Msimlaumu sana pengine alipokea Urithi mbaya kwa aliemtangulia, inawezekana aliambiwa neno moja tu na yeye amelichukulia vibaya sana. Kama mimi ninaweza kukwambia " hao jamaa usiwachekee sana" ingawa mimi ulikua unaniona nacheka nao kama kawaida. Sasa utakavolipokea wewe inakua tofauti na ili upate sifa hapo ndio panapokuja kuwa kituko. Ninaamini Magufuli amewahi kuonywa kuhusu wapinzani hili kwenye chama chake haliwezi kuepukika lakini anapitiliza na hao waliowahi kumpa maoni yao wanamshanga, na wengine wanaweza kutaka kuiona Tanzania mpya ambayo iliyokuwa haikuwahi kutokea.
Kwa sasa mtangulizi wake ameshamchoka kwa vioja alivomfanyia sizani kama anampa hata dondoo za ushauri, na kwa kawaida yetu waswahili ni watu wa kibri kama mtanielewa, unatamani umuone mwenzako anaanguka ili upate pa kuanzia kulaumu. ni wazo tu binafsi.