usomi kafungia kabatini kabaki na porojo za kisiasa na mujungu tu
 
Muhongo mnasema ni mtaalam anajua ni vipi tatizo lipo na atumie njia gani kutatua
Magufuli yeye ni kiongoz inawezekana kuna mengine hajui. Usikute Tanesco bado haijawa na uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha
Anyway mimi kwenye swala la MIKATABA namuunga mkono Rais hii MIKATABA ya kijinga ni ya kufutiliwa mbali.. Muhongo atueleze kama Tanesco haina haja ya kupata umeme toka kwa wafanyabiashara basi izalishe yenyewe kama anavotaka mheshimiwa
Hadi lini itakuwa na uwezo?
Kama ni uwezo wa kifedha si waseme kwa baba yao Magufuli awawezeshe .... ???
wacha mambo yenu ya kuedeleza mambo ya kizamani
 
Mawaziri wameshindwa muelewe Magu ni mfuasi wa ujamaa, mawaziri wao wanawaza kibepari,
By the way Magu anahitaji msaada mkubwa wa kisera na fikra,
Hajitambui anataka nini tofauti na majipu

!
!
Anakosa maono.... Vision hana.
 
Mnaosema prof. Muhongo aondolewe mnaongozwa na chuki binafsi ama mnatumika kama toilet papers kwa ulimbukeni wenu. Aondolewe!!!? Halafu uwekwe wewe mbwiga? Kuna wanosema anatumia cv na vyeti vyake kuongoza wizara.....mlitaka atumia makalio yenu?? Ebo!!! Majungu, majungu, majungu kila siku. Jadilini issues....swine!!!
 
Si ndo maana anaanza kusema watu wakamatwe wapelekwe kwenye makambi
kisa wanacheza pool...huku anatoa amri za kupunguza wafanya kazi kwenye mashirika..

yaani akiachwa kila kitu kiende ubongo wake unavyo mtuma...the worst is yet to come...

Guess we need to find him a psychologist cause he is too emotional,yaani kila akilala akiamka anatoa ni contradictions and confusions tu kiasi kwamba watendaji wake hawajui lipi anataka na lipi washike
 
Toa
Wale mliomsikia Rais Magufuli alichosema leo kuhusu sera ya nishati ya umeme
mtakubaliana na mimi alichofanya leo Magufuli ni 'kumpinga waziwazi'
waziri wake wa nishati ndugu Muhongo....

nimewahi kuleta thread humu nikiuliza anayoyasema Muhongo ndo aliyotumwa
na Magufuli?Anayoyasema Muhongo katumwa na Magufuli?

Tunaweza kusema sasa kuwa Muhongo alikuwa 'ana sera zake binafsi'
za nishati alizokuwa anazitekeleza na sera za Rais Magufuli ni tofauti
na za Muhongo

Muhongo toka ateuliwe amekuwa anazungumza kuhusu 'wawekezaji binafsi'
kuzalisha umeme na Tanesco kununua tu

akisema ndo solution ya matatizo ya umeme Tanzania

Leo Rais Magufuli kasema hataki kusikia tena biashara za kununua umeme na kukodisha
mitambo na mambo ya mikataba na kampuni binafsi
Tanesco ijiimarishe izalishe yenyewe....

Sasa najiuliza je hii sio confusion now?
why Muhongo aendelee kuwa waziri?
why Magufuli asimteue anaemuona anaelewa sera zake?

Je wawekezaji waliomsikiliza Muhongo waki invest mabilioni wakiwa
na imani kuwa 'muelekeo ni Tanesco kununua tu na si kuzalisha yenyewe si wataingizwa mkenge?

Niseme ingawa binafsi naona Magufuli yuko sahihi kwa hili
lakini hii 'confusion' inaweza leta shida huko mbele....

Kama Muhongo anatofautiana kimtazamo na Rais Magufuli kwenye sera za nishati ni bora
aondoke au aondolewe haraka asije sababisha 'mkanganyiko' huko mbele

Na Rais Magufuli awe very clear na sera ya nishati
tueleweke muelekeo ni upi? ili hata TANESCO nao wajipange huku wakijiamini kuwa
wapo sawa kisera na mkuu wa nchi
Kuliko kuwa na waziri anaewaambia 'wajiandae kuachia uzalishaji'
huku Rais anawaagiza 'wajiimarishe kwenye kuzalisha'
hii confusion ni jipu kubwa
Soln basi
 
...kwangu mimi credibility ya Muhongo ilipotea tangu wapige escrow....haya mengine yote ni matokeo tu....Nilishangaa sana huyu mtu kuwepo kwenye baraza la JPM...maana hata bunge lilimuhukumu kwenye yale mapendekezo ya bunge dhidi ya wapiga escrow(ikiwemo IPTL)...
...huwa ninajiuliza sana...kama kuna mawaziri kama Tibaijuka waliadhibiwa kwenye escow...ilikuwaje huyu jamaa akapona na hata kurudishwa uwaziri?...mi naona kuna mengi nyuma ya pazia yanafichwa kuhusu huyu jamaa...maana wala hajali kauli zake....mfano wakati ule akiwa kwenye baraza la mkwere alisema wazawa hawana jeuri ya kuwekeza kwenye nishati/gesi....leo akiwa kwenye baraza la JPM anaimba wimbo wa wazawa kuweza kuwekeza kwenye nishati...

...ifike mahali sasa viongozi vigeugeu hawa wasutwe live na bunge...kama mteuzi wao atawakalia kimya....
Halafu si ndiyo huyu inasemekana alimtonya mama wa bandari kuhusu ujio wa WAZIRI MKUU ili aweke mambo sawa?
Mi ninavyoona huyu keshawekewa X tayari? Siamini kama Magufuli anamwamini kwa dhati MTU aliyethubutu kuhujumu ziara ya WAZIRI MKUU!
Kinachosubiriwa ni wakati mwafaka tu wa kutumbua jipu hili! Tuweni na subira!
 
Hiyo confusion is according to your myopic view.prof.muhongo ni jembe.mkoa wa Mara hauwezi kutoa MTU ambaye sio ujembe.hilo ni angalizo
unaongea tu kama mnywa viroba,watu wanajadili kwa upeo wewe unaweka upuuzi usio na mashiko,we rudi kilabuni tu hapa hapakufai.
 
Back
Top Bottom