Magufuli 'anajihujumu' mwenyewe...

Magufuli 'anajihujumu' mwenyewe...

mie nasubiria hio tarehe moja,nione nani anachukua kombe,nina ugwadu balaaa,naona September mosi mbali vile
Mimi jirani yako hapa usisahau kunipitia....Si tunaanza saa tisa usiku? au ratiba imebadilika?
 
Sijui anataka watu wamwogope...?

Eti yeye hajaribiwi...kwani yeye nani? Mungu?

Keshaanza kuniboa sana kwa kweli.

Badala ya kukimbizana na majizi na mafisadi kabakia kutisha wananchi.
Sasa kama atachukiwa nyie mnaohitaji kupendwa na mafisadi na wazembe si muendelee. Mheshiwa magufuli endelea kujenga inchi hii hawa sasa hivi watabadili gear na kusema wewe ni dhaifu. Hapa kazi tu.
 
Sijui anataka watu wamwogope...?

Eti yeye hajaribiwi...kwani yeye nani? Mungu?

Keshaanza kuniboa sana kwa kweli.

Badala ya kukimbizana na majizi na mafisadi kabakia kutisha wananchi.
Mkuu, heshima kwako.

Usijiamini sana, si unajua kuna "Interpol"

Distance doesn't mater
 
Mimi jirani yako hapa usisahau kunipitia....Si tunaanza saa tisa usiku? au ratiba imebadilika?

hahaaa ole wako ujifungie,hahaaa,aisee Rais wetu atakuwa analala na stress sana siku za hivi karibuni,mkuu rais kama mambo magumu,umeshindwa kuongea na hao ukuta,call state of emergency u resign.....
 
Huyu Magufuli mimi simwelewi kabisa siku hizi.

Alipoanza kuna baadhi ya mambo nilimuunga mkono.

Lakini sasa hivi naona haeleweki kabisa.

Bada ya kupiga kazi tu anaishia kukimbizana na CHADEMA.

Tatizo lake ni nini?

Hana ustahmilizu wa kukosolewa?
Siyo wewe tu uliyekuwa na imani na JPM wakati alipoanza kazi ya Urais, hakika wengi tulikuwa na imani naye kwa kiasi fulani.....

Lakini kadri siku zinavyosogea ndivyo anavypoteza popularity kwa kasi ya kutisha......

Na kitu kikubwa kinachomponza sana Magu ni kutofanya 'editing' ya matamko yake anayotoa kwenye majukwaa ya kisiasa kutokana na kukataa kusoma hotuba anazoandaliwa na wasaidizi wake.

Ninaamini iwapo kura ya maoni itapigwa leo kutaka kujua ni wananchi wangapi wanamuunga mkono hivi sasa.

Upo uwezekano akawa anaungwa mkono na chini ya asilimia 30 ya watanzania kwa hivi sasa, na atakuwa amepoteza umaarufu wake kutokana na kutaka kuendesha nchi hii bila kufuata Katiba ya
nchi na Sheria nyinginezo mbalimbali za nchi.
 
Siyo wewe tu uliyekuwa na imani na JPM wakati alipoanza kazi ya Urais, hakika wengi tulikuwa na imani naye kwa kiasi fulani.....

Lakini kadri siku zinavyosogea ndivyo anavypoteza popularity kwa kasi ya kutisha......

Na kitu kikubwa kinachomponza sana Magu ni kutofanya 'editing' ya matamko yake anayotoa kwenye majukwaa ya kisiasa kutokana na kukataa kusoma hotuba anazoandaliwa na wasaidizi wake.

Ninaamini iwapo kura ya maoni itapigwa leo kutaka kujua ni wananchi wangapi wanamuunga mkono hivi sasa.

Upo uwezekano akawa anaungwa mkono na chini ya asilimia 30 ya watanzania kwa hivi sasa, na atakuwa amepoteza umaarufu wake kutokana na kutaka kuendesha nchi hii bila kufuata Katiba ya
nchi na Sheria nyinginezo mbalimbali za nchi.

Nakumbuka hapa JF ilikuwa ukianzisha thread ya kumkosoa unapingwa na wengi
sasa hali imegeuka...

Waliomzunguka wanamdanganya
 
Mbio za Marathon ni bora uanze taratibu kasi iongezeke katikati ya mbio.

Lakini sio uanze na kasi kubwa, automatic kasi yako itapungua katika ya mbio na hakika utamaliza vibaya.

Huyu Mwanariadha wetu hata robo ya mbio hajafika tayari ameshachoka na kupoteza mvuto katika Marathon ya 2015-2020.

Je ataweza kumaliza salama mbio zake? Yetu macho!!
 
Huyu Magufuli mimi simwelewi kabisa siku hizi.

Alipoanza kuna baadhi ya mambo nilimuunga mkono.

Lakini sasa hivi naona haeleweki kabisa.

Bada ya kupiga kazi tu anaishia kukimbizana na CHADEMA.

Tatizo lake ni nini?

Hana ustahmilizu wa kukosolewa?
Kweli kwa kasi aliyoanza nayo alisha gain political mileage ya kutosha tu kiasi hata asingewabana UKAWA bado alikua ana advantage. Hiki anachofanya sasa hata mie sikielewi aisee
 
Kuna vitu Rais yoyote akifanya ni rahisi mno kutengeneza maadui wapya weengi mno

La kwanza ni kuongeza kodi

la pili ni kupiga marufuku 'watu wasiongee'

Kiongozi yoyote akifanya hayo ni dhahiri upepo utabadilika na 'atachukiwa'
haraka mno.....

Huhitaji hata vyama vya siasa kubadili huo upepo

Sasa kama kuna watu wa kumshauri Magufuli....basi wamueleze tu ukweli

Kwanza awe makini na kupandisha kodi

kodi na tozo za biashara mbalimbali zimepandishwa kiholela

na sasa watu hawaruhusiwi hata kufanya mikutano
wala makongamano
wala kukosoa kwenye media........hivi vitu viwili vinaweza kufanya serikali
kutumia 'Jeshi la Polisi' kila siku na kila wakati.....

Kuna gharama kubwa mno serikali itaingia...ili kuimarisha jeshi la polisi
na kuliweka ready kila siku...kwa mambo ambayo busara kidogo ingetumika
kusingekuwa na ulazima.......
Busara ni bidhaa adimu kwa viongozi Wa awamu hii, nitajie Kama unamjua mwenye busara Kati yao
 
Kweli kwa kasi aliyoanza nayo alisha gain political mileage ya kutosha tu kiasi hata asingewabana UKAWA bado alikua ana advantage. Hiki anachofanya sasa hata mie sikielewi aisee

Watu wenye mentality za 'kufanya harakati' badala ya management ndo wanavyokuwa
lazima wajiangushe wenyewe

Harakati ni kabla hujapata power
ukishapata power inatakiwa management skills sio tena 'harakati'
 
Back
Top Bottom