Magufuli apangua hoja zote za Wabunge

Wadau, namsikiliza kupitia TBC1. Hakika Magufuli amejibu kikamilifu hoja zote za wabunge na kila mmoja ametulia na kuridhika majibu haya. Amesema kuwa ujenzi wa barabara ya Ndundu Somanga itakamilika ndani ya miezi miwili ijayo.

Njia ya mwongo ni fupi. Mwezi July 2014 tutawakumbusha hili suala.
 
Naomba kuuliza kwa ukubwa na umuhimu wa hii wizara wana jengo lao binafsi la ofisi?au ndo wamejazana pale morroco, na kilimo kwanza za kutosha mpaka barabarani?
 
Yaani bilioni 16 za kujenga barabara zetu tunasubiri "Kuwait Fund" ila bilioni 60 za posho bungeni serikali inatoa, tena kiwango cha posho wanasema ni kidogo, kwa siku sabini!

Everything that is wrong with Africa. Mizee mizima na vitambi vyao inakuja EU kuomba hela, wakati wanaowaomba hela wanashindia sandwich kutwa nzima.

Yani maviongozi ya Afrika ni kama yamechuliwa.creativity sifuri, kwao achievement kubwa ni kuomba na kupewa. ukisikiliza bajeti ni msaada, mkopo, msaada, mkopo. hivi na familia zao ndio wanaziendesha hivi? ni lini kutakuwa na fiscal responsibility?

kwa nini maendeleo ya TZ yategemee hisani ya watu wa EU, Uarabuni na Asia? hivi nani aliwahi kutwambia wale watu hawana matatizo yao? hawa waingereza kesho kutwa wanapiga kura ya kujindoa EU, kwani wamechoka kugeuzwa financial beneficiaries,na wazungu wenzao.sasa jiulizeni, kama ndugu zao pua na mdogo, wanawakana, itakuwa sisi tuliopigwa jua la Ikweta karne kwenda, karne rudi?

Viongozi wa Tanzania, ni muda muafaka kubadili mentality zenu za uongozi, kuanziza hapo maendeleo ya dhati (trickel down economy) yataonekana. hii plastic economy mnayoitengeneza ina mwisho wake. Hakuna cha dezo duniani, watakuja kudai vyao siku moja. mjiandae kulipa.
 
Mengi yamesemwa juu ya huyu jamaa mchapa kazi.
Lakini mwisho kabisa ni uzalendo wake kwa Tanzania na watu wake.
Kuna wanao mkebehi na kumwona msanii, lakini kazi inachapwa kwa kwenda mbele.
Wale wanao mkebehi utajua tu kuwa mwisho wa kuona kazi inayofanywa na Mgufuli ni hapa hapa Dar es salaam.
Hawajatembea mikoa yote nchini kuona barabara zinavyojengwa kwa kasi.

Tunajua fika kuwa kazi hii ya kujenga barabara si yake peke yake lakini chini ya usimamizi wake kazi inachapwa kiroho mbaya!
Yote tisa lakini kumi ni msimamo wake wa dhati wa kuwaendeleza wakandarasi wazalendo.
Sijui angekuwa Muhongo wizara ile angesemaje, lakini Watanzania tunaona uzolendo wa kutoka moyoni kwa Magufuli.
 
Namsikiliza mh kessy muda huu kupitia tbc anasema bajeti hii ni ya kulipa madeni na niyakisanii miradi mingi inachelewa sana na serikali inalipa sana tozo unakuta barabara gharama yake ni bilioni 70 lakini kutokana na kuchelewa kwake imradi unaongezeka gharama mpaka kuisha ni bilioni 120
 
Anashangaa mbunge anasifia wizara alafu mwisho anasema jimboni kwake kuna matatizo anaendelea kusema kuwa kuna upendeleo ukubwa wa wazi katika kugawa hela mwambao wa ziwa victoria ni lami tu,kaskazini ni lami tu lakini mwambao wa tanganyika hakuna lami wananchi miaka 50 ya uhuru hawajaona lami!ukimuuliza waziri anasema mkandarasi yuko site!miaka minne hakuna hata kilometa moja kujengwa matokeo yake wachina wanauza kokoto na kuwa waganga wa kienyeji
 
Ujinga wa watanzania ndiyo mtaji wa sisem, hivi kweli usanii wate ule wa magufuli mtu anakuja hapa kumsifia? kweli barabara ya 13km ijengwe ndani ya miezi wiwili? hivi mbonaa tunadanyana sana,
 
Back
Top Bottom